Advertise with Us

Advertise with Us

DHall

DHall

Pages

August 19, 2014

Tetesi: Aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya/jimbo la TMK kukabidhiwa kadi ya CCM kwa mbwembwe!

Bwn. Patrick Yohana Joseph

Tetesi ambazo Blog ya Maisha Times imezipata muda mfupi uliopita zinarepoti kwamba aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya/jimbo Temeke, Mwenyekiti BAVICHA mkoa wa Temeke, Mjumbe wa Baraza Kuu la Chadema Taifa, Mjumbe wa mkutano mkuu wa Chadema Taifa ambaye alivuliwa na kufukuzwa uanachama wa chama hicho kutokana na usaliti na hujuma Bwn. Patrick Yohana Joseph anatarajia kujiunga na Chama Cha Mapinduzi hapo mnamo tarehe 28/08/2014 ambapo atakabidhiwa rasmi Kadi ya CCM na Kiongozi Mkubwa kitaifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa mbwembwe za kila namna kama ilivyokuwa kwa Mtela Mwampamba, Juliana Shonza na Madiwani wa Shinyanga ambao walifukuzwa CHADEMA na kuonekana ni almasi ndani ya CCM.

Tetesi zaidi zinadai kwamba mbwembwe na kila ambacho kitafanyika katika siku hiyo lengo kubwa likiwa ni kutumia kiasi kikubwa cha fedha kuwahamasisha wanachama wengi wa CHADEMA kujiunga na CCM ili kukidhoofisha chama hicho pendwa na wananchi walio wengi ambacho kwa miaka kadhaa kimekuwa kikikipa changamoto kubwa chama tawala CCM katika medani ya siasa!

No comments:

Post a Comment