Advertise with Us

Advertise with Us

DHall

DHall

Pages

November 22, 2013

Breaking News: Zitto na Kitila wavuliwa vyeo vyote ndani ya (CHADEMA)!

  
Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Zitto Zuberi Kabwe
  
Dk. Kitila Mkumbo Mjumbe wa kamati kuu (CHADEMA)

Habari zilizoifikia Blog ya Maisha Times zinaripoti kwamba Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Zitto Zuberi Kabwe na Dk. Kitila Mkumbo ambaye ni Mjumbe wa kamati kuu wote wamevuliwa vyeo vyao vyote walivyonavyo ndani ya chama (CHADEMA) 

Habari kutoka katika chanzo chetu zinaeleza, nanukuu "Kikao cha Kamati Kuu ndiyo kimeisha muda huu, na taarifa zilizopo ni kwamba kambi ya PM7 imevunjwa rasmi baada ya viongozi wake kuvuliwa vyeo vyote walivyo navyo ndani ya chama.

Waliovuliwa vyeo ni Zitto Kabwe, ambaye amevuliwa nafasi ya Naibu Katibu Mkuu wa chama pamoja na nafasi ya Naibu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni. Dr. Kitila Mkumbo yeye amevuliwa nafasi ya mjumbe wa kamati kuu.

Kamati Kuu imewaandikia barua Zitto na Kitila, wajieleze ndani ya siku 14 kwanini wasifukuzwe uanachama".

No comments:

Post a Comment