Advertise with Us

Advertise with Us

DHall

DHall

Pages

June 4, 2013

RASIMU YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 2013


TAARIFA

Toleo la Rasimu ya Katiba limechapishwa kwenye Gazeti la Serikali kwa
mujibu wa kifungu cha 18(5) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya
83, kwa madhumuni ya kuwepo kwa wananchi kusoma na kutoa maoni zaidi
kwa Tume kuhusu maudhui yaliyomo kwenye Rasimu ya Katiba.
Dar es Salaam, JOSEPH S. WARIOBA,
3 Juni, 2013 Mwenyekiti wa Tume
ii
RASIMU YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA
TANZANIA YA MWAKA 2013
________
YALIYOMO
______
Ibara Kichwa cha Habari
UTANGULIZI
SURA YA KWANZA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SEHEMU YA KWANZA
MIPAKA, ALAMA, LUGHA, UTAMADUNI NA TUNU ZA TAIFA
1. Jamhuri ya Muungano
2. Eneo la Jamhuri ya Muungano
3. Alama na Siku Kuu za Taifa
4. Lugha ya Taifa na lugha za alama
5. Tunu za Taifa
SEHEMU YA PILI
MAMLAKA YA WANANCHI, UTII NA HIFADHI YA KATIBA
6. Mamlaka ya wananchi
7. Watu na Serikali
8. Mamlaka na utii wa Katiba
9. Hifadhi ya Katiba
SURA YA PILI
MALENGO MUHIMU, MISINGI YA MWELEKEO WA
SHUGHULI ZA SERIKALI NA SERA ZA KITAIFA
10. Utekelezaji wa malengo ya Taifa
11. Malengo Makuu
12. Sera kuhusu Mambo ya Nje
SURA YA TATU
MAADILI NA MIIKO YA UONGOZI WA UMMA
SEHEMU YA KWANZA
MAADILI YA UONGOZI WA UMMA
13. Dhamana ya Uongozi wa Umma
iii
14. Kanuni za Uongozi wa Umma
15. Zawadi katika Utumishi wa Umma
16. Wajibu wa kutangaza mali na madeni
17. Mgongano wa kimaslahi
18. Matumizi ya mali ya umma
19. Matumizi ya masharti ya maadili kwa watumishi wa umma
SEHEMU YA PILI
MIIKO YA UONGOZI WA UMMA
20. Utii wa Miiko ya Uongozi wa Umma
21. Marufuku kwa baadhi ya vitendo
SURA YA NNE
HAKI ZA BINADAMU, WAJIBU WA RAIA NA MAMLAKA ZA NCHI
SEHEMU YA KWANZA
HAKI ZA BINADAMU
22. Uhuru, utu na usawa wa binadamu
23. Haki ya kuwa hai
24. Marufuku kuhusu ubaguzi
25. Haki ya kutokuwa mtumwa
26. Uhuru wa mtu binafsi
27. Haki ya faragha na usalama wa mtu
28. Uhuru wa mtu kwenda anakotaka
29. Uhuru wa maoni
30. Uhuru wa habari na vyombo vya habari
31. Uhuru wa imani ya dini
32. Uhuru wa watu kujumuika na kushirikiana na wengine
33. Uhuru wa kushiriki shughuli za umma
34. Haki ya kufanya kazi
35. Haki za wafanyakazi na waajiri
36. Haki ya kumiliki mali
37. Haki ya uraia
38. Haki ya mtuhumiwa na mfungwa
39. Haki ya watu walio chini ya ulinzi
40. Uhuru na haki ya mazingira safi na salama
41. Haki ya elimu na kujifunza
42. Haki ya mtoto
43. Haki na wajibu wa vijana
44. Haki za watu wenye ulemavu
45. Haki za makundi madogo katika jamii
46. Haki za wanawake
47. Haki za wazee
iv
SEHEMU YA PILI
WAJIBU WA RAIA NA MAMLAKA ZA NCHI
(a) Wajibu wa Raia kwa Taifa
48. Wajibu wa kushiriki kazi
49. Ulinzi wa mali ya umma
50. Haki na wajibu muhimu
(b) Wajibu wa Mamlaka za Nchi
51. Hifadhi ya haki za binadamu
52. Usimamizi wa haki za binadamu
53. Mipaka ya haki za binadamu
SURA YA TANO
URAIA KATIKA JAMHURI YA MUUNGANO
SURA YA SITA
MUUNDO WA JAMHURI YA MUUNGANO
57. Muundo wa Muungano
58. Vyombo vya utendaji vya Jamhuri ya Muungano
59. Mamlaka ya Serikali ya Muungano
60. Mambo ya Muungano
61. Washirika wa Muungano
62. Mamlaka ya Washirika wa Muungano
63. Mahusiano kati ya Washirika wa Muungano
64. Mawaziri Wakaazi
65. Mamlaka ya wananchi
66. Wajibu wa kulinda Muungano
SURA YA SABA
SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO
SEHEMU YA KWANZA
SERIKALI, RAIS NA MAKAMU WA RAIS
(a) Serikali
67. Serikali ya Jamhuri ya Muungano
54. Uraia wa Jamhuri ya Muungano
55. Uraia wa kuzaliwa
56. Uraia wa kuandikishwa
v
(b) Rais
68. Rais wa Jamhuri ya Muungano
69. Madaraka na majukumu ya Rais
70. Utekelezaji wa madaraka ya Rais
71. Rais kuzingatia ushauri
72. Rais kushindwa kumudu majukumu yake
73. Utekelezaji wa majukumu ya Rais akiwa hayupo
(c) Uchaguzi wa Rais
74. Uchaguzi wa Rais
75. Sifa za Rais
76. Haki ya kuchaguliwa tena
77. Utaratibu wa Uchaguzi wa Rais
78. Malalamiko kuhusu uhalali wa uchaguzi wa Urais
79. Kiapo cha Rais
(d) Masharti Mahsusi kuhusu Mamlaka ya Rais
80. Madaraka ya kutangaza vita
81. Madaraka ya Rais kutangaza hali ya hatari
82. Mamlaka ya Rais kutoa msamaha
83. Kinga dhidi ya mashtaka ya Rais
84. Bunge kumshtaki Rais
85. Maslahi ya Rais
(e) Makamu wa Rais
86. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano
87. Upatikanaji wa Makamu wa Rais
88. Sifa za Makamu wa Rais
89. Kiapo cha Makamu wa Rais
90. Wakati wa Makamu wa Rais kushika madaraka
91. Bunge kumuondoa Makamu wa Rais
SEHEMU YA PILI
BARAZA LA MAWAZIRI LA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO
(a) Baraza la Mawaziri
92. Kuundwa kwa Baraza la Mawaziri
93. Uteuzi wa Mawaziri na Naibu Mawaziri
94. Sifa za Mawaziri na Naibu Mawaziri
95. Kiapo, muda na masharti ya kazi ya Waziri na Naibu Waziri
96. Utekelezaji wa shughuli za Serikali Bungeni
vi
(b) Mwanasheria Mkuu wa Serikali
97. Mwanasheria Mkuu wa Serikali
(c) Katibu Mkuu Kiongozi na Makatibu Wakuu
98. Katibu Mkuu Kiongozi
99. Makatibu Wakuu
(d) Utendaji Kazi wa Baraza la Mawaziri
100. Kamati Maalumu ya Makatibu Wakuu
101. Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri
SURA YA NANE
URATIBU WA MAHUSIANO YA WASHIRIKA WA MUUNGANO
102. Tume ya Mahusiano ya Uratibu wa Serikali
103. Malengo ya Tume
104. Majukumu ya Tume
SURA YA TISA
BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO
SEHEMU YA KWANZA
KUUNDWA KWA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO
105. Bunge la Jamhuri ya Muungano
106. Muda wa Bunge
107. Madaraka ya Bunge
108. Mipaka ya Bunge katika kutumia madaraka yake
109. Madaraka ya Bunge kutunga sheria
110. Utaratibu wa kutunga sheria
111. Utaratibu wa kubadilisha Katiba hii na baadhi ya sheria
112. Utaratibu wa kubadilisha masharti mahususi
113. Utaratibu wa kutunga sheria kuhusu mambo ya fedha
114. Madaraka ya Mkuu wa Nchi kuhusu Muswada wa Sheria
115. Kupitishwa kwa hoja za Serikali
SEHEMU YA PILI
WABUNGE
(a) Uchaguzi wa Wabunge
116. Uchaguzi wa Wabunge
117. Sifa za kuchaguliwa kuwa Mbunge
118. Watu wenye Madaraka Serikalini kukoma utumishi
119. Utaratibu wa uchaguzi wa Wabunge
120. Kiapo cha Wabunge
121. Masharti ya kazi ya Wabunge
vii
122. Muda wa Wabunge kushika madaraka
123. Uwajibikaji wa Wabunge
124. Haki ya wapiga kura kumwajibisha Mbunge.
125. Uamuzi wa suala kama mtu ni Mbunge
126. Tamko Rasmi la Wabunge kuhusu Maadili ya Viongozi
127. Wabunge kutoa taarifa ya mali
SEHEMU YA TATU
UONGOZI WA BUNGE
(a) Spika na Naibu Spika
128. Spika na mamlaka yake
129. Ukomo wa mamlaka ya Bunge
130. Naibu Spika
131. Utaratibu wa kumchagua Spika na Naibu Spika
132. Sifa za mtu anayefaa kuchaguliwa kuwa Spika au Naibu Spika.
(b) Ofisi ya Bunge
133. Katibu wa Bunge
134. Sekretarieti ya Bunge
SEHEMU YA NNE
UTARATIBU WA SHUGHULI BUNGENI
135. Kanuni za Kudumu za Bunge
136. Rais kulihutubia Bunge
137. Mikutano ya Bunge
138. Uongozi na vikao vya Bunge
139. Akidi ya vikao vya Bunge.
140. Kamati za Bunge
SEHEMU YA TANO
MADARAKA NA HAKI ZA BUNGE
141. Uhuru wa majadiliano Bungeni
142. Mipaka ya majadiliano Bungeni
SURA YA KUMI
MAHAKAMA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SEHEMU YA KWANZA
MISINGI YA UTOAJI HAKI NA UHURU WA MAHAKAMA
143. Kuanzishwa kwa Mahakama ya Tanzania
144. Misingi ya utoaji haki
145. Uhuru wa Mahakama
viii
SEHEMU YA PILI
MUUNDO WA MAHAKAMA
(a) Mahakama za Jamhuri ya Muungano
146. Muundo wa Mahakama
(b) Mahakama ya Juu ya Jamhuri ya Muungano
147. Mahakama ya Juu
148. Akidi ya vikao vya Mahakama ya Juu
149. Madaraka ya Mahakama ya Juu
150. Madaraka ya Majaji wa Mahakama ya Juu
(c) Uteuzi wa Majaji wa Mahakama ya Juu
151. Uteuzi wa Jaji Mkuu
152. Uteuzi wa Naibu Jaji Mkuu
153. Uteuzi wa Majaji wa Mahakama ya Juu
154. Kiapo cha Majaji wa Mahakama ya Juu
155. Muda wa kuwa madarakani kwa Jaji Mkuu, Naibu Jaji Mkuu na Majaji wengine
156. Utaratibu wa kukaimu katika Mahakama ya Juu
157. Utaratibu wa kushughulikia nidhamu ya Majaji wa Mahakama ya Juu
(d)Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano
158. Mahakama ya Rufani
159. Akidi ya vikao vya Mahakama ya Rufani
160. Mamlaka ya Mahakama ya Rufani
161. Mamlaka ya Majaji wa Mahakama ya Rufani
(e)Uteuzi wa Majaji wa Mahakama ya Rufani
162. Uteuzi wa Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani
163. Uteuzi wa Majaji wa Mahakama ya Rufani
164. Kiapo cha Majaji wa Mahakama ya Rufani
165. Muda wa kuwa madarakani kwa Mwenyekiti na Majaji wengine wa Mahakama
ya Rufani
166. Utaratibu wa kukaimu katika Mahakama ya Rufani
167. Utaratibu wa kushughulikia nidhamu ya Majaji wa Mahakama ya Rufani
(f)Usimamizi wa Shughuli za Mahakama
168. Msajili wa Mahakama
169. Majukumu ya Msajili wa Mahakama
170. Mtendaji Mkuu wa Mahakama
171. Majukumu ya Mtendaji Mkuu wa Mahakama
ix
SEHEMU YA TATU
TUME YA UTUMISHI WA MAHAKAMA NA MFUKO WA MAHAKAMA
(a) Tume ya Utumishi wa Mahakama
172. Tume ya Utumishi wa Mahakama
173. Majukumu ya Tume ya Utumishi wa Mahakama
174. Uanachama katika vyama vya siasa
(b) Mfuko wa Mahakama
175. Mfuko wa Mahakama
SURA YA KUMI NA MOJA
UTUMISHI KATIKA JAMHURI YA MUUNGANO
176. Misingi mikuu ya Utumishi wa Umma
177. Masharti kuhusu utumishi katika Jamhuri ya Muungano
178. Tume ya Utumishi wa Umma
179. Mamlaka na majukumu ya Tume
SURA YA KUMI NA MBILI
UCHAGUZI KATIKA VYOMBO VYA UWAKILISHI
NA VYAMA VYA SIASA
SEHEMU YA KWANZA
UWAKILISHI WA WANANCHI
180. Ushiriki katika vyombo vya uwakilishi
SEHEMU YA PILI
TUME HURU YA UCHAGUZI
(a) Muundo wa Tume Huru yaUchaguzi
181. Kuundwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi
182. Kamati ya Uteuzi
183. Ukomo wa kushika madaraka ya Ujumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi
184. Wajibu wa Tume Huru ya Uchaguzi
185. Malalamiko kuhusu uchaguzi
(b) Vyama vya Siasa
186. Vyama vya siasa
(c) Mkurugenzi wa Uchaguzi na Msajili wa Vyama vya Siasa
187. Utekelezaji wa majukumu ya Tume Huru ya Uchaguzi
x
SURA YA KUMI NA TATU
TAASISI ZA UWAJIBIKAJI
SEHEMU YA KWANZA
TUME YA MAADILI YA UONGOZI NA UWAJIBIKAJI
188. Tume ya Maadili ya Uongozi na Uwajibikaji
189. Majukumu ya jumla ya Tume
190. Muda wa kukaa madarakani wa Wajumbe wa Tume
191. Kuondolewa madarani kwa Wajumbe wa Tume
192. Uhuru wa Tume
193. Uwezeshaji wa nyenzo na rasilimali
SEHEMU YA PILI
TUME YA HAKI ZA BINADAMU
194. Tume ya Haki za Binadamu
195. Kazi na majukumu ya Tume
196. Muda wa kukaa madarakani wa Wajumbe wa Tume
197. Kuondolewa madarani kwa Wajumbe wa Tume
198. Uhuru wa Tume
199. Uwezeshaji wa nyenzo na rasilimali
SEHEMU YA TATU
MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI
200. Uteuzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
201. Sifa za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
202. Kazi na majukumu yake
203. Muda wa kukaa madarakani
204. Kuondolewa madarakani
205. Uwezeshaji wa nyezo na rasilimali
SURA YAKUMI NA NNE
MASHARTI KUHUSU FEDHA ZA JAMHURI YA MUUNGANO
(a) Mfuko Mkuu wa Hazina na Fedha za
Jamhuri ya Muungano
206. Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano
207. Masharti ya kutoa fedha za matumizi katika Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali
208. Utaratibu wa kuidhinisha matumizi ya fedha zilizomo katika Mfuko Mkuu wa
Hazina ya Serikali
209. Utaratibu wa kuidhinisha matumizi ya fedha kabla ya Sheria ya Matumizi ya
Fedha za Serikali kuanza kutumika
210. Mfuko wa matumizi ya dharura
211. Mishahara ya baadhi ya watumishi kudhaminiwa na Mfuko Mkuu
xi
(b) Deni la Taifa na Mikopo ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano
212. Deni la Taifa
213. Mamlaka ya kukopa ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano
214. Mamlaka ya Kukopa fedha kwa Serikali za Washirika wa Muungano
(c) Vyanzo vya Mapato ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano
215. Vyanzo vya mapato vya Serikali ya Jamhuri ya Muungano
216. Manunuzi ya umma
(d) Benki Kuu
217. Benki Kuu ya Jamhuri ya Muungano
218. Benki za Serikali za Washirika
SURA YA KUMI NA TANO
ULINZI NA USALAMA KATIKA JAMHURI YA MUUNGANO
(a) Ulinzi na Usalama wa Taifa
219. Usalama wa Taifa
220. Taasisi za ulinzi na usalama wa Taifa
221. Kuanzishwa kwa Baraza la Ulinzi na Usalama la Taifa
222. Majukumu ya Baraza la Ulinzi na Usalama la Taifa
(b)Jeshi la Wananchi wa Tanzania
223. Kuanzishwa kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania
224. Uteuzi wa Mkuu wa Majeshi
225. Madaraka ya Amiri Jeshi Mkuu
226. Tume ya Utumishi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania
(b) Polisi wa Jamhuri ya Muungano
227. Jeshi la Polisi wa Tanzania
228. Misingi ya utendaji wa Jeshi la Polisi
229. Uteuzi wa Mkuu wa Jeshi la Polisi
230. Majukumu na uhuru wa Mkuu wa Jeshi la Polisi
231. Tume ya Utumishi wa Jeshi la Polisi
232. Polisi wa Washirika wa Muungano
(e) Idara ya Usalama ya Jamhuri ya Muungano
233. Kuanzishwa kwa Idara ya Usalama ya Taifa
234. Uteuzi wa Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa
235. Usalama wa Washirika wa Muungano
xii
______
NYONGEZA
_______
SURA YA KUMI NA SITA
MENGINEYO
236. Masharti kuhusu utaratibu wa kukabidhi madaraka
237. Masharti kuhusu madaraka ya kazi
238. Ufafanuzi
239. Jina la Katiba na kuanza kutumika
240. Kufutwa kwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Mwaka 1977
1
UTANGULIZI
KWA KUWA, Sisi, Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua
rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayoheshimu na kuzingatia misingi ya
utu, uhuru, haki, usawa, udugu, amani, umoja na mshikamano katika nyanja zote za
maisha yetu;
NA KWA KUWA, tunaamini kuwa misingi hiyo inaweza tu kutekelezwa katika
jamii yenye mfumo wa demokrasia na utawala bora ambayo Serikali yake inasimamiwa
na Bunge lenye Wabunge waliochaguliwa na wanaowawakilisha wananchi na Mahakama
huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na
kuhakikisha kuwa haki za binadamu zinalindwa na kudumishwa na kwamba wajibu wa
kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu;
NA KWA KUWA, umuhimu wa kutunza mali ya Mamlaka za Nchi na ya pamoja,
kupiga vita aina zote za uharibifu, ubadhilifu, na kuhimiza matumizi bora na endelevu ya
rasilimali na maliasili zetu pamoja na kulinda na kuhifadhi mazingira yetu kwa
mustakabali wa maisha ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo;
NA KWA KUWA, umuhimu na faida za kujenga, kukuza na kuendeleza, amani,
umoja, urafiki na ushirikiano miongoni mwa Watanzania, Mataifa mbalimbali ya Afrika
na Dunia kwa ujumla;
KWA KUWA, azma ya kujenga Umoja wa Bara la Afrika katika misingi ya
Umajimui wa Afrika ambao inadhihirishwa na Muungano wa iliyokuwa Jamhuri ya
Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar;
NA KWA KUENDELEZA, dhamira yetu hiyo ni muhimu:
(a) kulinda, kuimarisha na kuudumisha Muungano wa nchi za Jamhuri ya
Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar;
(b) kujenga Taifa huru na linalojitegemea;
(c) kuimarisha na kuendeleza utawala wa sheria;
(d) kukuza na kuendeleza maadili, uwajibikaji na uwazi;
(e) kujenga umoja na mshikamano utakaowezesha kutimiza malengo ya kisiasa,
kiuchumi, kijamii, kimazingira na kulinda urithi kwa ujumla;
(f) kujenga na kuendeleza ukuu wa mamlaka ya watu;
(g) kujenga na kuendeleza utii wa mamlaka ya Katiba; na
(h) kuimarisha na kudumisha uzalendo kwa Taifa miongoni mwa Watanzania;
NA KWA KUZINGATIA, urithi tulioachiwa na Waasisi wa Taifa letu wa kujenga
nchi yenye Umoja wa Watu wake ambao hawabaguani kwa misingi ya ukabila, udini,
rangi, jinsi au ubaguzi wa aina nyingine yoyote;
NA KWA KUZINGATIA, uzoefu wa zaidi ya Miaka Hamsini ya Uhuru na Miaka
Hamsini ya Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na
umuhimu wa ushiriki mpana na bayana wa wananchi katika utungaji wa Katiba ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
2
HIVYO BASI, KATIBA HII YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
ILIYOPENDEKEZWA NA BUNGE MAALUM LA KATIBA imetungwa na SISI
WANANCHI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA kupitia KURA
YA MAONI kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na kuhakikisha kuwa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia
na utawala wa sheria, kujitegemea na isiyokuwa na dini.
‐ 3 ‐
SURA YA KWANZA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SEHEMU YA KWANZA
MIPAKA, ALAMA, LUGHA, UTAMADUNI NA TUNU ZA TAIFA
Jamhuri ya
Muungano 1.-(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Shirikisho lenye
mamlaka kamili ambayo imetokana na Muungano wa nchi mbili za
Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ambazo kabla
ya Hati za Makubaliano ya Muungano ya mwaka 1964 zilikuwa nchi
huru.
(2) Jamhuri ya Muungano ni Shirikisho la kidemokrasia
linalofuata mfumo wa vyama vingi vya siasa, usawa wa binadamu,
kujitegemea, utawala wa sheria na kuheshimu haki za binadamu.
(3) Hati ya Makubaliano ya Muungano iliyorejewa katika Ibara
ndogo ya (1), ndio msingi mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
na Katiba hii, kwa kadri itakavyorekebishwa, itakuwa ni mwendelezo wa
Makubaliano hayo.
Eneo la
Jamhuri ya
Muungano
2. Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara
ikijumuisha sehemu yake ya bahari na eneo lote la Zanzibar ikijumuisha
sehemu yake ya bahari.
Alama na Siku
Kuu za Taifa 3.-(1) Alama za Taifa ni:
(a) Bendera ya Taifa;
(b) Wimbo wa Taifa; na
(c) Nembo ya Taifa,
kama zitakavyoainishwa katika sheria itakayotungwa na Bunge.
(2) Siku Kuu za Kitaifa zitakuwa ni:
(a) Siku ya Uhuru wa Tanganyika, itakayoadhimishwa tarehe 9
Disemba;
(b) Siku ya Mapinduzi ya Zanzibar, itakayoadhimishwa tarehe 12
Januari;
(c) Siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,
itakayoadhimishwa tarehe 26 Aprili; na
(d) Siku Kuu nyingine zitakazoainishwa na sheria za nchi.
(3) Kila Siku Kuu ya Kitaifa itakuwa ni siku ya mapumziko.
Lugha ya Taifa
na lugha za
alama
4.-(1) Lugha ya Taifa ya Jamhuri ya Muungano ni Kiswahili na
itatumika katika mawasiliano rasmi ya kitaifa na kiserikali.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), lugha ya
Kiingereza inaweza kutumika kuwa lugha rasmi ya mawasiliano ya
kiserikali pale itakapohitajika.
(3) Serikali itaweka mazingira yatakayowezesha kuwepo kwa
mawasiliano ya lugha mbadala zikiwemo lugha za alama na nukta nundu
kwenye sehemu muhimu za umma na katika vyombo vya habari
vinavyotangaza habari zake kitaifa kwa ajili ya watu wenye mahitaji
maalum.
‐ 4 ‐
Tunu za Taifa 5. Jamhuri ya Muungano itaenzi na kuzingatia Tunu za Taifa
zifuatazo:
(a) utu;
(b) uzalendo;
(c) uadilifu;
(d) umoja;
(e) uwazi;
(f) uwajibikaji; na
(g) lugha ya Taifa.
SEHEMU YA PILI
MAMLAKA YA WANANCHI, UTII NA HIFADHI YA KATIBA
Mamlaka ya
wananchi 6. Jamhuri ya Muungano ni nchi inayofuata misingi ya
demokrasia inayozingatia haki ya kijamii, na kwa hiyo:
(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka za nchi, na Serikali
itapata madaraka na mamlaka yake kutoka kwa wananchi
ambao kwa umoja na ujumla wao wanaimiliki na kuipatia
Katiba hii uhalali;
(b) lengo kuu la Serikali litakuwa ni maendeleo na ustawi wa
wananchi;
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi; na
(d) wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali kwa
mujibu wa masharti ya Katiba hii.
Watu na
Serikali 7.-(1) Muundo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo
vyake, katika uendeshaji na utekelezaji wa shughuli zake utazingatia
azma ya kukuza umoja wa kitaifa na kudumisha heshima ya Taifa.
(2) Kwa madhumuni ya masharti ya Ibara ndogo (1), mamlaka
ya nchi na vyombo vyake vinawajibika kuelekeza sera na shughuli zake
zote kwa lengo la kuhakikisha kwamba:
(a) utu na haki nyingine zote za binadamu zinaheshimiwa na
kuthaminiwa;
(b) sheria za nchi zinasimamiwa na kutekelezwa;
(c) Serikali itahakikisha kuwa shughuli zinazofanywa
zinatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha kwamba
utajiri wa Taifa unaendelezwa, unahifadhiwa na
unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote kwa jumla na
pia kuzuia mtu kumnyonya mtu mwingine;
(d) ardhi ikiwa rasilimali kuu na msingi wa Taifa, inalindwa,
inatunzwa na kutumiwa na wananchi wa Tanzania kwa
manufaa, maslahi na ustawi wa kizazi cha sasa na vizazi
vijavyo;
(e) maendeleo ya uchumi wa Taifa yanapangwa na kukuzwa
kwa ulinganifu na kwa pamoja na kwa namna ambayo
inawanufaisha wananchi wote;
(f) kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anafanya kazi,
na kazi maana yake ni shughuli yoyote ya halali
inayompatia mtu kipato chake;
‐ 5 ‐
(g) utu, heshima na haki nyingine zote za binadamu
zinahifadhiwa na kudumishwa kwa kuzingatia mila na
desturi za kitanzania na kwa kufuata mikataba mbalimbali
iliyoridhiwa na Jamhuri ya Muungano;
(h) mamlaka za nchi zinatoa fursa na haki zilizo sawa kwa
wananchi wote, wanawake na waume, bila ya kujali rangi,
kabila, nasaba, dini au hali ya mtu;
(i) aina zote za dhulma, vitisho, ubaguzi, unyanyasaji,
rushwa, uonevu au upendeleozinaondolewa nchini;
(j) utajiri wa rasilimali na maliasili za Taifa unaelekezwa
katika kuleta maendeleo, kuondoa umaskini, ujinga na
maradhi; na
(k) nchi inatawaliwa kwa kufuata misingi ya demokrasia na
kujitegemea.
Mamlaka na
utii wa Katiba 8.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba za Washirika wa
Muungano kwa mambo yasiyo ya Muungano, Katiba hii itakuwa sheria
kuu katika Jamhuri ya Muungano.
(2) Mtu yeyote, chombo, taasisi, jumuiya na wakala wowote wa
mamlaka ya nchi na mamlaka binafsi zinao wajibu wa kuzingatia
masharti ya Katiba hii na kuyatii.
(3) Sheria yoyote, mila, desturi au uamuzi wowote wa chombo
cha dola, ofisa wa Serikali au mtu binafsi ni sharti ufuate na kuendana na
masharti yaliyomo kwenye Katiba hii na kwamba, sheria, mila, desturi
au uamuzi wowote ambao hautawiana au kwenda sambamba na masharti
ya Katiba hii utakuwa batili.
Hifadhi ya
Katiba 9.-(1) Mtu au kikundi cha watu hakitachukua au kushikilia
mamlaka ya nchi isipokuwa kwa mujibu wa Katiba hii.
(2) Kitendo chochote kinachokiuka masharti ya Ibara ndogo ya
(1) ni batili na ni kitendo cha uhaini kama itakavyoelezwa katika sheria
za nchi.
(3) Kwa madhumuni ya kuhifadhi masharti ya Ibara ndogo ya (1)
na (2), Serikali itaweka utaratibu wa kuisambaza Katiba hii kwa
wananchi na kuiweka katika mitaala ya elimu ili kuwezesha wananchi
kuifahamu, kuilinda na kuitii.
SURA YA PILI
MALENGO MUHIMU, MISINGI YA MWELEKEO WA
SHUGHULI ZA SERIKALI NA SERA ZA KITAIFA
Utekelezaji wa
malengo ya
Taifa
10.-(1) Malengo ya Taifa yaliyoainishwa ndani ya Katiba hii
yatakuwa ni mwongozo kwa Serikali, Bunge, Mahakama, vyama vya
siasa, taasisi, asasi na mamlaka nyingine na kwa kila mwananchi
katika matumizi au kutafsiri masharti ya Katiba hii au sheria nyingine
yoyote na katika utekelezaji wa uamuzi wa kisera kwa madhumuni ya
kujenga jamii huru, makini na iliyo bora.
(2) Serikali itatoa taarifa Bungeni si chini ya mara moja katika
‐ 6 ‐
kila mwaka, kuhusu hatua zilizochukuliwa na mamlaka ya nchi ili
kuhakikisha utekelezaji wa malengo ya Taifa yaliyoainishwa katika
Katiba hii.
Malengo
Makuu 11.-(1) Lengo Kuu la Katiba hii ni kulinda, kuimarisha na
kudumisha udugu, amani, umoja na utengamanowa wananchi wa
Jamhuri ya Muungano kwa kuzingatia ustawi wa wananchi na kujenga
Taifa huru lenye demokrasia, utawala bora na kujitegemea.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), lengo hilo
kuu litaendelezwa na kuimarishwa katika nyanja zote kuu,
ikijumuisha nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na
kimazingira.
(3) Katika kutekeleza malengo ya Taifa ya:
(a) kisiasa, Serikali itachukua hatua zinazofaa ili –
(i) kuhakikisha kuwa inazuia, inapinga na kuondoa
dhulma, vitisho, ubaguzi, unyanyasaji, rushwa,
uonevu na upendeleo miongoni mwa wananchi
kwa misingi ya asili ya mtu, sehemu anayotoka,
nasaba,kabila, jinsi, dini au imani yake;
(ii) kuhakikisha uwepo wa amani na kujenga
utamaduni wa kuenzi, kuheshimu na kudumisha
amani, umoja na utengamano, ushirikiano na
uvumilivu wa kisiasa kwa madhumuni ya kukuza
maendeleo ya kijamii na kiuchumi;
(iii) kuhakikisha uwepo wa ulinzi, usalama na ustawi
wa watu na mali zao, na kuepuka kufanya jambo
lolote litakalohatarisha au kwenda kinyume na
lengo hilo;
(b) kijamii, Serikali inachukua hatua zinazofaa ili:
(i) kuhakikisha kwamba heshima ya binadamu
inahifadhiwa na kudumishwa kwa kufuata mila,
desturi na Kanuni za Tangazo la Dunia kuhusu
Haki za Binadamu na mikataba mingine ya
kimataifa iliyoridhiwa na Tanzania;
(ii) kuhakikisha kwamba Serikali na vyombo vyake
vyote vya umma vinatoa nafasi na fursa zilizo
sawa kwa raia wote, bila ya kujali rangi, kabila,
dini, nasaba, hali ya mtu au mahali alipo;
(iii) kujenga utamaduni wa kuwepo ushirikiano,
maelewano na maridhiano, uvumilivu na
kuheshimu mila, desturi na imani ya dini ya kila
mtu;
(iv) kuhakikisha kuwa msaada na hifadhi ya jamii
inatolewa kwa watu wasiojiweza, wazee,
‐ 7 ‐
wagonjwa, watoto na watu wenye ulemavu;
(c) kiuchumi, Serikali inachukua hatua zinazofaa ili:
(i) kuwaletea wananchi maisha bora kwa kuondoa
umaskini;
(ii) kuhakikisha kwamba shughuli za Serikali
zinatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha
kuwa utajiri wa Taifa unaendelezwa,
unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya
wananchi wote kwa jumla na pia kuzuia mtu
kumnyonya mtu mwingine;
(iii) kuweka mazingira bora kwa ajili ya kuanzisha na
kuendeleza vyombo vya uwakilishi wa wakulima,
wafugaji na wavuvi;
(iv) kuweka mazingira bora ya kufanya biashara na
kukuza fursa za uwekezaji;
(v) kuweka mazingira bora kwa ajili ya kukuza
kilimo, ufugaji na uvuvi kwa kuhakikisha kuwa
wakulima, wafugaji na wavuvi wanakuwa na
ardhi na nyenzo kwa ajili ya kuendeleza shughuli
zao;
(vi) kuweka mazingira bora ya uzalishaji wa mazao
kwa wakulima, wafugaji na wavuvi, utafutaji na
uendelezaji wa masoko ya mazao yao;
(vii) kuweka utaratibu mzuri wa upangaji na
usimamiaji wa mizania ya bei za mazao na
pembejeo;
(viii) kuimarisha na kuendeleza uwekezaji wa ndani,
upatikanaji wa pembejeo za kilimo, maeneo ya
ufugaji na vifaa vya uvuvi;
(ix) kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa fursa na
nafasi za wazi kwa watu wote na kuanzisha
shughuli za kiuchumi na kukuza mazingira yaliyo
bora kwa ajili ya kuhamasisha sekta binafsi
katika uchumi;
(x) kuhakikisha kuwa kila mtu mwenye uwezo wa
kufanya kazi anapata fursa ya kufanya kazi, kwa
maana ya kufanya shughuli yoyote halali
inayompatia kipato;
(xi) kuweka utaratibu unaofaa kwa ajili ya
kufanikisha utekelezaji wa haki ya mtu kujipatia
elimu na kuwa huru kupata fursa sawa ya
kutafuta elimu katika fani anayoipenda hadi
kufikia upeo wowote kulingana na stahili na
uwezo wake;
(d) kiutamaduni, Serikali itachukua hatua zinazofaa ili:
(i) kulinda na kuhifadhi urithi wa asili, malikale na
sehemu zenye umuhimu wa kihistoria au kidini ili
kuepuka uharibifu, udhalilishaji na wizi au
utoroshwaji nje ya nchi;
‐ 8 ‐
(ii) kulinda, kuhifadhi na kuendeleza tamaduni za
watu wa jamii mbalimbali ambazo zinaendeleza
na kukuza utu na hadhi yao kwa namna ambayo
haikinzani na Misingi ya Kitaifa, na Malengo
Muhimu na Sera za Taifa;
(iii) kutambua, kulinda na kuendeleza lugha ya
Kiswahili; na
(e) kimazingira, Serikali itachukua hatua zinazofaa ili
kuhakikisha kuwa ni haki na jukumu la kila kizazi kulinda
na kudumisha mazingira kwa faida ya kizazi cha sasa na
vizazi vijavyo.
Sera kuhusu
Mambo
ya Nje
12. Sera ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Muungano inalenga
nainazingatia maslahi ya Taifa na mamlaka kamili ya nchi na kwamba
sera hiyo inatekelezwa kwa uwazi ili:
(a) kukuza ushirikiano wa kikanda na ushirikiano wa
kimataifa;
(b) kukuza ushirikiano wa kiuchumi wenye tija kwa Taifa;
(c) kuleta maendeleo ya kiuchumi kwa mataifa ya Afrika
kwa kushiriki katika hatua mbalimbali za mtangamano
wa kiuchumi wa kikanda;
(d) kuheshimu sheria za kimataifa;
(e) kuzingatia mikataba ya kimataifa, mikataba ya kikanda
yenye maslahi kwa Jamhuri ya Muungano na kutatua
migogoro ya kimataifa kwa njia ya majadiliano,
usuluhishi, maridhiano na mahakama;
(f) kukuza uzingatiaji wa haki za binadamu na uhuru wa
watu;
(g) kupambana na makosa ya kimataifa ya kijinai; na
(h) kuheshimu uhuru wa mataifa mengine.
SURA YA TATU
MAADILI NA MIIKO YA UONGOZI NA UTUMISHI WA UMMA
SEHEMU YA KWANZA
MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA
Dhamana ya
Uongozi wa
Umma
13.-(1) Madaraka anayopewa kiongozi wa umma:
(a) ni dhamana na atatumia madaraka hayo na kutekeleza
wajibu wake kwa:
(i) kuzingatia masharti ya Katiba hii;
(ii) kuheshimu wananchi;
(iii) namna inayokuza hadhi ya taifa na kulinda
heshima ya ofisi anayoitumikia; na
(iv) kukuza imani na heshima ya ofisi kwa
wananchi;
(b) yanatoa wajibu kwa kiongozi kuwatumikia wananchi.
(2) Dhamana ya uongozi na heshima kwa kiongozi wa umma
itazingatia mambo yafuatayo:
‐ 9 ‐
(a) uteuzi kwa misingi ya mwenendo wa mtu, uwezo, sifa
au uchaguzi uliyo huru na haki;
(b) uwezo pasipo upendeleo katika kufanya uamuzi na
kuhakikisha kwamba uamuzi haufuati udugu, ukabila,
udini, upendeleo, rushwa au vigezo vingine visivyo
sahihi;
(c) utoaji wa huduma pasipo upendeleo na kwa kufuata
maslahi ya umma kwa kuonyesha-
(i) uaminifu katika utekelezaji wa kazi za umma;
(ii) wajibu wa kutangaza maslahi binafsi ili kuepuka
mgongano wa maslahi;
(d) uwajibikaji kwa umma katika kufanya uamuzi na
vitendo; na
(e) nidhamu na kujituma katika kutoa huduma kwa umma.
Kanuni za
Uongozi wa
Umma
14.-(1) Kiongozi wa umma, akiwa ama katika kazi za ofisi au
kazi binafsi au wakati amejumuika na watu wengine, atahakikisha
kwamba mwenendo wake:
(a) hauruhusu kutokea mgongano wa maslahi kati ya
maslahi binafsi na maslahi ya utumishi wa umma;
(b) hauhatarishi maslahi ya umma kwa ajili ya maslahi
binafsi; au
(c) haushushi hadhi ya ofisi anayofanyia kazi.
(2) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (1), mamlaka ya nchi
itaweka utaratibu wa sheria utakaowezesha Tume ya Maadili ya
Uongozi na Uwajibikaji kusimamia utekelezaji wa masharti
yanayohusu kanuni za uongozi wa umma.
(3) Wadhifa “Kiongozi wa Umma” kama ulivyotumika katika
Sehemu hii utajumuisha viongozi wa kuchaguliwa na kuteuliwa kama
watakavyoainishwa kwenye sheria itakayotungwa na Bunge.
Zawadi katika
Utumishi wa
Umma
15.-(1) Zawadi au kitu chochote kitakachotolewa kwa
mtumishi wa umma katika shughuli za kiserikali ni zawadi kwa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na itawasilishwa kwa Katibu
Mkuu Kiongozi kupitia kwa Katibu Mkuu wa Wizara au taasisi ya
Serikali inayohusika, akiainisha:
(a) aina ya zawadi;
(b) thamani ya zawadi;
(c) sababu ya kupewa zawadi; na
(d) mtu au mamlaka iliyotoa zawadi hiyo.
(2) Mtumishi wa Umma -
(a) hatafungua au kuendesha akaunti ya benki nje ya
Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kwa namna
ambayo sheria za nchi zinaruhusu; na
(b) hataomba au kupokea mkopo au faida yoyote kwa
namna au mazingira ambayo yanashusha hadhi au
heshima ya mtumishi wa umma.
‐ 10 ‐
(3) Bunge litatunga sheria itakayosimamia, pamoja na mambo
mengine, thamani, kiwango, aina na uhifadhi wa zawadi inayohusika
na masharti ya Sehemu hii na masharti mengine yanayohusu
utekelezaji wa masharti ya Ibara hii.
Wajibu wa
kutangaza mali
na madeni
16.-(1) Kiongozi wa Umma atalazimika kutangaza, ndani ya
siku thelathini baada ya kupata uongozi na baada ya kuacha uongozi,
mali na thamani zake na madeni yake katika Tume ya Maadili na
Uwajibikaji.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), Kiongozi
wa Umma atalazimika kutangaza mali zake na madeni:
(a) yake binafsi;
(b) ya mwenza wake wa ndoa; na
(c) watoto wake walio chini ya umri wa miaka kumi na nane,
mara moja kila mwaka, au kadri itakavyoamuliwa na sheria.
Mgongano wa
kimaslahi
17.-(1) Kiongozi wa Umma hatashiriki katika jambo au
shughuli yoyote ambayo ana maslahi nayo yeye binafsi, mwenza
wake, mtoto wake, jamaa yake, rafiki au mtu yeyote wake wa karibu.
(2) Kiongozi wa umma hatozungumzia kitu chochote katika
Baraza la Mawaziri, Bunge, kamati au chombo kingine chochote
rasmi ambacho ana maslahi nacho ya moja kwa moja au vinginevyo,
isipokuwa tu kama atatoa taarifa ya mgongano huo wa maslahi katika
vyombo hivyo.
(3) Itakuwa ni marufuku kwa Kiongozi yeyote wa Umma,
kushiriki kuongeza au kwa namna yoyote ile, kuboresha maslahi
yanayohusu wadhifa alionao, na endapo atashiriki, basi masharti hayo
mapya yataanza kutumika kwa Kiongozi atakayekuja baada ya yeye
kuondoka au kumaliza muda wa kukaa madarakani.
(4) Bunge litatunga sheria itakayosimamia, pamoja na mambo
mengine, masuala ya:
(a) ngazi au orodha ya Viongozi wa Umma, wanaopaswa
kutangaza mali zao;
(b) utaratibu wa utwaaji wa mali za Viongozi wa Umma
zilizopatikana kwa njia za ukiukaji wa sheria;
(c) utaratibu wa kumwajibisha Kiongozi wa Umma aliyeenda
kinyume na maadili na Miiko ya Uongozi;
(d) uanzishaji wa mitaala inayohusu maadili na uraia,
mashuleni na vyuoni; na
(e) uanzishaji wa mitaala inayohusu Katiba mashuleni na
vyuoni.
(5) Kiongozi wa Umma hataruhusiwa kushika nyadhifa mbili
au zaidi au kutumikia Mihimili ya Dola zaidi ya mmoja kwa wakati
mmoja.
Matumizi ya
mali ya umma 18. Haitaruhusiwa kwa Kiongozi yeyote wa Umma kutumia au
kuruhusu kutumika kwa mali yoyote ya umma, zikiwemo
zilizokodishwa kwa Serikali, kwa madhumuni ya kumpatia yeye
binafsi au mtu mwingine yeyote manufaa ya kiuchumi.
‐ 11 ‐
Matumizi ya
masharti ya
maadili kwa
Watumishi wa
Umma
19. Masharti yaliyoainishwa katika Ibara za 13 mpaka 18
yatatumika pia kwa watumishi wa umma baada ya kufanyiwa
marekebisho stahiki.
SEHEMU YA PILI
MIIKO YA UONGOZI WA UMMA
Utii wa Miiko
ya Uongozi wa
Umma
20.-(1) Bila ya kuathiri masharti yoyote ya Katiba hii, kiongozi
yeyote wa Umma atapaswa kuheshimu na kutii maadili ya viongozi
wa umma, ikiwemo Miiko ya Uongozi.
(2) Miiko ya Uongozi inayorejewa katika Ibara ndogo (1),
itakuwa kama ifuatavyo:
(a) Kiongozi wa umma hatopaswa:
(i) kuvunja au kukiuka masharti ya Katiba ya
Jamhuri ya Muungano;
(ii) kutoa au kupokea rushwa;
(iii) kujilimbikizia mali kinyume cha sheria;
(iv) kusema uongo au kutoa taarifa zisizo za ukweli;
(v) kutoa siri za Serikali kinyume na sheria;
(vi) kutumia wadhifa, nafasi au cheo chake kwa
manufaa yake binafsi, familia yake, ndugu, jamaa
au marafiki zake au mtu yeyote aliye na uhusiano
naye wa karibu;
(vii) kufanya vitendo vya uzembe, uvivu, ubaguzi,
kiburi, dharau au unyanyasaji wa kijinsia.
(b) Kiongozi wa umma atapaswa:
(i) kuheshimu na kuendeleza dhana ya uwajibikaji
wa pamoja, kwa viongozi wanaohusika; na
(ii) kuheshimu na kuendeleza maadili ya viongozi wa
umma, ikijumuisha:
(aa) kuwa na tabia na mienendo inayokubalika
katika jamii;
(bb) kuheshimu, kutunza na kulinda mali za
umma; na
(cc) kutambua, kuheshimu na kuzingatia
Kanuni za Maadili na Mienendo ya
Watumishi wa Umma, Kanuni za Kudumu
za Watumishi wa Umma, nyaraka za
umma na miongozo mbalimbali ya Serikali
kuhusu viongozi na watumishi wa umma.
(iii) kutenganisha shughuli za biashara na masuala
yanayohusiana na uongozi.
(3) Kiongozi yeyote wa umma ambaye anatuhumiwa na
kuthibitika kwa makosa ya:
(a) kimaadili;
(b) udhalilishaji wa mtu au wa kijinsia; na
(c) wizi au ubadhirifu wa mali za umma,
‐ 12 ‐
atasimamishwa kazi mpaka suala lake litakapoamuliwa kwa mujibu
wa sheria au taratibu nyingine zinazowahusu viongozi wa umma.
Marufuku
baadhi ya
vitendo
21.-(1) Mtumishi wa umma aliye katika ajira ya kudumu
hataruhusiwa kuingia katika ajira nyingine yoyote yenye malipo ya
mshahara.
(2) Mtumishi wa umma haruhusiwi kuchaguliwa au kuteuliwa
kushika madaraka katika chama cha siasa.
(3) Mtumishi wa umma aliyestaafu na anayepokea malipo ya
pensheni kutokana na fedha za umma haruhusiwi kuwa mwenyekiti,
mkurugenzi au mtumishi zaidi ya vipindi viwili katika:
(a) shirika au kampuni inayomilikiwa au kuendeshwa kwa
fedha za umma; au
(b) chombo chochote cha umma.
SURA YA NNE
HAKI ZA BINADAMU, WAJIBU WA RAIA NA MAMLAKA ZA NCHI
SEHEMU YA KWANZA
HAKI ZA BINADAMU
Uhuru, utu na
usawa wa
binadamu
22.-(1) Binadamu wote huzaliwa huru na wote ni sawa.
(2) Kila mtu anayo haki ya kuheshimiwa, kutambuliwa na
kuthaminiwa utu wake.
Haki ya
kuishi
23. Kila mtu anayo haki ya kuishi na kupata hifadhi ya maisha
yake kutoka katika Serikali na jamii kwa mujibu wa sheria.
Marufuku
kuhusu
ubaguzi
24.-(1) Watu wote ni sawa mbele ya sheria na wanayo haki ya
kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria.
(2) Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu, mamlaka ya
nchi au mamlaka yoyote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria
yoyote au katika kutekeleza kazi au shughuli yoyote ya mamlaka ya nchi.
(3) Ni marufuku kwa sheria yoyote iliyotungwa na mamlaka
yoyote katika Jamhuri ya Muungano kuweka sharti lolote ambalo ni la
ubaguzi ama wa dhahiri au kwa taathira yake.
(4) Haki ya raia, wajibu na maslahi ya kila mtu na jumuiya ya
watu yatalindwa na kuamuliwa na mahakama na vyombo vinginevyo vya
mamlaka ya nchi vilivyowekwa kwa mujibu wa sheria.
(5) Kwa madhumuni ya masharti ya Ibara hii na kwa kuzingatia
masharti ya Ibara ndogo ya (4), neno “kubagua” maana yake ni kutimiza
utashi, haki au mahitaji mengineyo kwa watu mbalimbali kwa kuzingatia
utaifa wao, kabila, mahala walipotokea, maoni yao ya kisiasa, rangi, dini,
jinsi au hali yao ya maisha kwa namna ambayo watu wa aina fulani
wanafanywa au kuhesabiwa kuwa dhaifu au duni na kuwekewa vikwazo
au masharti ya vipingamizi ambapo watu wa aina nyingine wanatendewa
tofauti au wanapewa fursa au faida iliyoko nje ya masharti au sifa za
lazima.
‐ 13 ‐
(6) Neno “kubagua” lilivyotumiwa katika Ibara ndogo ya (2),
halitafafanuliwa kwa namna ambayo itaizuia mamlaka ya nchi kuchukua
hatua za makusudi zenye lengo la kurekebisha matatizo mahsusi katika
jamii.
(7) Kwa madhumuni ya kuhakikisha usawa mbele ya sheria,
mamlaka ya nchi itaweka utaratibu unaofaa na unaozingatia misingi
kwamba -
(a) wakati haki na wajibu kwa mtu yeyote vinapohitajika
kufanyiwa uamuzi na mahakama au mamlaka nyingine
inayohusika, basi mtu huyo atakuwa na haki ya kupewa
fursa ya kusikilizwa kwa ukamilifu, na pia atakuwa na haki
ya kukata rufani au kupata nafuu nyingine ya kisheria
kutokana na uamuzi wa mahakama au mamlaka nyingine
inayohusika;
(b) ni marufuku kwa mtu aliyeshtakiwa kwa kosa la jinai
kutendewa kama mtu aliyehukumiwa kwa kutenda kosa
hilo hadi itakapothibitika mahakamani kuwa anayo hatia
ya kutenda kosa hilo;
(c) ni marufuku kwa mtu kuadhibiwa kwa sababu ya kitendo
chochote ambacho wakati alipotenda kitendo hicho
hakikuwa ni kosa chini ya sheria;
(d) ni marufuku kwa mtu kupewa adhabu ambayo ni kubwa
kuliko adhabu iliyokuwapo wakati kosa linalohusika
lilipotendeka;
(e) kwa ajili ya kuhifadhi haki ya usawa wa binadamu,
heshima ya mtu na faragha itahifadhiwa katika shughuli
zote zinazohusu upelelezi wa tuhuma na uendeshaji wa
masharti ya jinai na katika shughuli nyingine ambazo mtu
anakuwa katika kizuizi cha mamlaka ya nchi au katika
kuhakikisha utekelezaji wa adhabu; na
(f) ni marufuku kwa mtu kuteswa, kuadhibiwa kinyama au
kupewa adhabu zinazotweza au kudhalilisha.
Haki ya
kutokuwa
mtumwa
25.-(1) Kila mtu ana haki ya kutotendewa au kutotumikishwa kama
mtumwa, kutofanyishwa kazi za kulazimishwa au kutweza, na kwa msingi
huo, ni marufuku kwa mtu:
(a) kufanywa au kutendewa kama mtumwa;
(b) kulazimishwa kufanya kazi bila hiyari yake; au
(c) kusafirishwa kwa nia ya kufanyiwa biashara au faida ya mtu
mwingine.
(2) Biashara ya kusafirisha binadamu ni marufuku katika Jamhuri
ya Muungano.
Uhuru wa mtu
binafsi 26.-(1) Kila mtu anayo haki ya kuwa huru na kuishi akiwa mtu
huru.
(2) Kwa madhumuni ya kuhifadhi haki ya mtu kuwa huru na
kuishi kwa uhuru, itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote kukamatwa,
kufungwa, kufungiwa, kuwekwa kizuizini, kuhamishwa kwa nguvu au
kunyang’anywa uhuru wake vinginevyo, isipokuwa tu katika‐
14 ‐
(a) hali na kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria; au
(b) kutekeleza hukumu, amri au adhabu iliyotolewa na
mahakama kutokana na shauri au kutiwa hatiani kwa kosa la
jinai.
Haki ya
faragha na
usalama wa
mtu
27.-(1) Kila mtu anastahili kuheshimiwa na kupata hifadhi kwa
nafsi yake, maisha yake binafsi na familia yake na nyumbani kwake,
kutoteswa au kudhalilishwa, na pia heshima na hifadhi ya maskani yake na
mawasiliano yake ya binafsi.
(2) Kwa madhumuni ya kuhifadhi haki ya mtu, mamlaka ya nchi
itaweka utaratibu wa sheria kuhusu hali, namna na kiasi ambacho haki ya
mtu ya faragha na ya usalama wa nafsi yake, mali na maskani yake,
yanaweza kuingiliwa bila ya kuathiri masharti ya Ibara hii.
Uhuru wa mtu
kwenda
anakotaka
28.-(1) Kila raia anayo haki ya kwenda kokote katika Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na kuishi katika sehemu yoyote, kutoka nje ya
nchi na kuingia, na pia haki ya kutoshurutishwa, kuhama au kufukuzwa
kutoka katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
(2) Kitendo chochote halali au sheria yoyote yenye madhumuni
ya -
(a) kupunguza uhuru wa mtu kwenda anakotaka na kumweka
chini ya ulinzi au kifungoni; au
(b) kuweka mipaka kwa matumizi ya uhuru wa mtu kwenda
anakotaka ili-
(i) kutekeleza hukumu au amri ya mahakama;
(ii) kumlazimisha kutimiza kwanza wajibu wowote
anaotakiwa na sheria nyingine kuutimiza; au
(iii) kulinda manufaa ya umma kwa jumla au
kuhifadhi maslahi fulani mahsusi au maslahi ya
sehemu fulani ya umma,
hakitahesabiwa au sheria hiyo haitahesabiwa kuwa ni kinyume cha
masharti ya Ibara hii.
Uhuru wa
maoni 29.-(1) Kila mtu:
(a) anao uhuru wa-
(i) kuwa na maoni na kueleza fikra zake;
(ii) kufanya mawasiliano na vile vile anayo haki ya
kutoingiliwa katika mawasiliano yake;
(iii) ubunifu na sanaa;
(iv) kitaaluma na tafiti za kisayansi; na
(b) anayo haki ya kupewa taarifa wakati wowote kuhusu:
(i) matukio mbalimbali muhimu kwa maisha na
shughuli za wananchi; na
(ii) utekelezaji wa mamlaka ya nchi kuhusu sera za
kitaifa na shughuli ya maendeleo ya jamii; na
(iii) masuala mengine muhimu kwa jamii.
(2) Utekelezaji wa haki zilizoainishwa katika Ibara ndogo ya (1),
utajumuisha wajibu muhimu kwa mwananchi na wajibu huo unaweza
kupunguza haki hizo kutokana na:
‐ 15 ‐
(a) vita au machafuko ya kisiasa; au
(b) propaganda kuhusu vita, ushawishi wa chuki kwa misingi
ya rangi, ukabila, ubaguzi wa kijinsia, dini au masuala
yoyote yanayoweza kuleta madhara kwa Taifa.
Uhuru wa
habari na
vyombo vya
habari
30.-(1) Kila mtu anao uhuru wa-
(a) kutafuta, kupata na kutumia habari na taarifa na
kusambaza taarifa hizo; na
(b) kuanzisha vyombo vya habari na njia nyingine za
upashanaji wa habari bila kujali mipaka ya nchi.
(2) Vyombo vya habari vitakuwa huru na vile vile vitakuwa na:
(a) haki ya kupata, kutumia na kusambaza habari na taarifa
wanazopata;
(b) wajibu wa:
(i) kusambaza habari na taarifa kwa wananchi; na
(ii) kuheshimu na kulinda utu, heshima, uhuru na staha
ya wananchi dhidi ya habari na taarifa
wanazozitumia, wanazozitayarisha na kuzisambaza.
(3) Serikali na taasisi zake, asasi za kiraia na watu binafsi
watakuwa na wajibu wa kutoa habari kwa umma juu ya shughuli na
utekelezaji wa shughuli zao.
(4) Masharti ya Ibara hii yatalazimika kuzingatia masharti ya
sheria ya nchi itakayotungwa kwa ajili hiyo na kwa madhumuni ya
kulinda usalama wa Taifa, amani, maadili ya umma, haki, staha na uhuru
wa watu wengine.
Uhuru wa
imani ya dini 31.-(1) Kila mtu anao uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi
katika mambo ya imani ya dini na anao uhuru pia wa kubadilisha dini,
imani yake au kutokuwa na imani na dini.
(2) Kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa
ni huru na jambo la hiari kwa mtu binafsi ili mradi asivunje sheria za nchi.
(3) Shughuli ya uendeshaji wa jumuiya za dini itakuwa nje ya
shughuli za mamlaka ya Serikali.
(4) Hifadhi ya haki zilizotajwa katika Ibara hii itakuwa chini ya
taratibu zilizowekwa na sheria ambazo ni muhimu katika jamii ya
kidemokrasia kwa ajili ya usalama, amani, maadili na umoja wa jamii na
wa kitaifa na vitasimamiwa kwa utaratibu ulioainishwa kwenye sheria za
nchi.
(5) Ni marufuku kwa mtu, kikundi au taasisi ya dini kutumia uhuru
wa kutangaza dini kwa kukashifu imani na dini nyingine, kujenga chuki au
kuchochea vurugu na ghasia kwa madai ya kutetea imani au dini.
(6) Dini na imani ya dini haitatumika kwa namna yoyote
itakayowagawa wananchi, kuleta uhasama au kuharibu amani miongoni
mwa wananchi.
(7) Neno “dini” kama lilivyotumika katika Ibara hii litatafsiriwa
kwamba maana yake ni pamoja na madhehebu ya dini, na maneno
mengine yanayofanana au kuambatana na neno hilo nayo yatatafsiriwa
kwa maana hiyo.
‐ 16 ‐
Uhuru wa mtu
kujumuika na
kushirikiana
na
wengine
32.Kila mtu anastahili kuwa huru, bila ya kuathiri sheria za nchi,
kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani, kujumuika na
kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo hadharani, na hasa zaidi
kuanzisha au kujiunga na vyama au mashirika yaliyoanzishwa kwa
madhumuni ya kuhifadhi au kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi
mengineyo.
Uhuru wa
kushiriki
shughuli
za umma
33.-(1) Kila raia wa Jamhuri ya Muungano ana haki ya kushiriki
katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia
wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia
utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria.
(2) Kila raia ana haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika
kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomhusu yeye, maisha yake au
yanayolihusu Taifa.
Haki ya
kufanya kazi 34.-(1) Kila mtu ana haki ya kufanya kazi ya kuajiriwa au kujiajiri
mwenyewe.
(2) Kila mtu ana haki na fursa sawa kushika nafasi yoyote ya
kazi, uongozi au shughuli yoyote iliyo chini ya mamlaka ya nchi.
Haki za
wafanyakazi
na waajiri
35.-(1) Kila mfanyakazi ana haki zifuatazo:
(a) kufanya kazi bila ubaguzi wa aina yoyote;
(b) kupata ujira na malipo halali kulingana na kiasi na sifa za kazi
anayofanya;
(c) kuunda au kujiunga na chama cha wafanyakazi mahala pa
kazi; na
(d) kushiriki katika shughuli za chama cha wafanyakazi;
(2) Kila chama cha waajiri na wafanyakazikitakuwa na haki ya:
(a) kuamua kuhusu uongozi, programu na shughuli zake; na
(b) kuanzisha, kujiunga na kusimamia shirikisho lao.
(3) Kila chama cha wafanyakazikitakuwa na haki ya kufanya
majadiliano ya pamoja na mwajiri na kuingia mikataba ya hali bora ya kazi.
(4) Bunge litatunga sheria itakayoweka masharti kuhusu haki za
wafanyakazi na utaratibu utakaowezesha wafanyakazi kutumia haki zao.
Haki ya
kumiliki mali 36.-(1) Kila mtu anayo haki ya kumiliki mali na hifadhi ya mali
yake aliyonayo kwa mujibu wa sheria.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), itakuwa ni
marufuku kwa mtu yeyote kunyang’anywa mali yake kwa madhumuni ya
kuitaifisha au madhumuni mengine bila malipo yanayolingana na thamani
halisi ya mali hiyo na yatakayotolewa mapema.
(3) Kwa madhumuni ya masharti ya Ibara hii, haki ya umiliki na
hifadhi ya mali haitahusu mali iliyothibitishwa kwamba haikupatikana
kwa njia halali.
Haki ya uraia 37. Kila raia ana haki ya kutambuliwa uraia wake na kwa
madhumuni haya, mamlaka ya nchi itaweka utaratibu wa sheria
utakaowezesha wananchi kupata hati ya kuzaliwa, kitambulisho cha uraia
‐ 17 ‐
wake bila ya upendeleo na ubaguzi wa aina yoyote, na pale inapohitajika,
nyaraka za kumwezesha kusafiri.
Haki ya
mtuhumiwa
na mfungwa
38.-(1) Mtu aliyekamatwa au aliyewekwa kizuizini anayo haki ya:
(a) kuelezwa kwa lugha anayoifahamu -
(i) sababu ya kukamatwa;
(ii) haki ya kutokutoa maelezo yoyote; na
(iii) matokeo ya kutoa maelezo;
(b) kutoa maelezo;
(c) kuwasiliana na wakili na mtu mwingine ambaye msaada wake
ni muhimu kwa mtuhumiwa;
(d) kutolazimishwa kutoa maelezo ya kukiri kosa ambayo
yatatumika kama ushahidi dhidi yake; na
(e) kupelekwa mahakamani mapema iwezekanavyo.
(2) Mamlaka za nchi zitaweka utaratibu wa sheria utakaowezesha:
(a) mtuhumiwa kupata nakala ya mashtaka yanayomkabili na
kumbukumbu ya mwenendo wa mashtaka;
(b) mtuhumiwa au mfungwa kupata nakala ya mwenendo wa
mashtaka baada ya shauri kukamilika mahakamani;
(c) mtuhumiwa au mfungwa kufikishwa mahakamani ili
kuthibitisha uwepo wake.
Haki ya
watu waliyo
chini ya
ulinzi
39.-(1) Mtu aliye katika kizuizi au ulinzi ataendelea kuwa na haki
zote za msingi zilizoainishwa katika Katiba hii kwa kiwango anachostahiki
katika mazingira ya kuwekwa kizuizini au katika ulinzi.
(2) Mtu aliye katika kizuizi au ulinzi ana haki ya kuiomba
mahakama ili mamlaka ya nchi inayomuhifadhi kueleza sababu za yeye
kuwekwa au kuendelea kuwa katika kizuizi au ulinzi.
(3) Raia wa Jamhuri ya Muungano hatapelekwa katikanchi ya nje
yoyote kujibu mashtaka au kufanyiwa mahojiano ya aina yoyote kinyume
cha ridhaa yake.
Uhuru na haki
ya mazingira
safi na salama
40.-(1) Kila mtu anayeishi katika Jamhuri ya Muungano ana haki
ya kuishi katika mazingira safi, salama na ya kiafya.
(2) Haki ya kuishi katika mazingira safi, salama na ya kiafya
inahusisha haki kwa kila raia kutumia maeneo ya umma au sehemu
mbalimbali za mazingira yaliyotengwa kwa madhumuni ya burudani,
elimu, afya, ibada, utamaduni na shughuli za kiuchumi.
(3) Mtu yeyote anayeishi Tanzania anao wajibu wa kutunza na
kuendeleza mazingira na kutoa taarifa kwa mamlaka za nchi kuhusu
shughuli au jambo lolote ambalo ni hatarishi au linauwezekano mkubwa
wa kuharibu au kuathiri mazingira.
Haki ya elimu
na kujifunza
41.-(1) Kila mtu ana haki ya:
(a) kupata fursa ya kupata elimu bila ya vikwazo;
‐ 18 ‐
(b) kupata elimu bora ya msingibila ya malipo na inayomtayarisha
kikamilifu mwanafunzi ama kuendelea na elimu ya ngazi
inayofuatia au kuweka msingi wa kuanza kujitegemea;
(c) kwa elimu inayotolewa nje ya utaratibu wa umma, kupata
elimu kwa gharama nafuu; na
(d) kupata fursa sawa ya kupata elimu ya juu ili mradi ana sifa
stahiki kupata elimu hiyo,
bila ya ubaguzi wa aina yoyote.
(2) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (1), kila mtu ana haki ya
kuchagua taaluma na ajira anayoitaka kwa mujibu wa elimu yake na ujuzi
aliyonao.
Haki ya
mtoto 42.-(1) Kila mtoto ana haki ya-
(a) kupewa jina na uraia;
(b) kutoa mawazo, kusikilizwa na kulindwa dhidi ya uonevu,
ukatili na udhalilishaji;
(c) kucheza na kupata elimu;
(d) kuhifadhiwa katika mazingira mazuri, kwa walio katika
ukinzani na sheria;
(e) kupata lishe bora, makazi na huduma ya afya; na
(f) kushiriki katika shughuli zinazolingana na umri alionao; na
(g) kupata malezi na ulinzi wa wazazi, walezi au mamlaka ya
nchi,
bila ya ubaguzi wa rangi, utaifa, lugha, mtazamo wa kisiasa, jamii
anayotokea, mali, uzazi, kabila, dini, jinsi au aina nyingine za hadhi.
(2) Mamlaka ya nchi itaweka utaratibu wa sheria utakaowezesha
utekelezaji na usimamizi wa haki za mtoto kwa kufuata msingi wa kutoa
kipaumbele kwa maslahi na manufaa ya mtoto.
Haki na
wajibu wa
vijana
43. Kila kijana ana haki na wajibu wa kushiriki kikamilifu katika
shughuli za maendeleo ya Jamhuri ya Muungano pamoja na jamii kwa
ujumla, na kwa mantiki hiyo, Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Serikali
za Washirika wa Muungano na jamii zitahakikisha kuwa vijana
wanawekewa mazingira mazuri ya kuwa raia wema na kupatiwa fursa za
kushiriki kikamilifu katika nyanja za kisiasa, kiuchumi,kijamii na
kiutamaduni.
Haki za
watu wenye
ulemavu
44.-(1) Mtu mwenye ulemavu anastahiki:
(a) kuheshimiwa, kutambuliwa na kutendewa kwa namna
ambayo haishushi utu wake;
(b) kupata elimu kwa kutumia vifaa maalum na kushiriki
katika shughuli za kijamii;
(c) kuwekewa miundombinu na mazingira yatakayowezesha
kwenda anapotaka, kutumia vyombo vya usafiri na kupata
habari;
(d) kutumia lugha za alama, maandishi ya nukta nundu au njia
nyingine zinazofaa;
‐ 19 ‐
(e) haki ya kusoma na kuchanganyika na watu wengine; na
(f) haki ya kupata ajira na kugombea nafasi za uongozi katika
nyadhifa mbalimbali kwa usawa.
(2) Mamlaka ya nchi itaweka utaratibu wa sheria utakaowezesha
watu wenye ulemavu kushiriki katika nafasi za uwakilishi.
Haki za
makundi
madogo
katika jamii
45.-(1) Mamlaka ya nchi itaweka utaratibu wa sheria
utakaowezesha makundi madogo katika jamii:
(a) kushiriki katika uongozi wa mamlaka za nchi;
(b) yanapewa fursa maalum za elimu na fursa za kujiendeleza
kiuchumi na fursa za ajira;na
(c) kutengewa maeneo ya ardhi ambayo kwa desturi makundi
hayo kuitumuia kama eneo la kuishi na kupata riziki ya
chakula.
(2) Serikali na mamlaka za nchi zitachukua hatua za makusudi za
kukuza na kuendeleza shughuli za kiuchumi na kuweka miundombinu ya
makazi, elimu na afya kwa ajili ya kizazi cha sasa na vijavyo vya jamii ya
watu walio katika makundi madogo.
Haki za
wanawake 46.-(1) Kila mwanamke ana haki ya:
(a) kuheshimiwa utu wake;
(b) kuwa salama dhidi ya unyonyaji na ukatili;
(c) kushiriki bila ya ubaguzi katika chaguzi na ngazi zote za
maamuzi;
(d) kupata ujira sawa na mwanaume katika kazi;
(e) kulindwa dhidi ya ubaguzi, uonevu na mila zenye madhara;
(f) kulindwa kwa ajira yake wakati wa ujauzito na pale
anapojifungua; na
(g) kupata huduma ya juu ya afya inayopatikana.
(2) Mamlaka husika za nchi zitaweka utaratibu wa kisheria
utakaosimamia masuala yanayohusu utekelezaji wa masharti ya Ibara hii
ikiwa ni pamoja na kukuza utu, usalama na fursa za wanawake wakiwemo
wajane.
Haki za
wazee 47. Mamlaka ya nchi itaweka utaratibu utakaowezesha wazee
kupata fursa ya:
(a) kushiriki katika shughuli za kijamii;
(b) kuendeleza maisha yao;
(c) kutambuliwa utu wao na kuheshimiwa pasipo
kudharauliwa;
(d) kulelewa na kupata misaada kutoka katika familia zao,
jamii na mamlaka ya nchi; na
(e) kupewa fursa ya kuendelea kutumia utaalamu na ujuzi wao
kwa faida na manufaa ya jamii.
‐ 20 ‐
SEHEMU YA PILI
WAJIBU WA RAIA NA MAMLAKA ZA NCHI
(a) Wajibu wa Raia kwa Taifa
Wajibu wa
kushiriki kazi 48.-(1) Kila mtu ana wajibu wa -
(a) kushiriki kwa kujituma na kwa uaminifu katika kazi halali
ya uzalishaji mali; na
(b) kuwa na nidhamu ya kazi na kujitahidi kufikia malengo ya
uzalishaji mali yake binafsi na yale malengo ya pamoja
yanayotakiwa au yaliyowekwa na sheria.
(2) Bila ya kujali masharti ya Ibara ndogo ya (1), kazi yoyote ya
shuruti ni marufuku katika Jamhuri ya Muungano.
(3) Kwa madhumuni ya Katiba hii, kazi yoyote haitahesabiwa
kuwa ni kazi ya shuruti au kazi ya kikatili au ya kutweza endapo kazi
hiyo, kwa mujibu wa sheria ni -
(a) kazi ambayo haina budi ifanywe kutokana na
hukumu au amri ya mahakama;
(b) kazi ambayo haina budi kufanywa na askari wa jeshi
lolote katika kutekeleza majukumu yao;
(c) kazi ambayo haina budi kufanywa kutokana na kuwapo hali
ya hatari au baa lolote linalotishia uhai na ustawi wa
jamii; na
(d) kazi au huduma yoyote ambayo ni sehemu ya -
(i) majukumu ya kawaida ya kuhakikisha ustawi wa
jamii;
(ii) ujenzi wa Taifa wa lazima kwa mujibu wa sheria;
(iii) jitihada za Taifa za kutumia uwezo wa kila mtu
kufanya kazi kwa ajili ya kuimarisha ustawi wa
jamii na uchumi wa Taifa na kuhakikisha
maendeleo na tija ya kitaifa.
Ulinzi wa
mali ya
umma
49.-(1) Kila raia anao wajibu wa kulinda maliasili ya Taifa, mali
ya mamlaka ya nchi na mali yoyote inayomilikiwa kwa pamoja na
wananchi, na pia kuiheshimu mali ya mtu mwingine.
(2) Kila mtu ana wajibu wa kulinda, kuhifadhi na kudumisha
rasilimali za nchi na maliasili za Taifa.
(3) Kila mtu anao wajibu wa kutunza vizuri mali ya mamlaka ya
nchi na mali inayomilikiwa kwa pamoja, kupiga vita aina zote za
uharibifu na ubadhirifu, na kuendesha uchumi wa Taifa kwa makini
kwa kuzingatia mipango endelevu na haki ya vizazi vijavyo.
Haki na
wajibu
muhimu
50.-(1) Kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya
kufaidi haki za msingi za binadamu, na matokeo ya kila mtu kutekeleza
wajibu wake kwa jamii, kama zilivyofafanuliwa katika Katiba hii.
(2) Kila raia katika Jamhuri ya Muungano anayo haki ya
kupata hifadhi sawa chini ya sheria za Jamhuri ya Muungano.
(3) Mtu yeyote katika Jamhuri ya Muungano hatakuwa na haki,
hadhi au cheo maalum kwa misingi ya nasaba, jadi au urithi wake.
(4) Ni marufuku kwa sheria yoyote kutoa haki, hadhi au cheo
‐ 21 ‐
maalum kwa mtu yeyote wa Jamhuri ya Muungano kwa misingi ya
nasaba, jadi au urithi.
(5) Ili watu wote wafaidi haki na uhuru uliotajwa katika Katiba
hii, kila mtu anao wajibu wa kutenda na kuendesha shughuli zake kwa
namna ambayo haitaingilia haki na uhuru wa watu wengine au maslahi
ya umma.
(b) Wajibu wa Mamlaka za Nchi
Hifadhi ya
haki za
binadamu
51.-(1) Serikali na mamlaka zote za nchi zinao wajibu wa
kuzingatia na kuhifadhi haki za binadamu ikiwa ni msingi wa uhuru kama
ilivyoainishwa katika Katiba hii.
(2) Haki na uhuru wa kila mtu kama zilivyoainishwa katika Katiba
hii zitaheshimiwa, kuhifadhiwa na kudumishwa na mamlaka za nchi,
mamlaka binafsi na kila mwananchi.
(3) Haki na uhuru ambao umeainishwa katika mikataba ya
kimataifa kuhusu haki za binadamu ambazo Jamhuri ya Muungano
imeridhia, isipokuwa masharti ambayo Jamhuri ya Muungano imeeleza
wazi kutojifunga nayo, zitakuwa Sehemu ya Haki za Binadamu
zilizoainishwa katika Sura hii.
Usimamizi
wa haki za
binadamu
52.-(1) Katika kutafsiri masharti ya Sura hii ya Haki za
Binadamu, Mahakama, Baraza au chombo kingine chochote cha
kufanya uamuzi kitazingatia mambo yafuatayo:
(a) haki ya usawa, utu na uhuru wa mtu binafsi;
(b) sheria za kimataifa na haki za binadamu; na
(c) haki za jamii na maslahi ya jamii kwa ujumla.
(2) Mtu anayeamini kuwa masharti yaliyomo katika Sura hii
yamekiukwa au yanaelekea kukiukwa na mamlaka, chombo cha
uamuzi, au sheria au sera yoyote, dhidi yake, anaweza kuwasilisha au
kufungua shauri katika Mahakama Kuu kwa hati maalumu ya maombi
kwa mujibu wa sheria za nchi ili kupata nafuu inayohitajika.
(3) Mahakama inaweza, kwa mujibu wa Ibara ndogo ya (1)
kutoa maelekezo itakayoona yanafaa, kuweka zuio, katazo au kuamuru
jambo lifanyike ambalo lilikuwa limenyimwa.
(4) Shauri katika Mahakama ya kudai haki za kikatiba kwa
mujibu wa masharti ya Ibara hii yanaweza kufunguliwa na:
(a) Mtu anayejiwakilisha mwenyewe au taasisi
inayowawakilisha wanachama wake;
(b) mtu anayemwakilisha mtu ambaye hawezi kujiwakilisha
mwenyewe kwa mujibu wa sheria; au
(c) mtu anayewakilisha kundi la watu wenye malengo
yanayofanana au jamii ya watu fulani wenye kuvunjiwa
haki husika.
Mipaka ya
haki za
binadamu
53.-(1) Haki zote zilizoainishwa katika Sura hii ya Katiba
endapo zitahitajika kuwekewa mipaka ni lazima mipaka hiyo kutumika
kwa uwazi na kidemokrasia kwa kuzingatia utu, usawa, uhuru na
vigezo muhimu, ikijumuisha:
‐ 22 ‐
(a) aina ya haki;
(b) umuhimu na sababu za kuweka mipaka;
(c) asili na ukubwa wa mpaka husika;
(d) uhusiano baina ya mpaka husika na sababu yake;
(e) njia nyepesi ya kufikia madhumuni ya matumizi ya mpaka
husika; na
(f) umuhimu wa kulinda usalama wa nchi.
(2) Bunge litatunga sheria, ambayo pamoja na mambo mengine,
itasimamia matumizi na utekelezaji wa masharti ya Ibara hii.
SURA YA TANO
URAIA KATIKA JAMHURI YA MUUNGANO
Uraia wa
Jamhuri ya
Muungano
54.-(1) Mtu ambaye,kablaya Katiba hii kuanza kutumika, ni raia wa Jamhuri
ya Muungano ataendelea kuwa raia wa Tanzania.
(2) Uraia wa Jamhuri ya Muungano ni wa aina mbili na utapatikana kwa njia
ya kuzaliwa au kujiandikisha.
Uraia wa
kuzaliwa
55.-(1) Kila mtu anayezaliwa Tanzania Bara au Zanzibar atakuwa raia wa
Jamhuri ya Muungano iwapo, wakati wa tarehe ya kuzaliwa, mama au baba yake ni
au alikuwa raia wa Jamhuri ya Muungano.
(2) Kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii, mtu aliyezaliwa nje ya Tanzania
atakuwa ni raia wa Jamhuri ya Muungano kwa kuzaliwa kuanzia tarehe ya kuzaliwa
kwake ikiwa wazazi wake au mmoja kati ya wazazi wake ni raia wa Jamhuri ya
Muungano.
(3) Endapo mmoja kati ya wazazi alifariki kabla ya mtu huyo kuzaliwa,
uraia wa mzazi huyo wakati wa kifo chake unatumika, kwa madhumuni ya
kutambua uraia wa mtu huyo aliyezaliwa baada ya mzazi aliyefariki kama kwamba
mzazi huyo alikuwa anaishi hadi kuzaliwa kwa mtu huyo.
(4) Mtoto mwenye umri chini ya miaka saba akikutwa ndani ya mipaka ya
Jamhuri ya Muunganokatika mazingira ambayo wazazi wake hawajulikani,
atahesabika kuwa ni raia wa Jamhuri ya Muungano wa kuzaliwa.
(5) Mtoto aliye na umri wa chini ya miaka kumi na nane ambaye wazazi
wake sio raia wa Tanzania, akiasiliwa na raia wa Jamhuri ya Muungano, kwa
kuasiliwa kwake huko, kutawezesha mtoto huyo kuwa raia wa Jamhuri ya
Muungano wa kujiandikisha.
Uraia wa
kuandikishwa
56.-(1) Mara baada ya kuanza kutumika kwa Katiba hii, mtu ambaye
amekuwa mkazi wa Tanzania Bara au Zanzibar kwa muda uliowekwa na sheria
inayotumika Tanzania Bara au Zanzibar, na ambaye ametimiza masharti yote ya
sheria ya Bunge la Tanzania Bara au Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, anaweza
kuomba kuandikishwa kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano.
(2) Mtu aliyefunga ndoa na raia wa Jamhuri ya Muunganoanaweza kutuma
maombi ya kuandikishwa kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano.
(3)Endapo ndoa iliyorejewa katika Ibara ndogo ya (2) itavunjika, kama mtu
huyo hakuukana uraia wake, ataendelea kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano.
(4) Mtoto aliyezaliwa katika ndoa iliyorejewa katika Ibara ndogo ya (2),
ataendelea kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano isipokuwa kama ataukana uraia huo
au ataomba na kupata uraia wa nchi nyingine.
‐ 23 ‐
SURA YA SITA
MUUNDO WA JAMHURI YA MUUNGANO
Muundo wa
Muungano
57.-(1) Jamhuri ya Muungano itakuwa na muundo wa shirikisho lenye
serikali tatu ambazo ni:
(a) Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
(b) Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar; na
(c) Serikali ya Tanzania Bara.
(2) Shughuli za Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kusimamiwa
na:
(a) Serikali ya Jamhuri ya Muungano;
(b) Bunge la Jamhuri ya Muungano; na
(c) Mahakama ya Jamhuri ya Muungano.
(3) Muundo, madaraka na mambo mengine ya kiutendaji yahusuyo
Serikali yaTanzania Bara na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar yataainishwa
katika Katiba za Washirika wa Muungano.
Vyombo
vya utendaji
vya Jamhuri
ya
Muungano
58.-(1) Serikali ya Jamhuri ya Muungano itakuwa ndiyo chombo
chenye mamlaka ya utendaji, Bunge litakuwa na mamlaka ya kutunga sheria
kwa mambo ya Muungano na kusimamia utekelezaji wa shughuli za Serikali
ya Jamhuri ya Muungano na Mahakama itakuwa ni chombo cha utoaji haki.
(2) Kila chombo kilichotajwa katika ibara hii kitaundwa na kutekeleza
majukumu yake kwa kufuata masharti ya Katiba hii.
Mamlaka
ya Serikali
ya
Muungano
59.-(1) Serikali ya Jamhuri ya Muungano itakuwa na mamlaka ya
utekelezaji kwa mambo yote yaliyoorodheshwa kuwa Mambo ya Muungano, na
wakati inapotekeleza majukumu yake, itazingatia mamlaka yake iliyopewa chini
ya Katiba hii.
(2)Utekelezaji wa majukumu ya Serikali utafanywa kwa namna na kwa
misingi iliyowekwa na Katiba hii au sheria iliyotungwa na Bunge.
(3) Bila ya kuathiri aukukiuka masharti ya Ibara hii, Serikali ya Jamhuri
ya Muungano, kwa makubaliano na masharti maalum baina yake na Serikali ya
Zanzibar au Serikali ya Tanzania Bara, inaweza kutekeleza jambo lolote lililo
chini ya mamlaka ya Serikali ya Zanzibar au Serikali ya Tanzania Bara kwa
mujibu wa masharti ya makubaliano hayo.
Mambo ya
Muungano
60. Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali ya Jamhuri ya
Muungano, na kwa ajili ya mgawanyo wa madaraka juu ya shughuli hizo
baina ya vyombo vilivyotajwa katika Ibara ya 58, Serikali ya Muungano
itakuwa na mamlaka juu ya mambo ya Muungano yalivyoorodheshwa katika
Nyongeza ya Katiba hii.
Washirika
wa
Muungano
61.-(1) Kwa mujibu wa Katiba hii, Washirika wa Muungano ni
Tanzania Bara na Zanzibar.
(2) Serikali ya Tanzania Bara itakuwa na mamlaka juu ya mambo yote
(5) Bunge litatunga sheria, pamoja na mambo mengine, kusimamia masuala
yanayohusu uraia wa Jamhuri ya Muungano.
‐ 24 ‐
yasiyo ya Muungano yahusuyo Tanzania Bara.
(3) Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itakuwa na mamlaka juu ya
mambo yote yasiyo ya Muungano yahusuyo Zanzibar.
(4) Washirika wa Muungano watatekeleza majukumu yao kwa
kuzingatia masharti ya Katiba hii na Katiba zao.
(5) Washirika wa Muungano watakuwa na hadhi na haki sawa ndani
ya Jamhuri ya Muungano na watatekeleza majukumu yao kwa masuala yote
yasiyo ya Muungano katika mamlaka ya Washirika wa Muungano kwa
mujibu wa masharti yatakayowekwa na Katiba za Washirika wa Muungano.
Mamlaka
ya
Washirika
wa
Muungano
62.-(1) Kila Mshirika wa Muungano atakuwa na mamlaka na haki zote
juu ya mambo yote yasiyo ya Muungano, na katika utekelezaji wa mamlaka
hayo, kila Mshirika wa Muungano atazingatia misingi ya ushirikiano na
mshirika mwingine kwa kuzingatia haki na usawakwa ajili ya ustawi ulio bora
kwa wananchi wa pande zote mbili za Jamhuri ya Muungano.
(2) Bila ya kuathiri mipaka iliyowekwa na Katiba hii, kila Mshirika wa
Muungano atakuwa na uwezo na uhuru wa kuanzisha mahusiano au
ushirikiano na jumuiya au taasisi yoyote ya kikanda au kimataifa kwa mambo
yaliyo chini ya mamlaka yake kwa mujibu wa Katiba ya Mshirika wa
Muungano.
(3) Mshirika wa Muungano anaweza, wakati wa kutekeleza majukumu
yake chini ya Ibara ndogo ya (2), kuomba mashirikiano kutoka Serikali ya
Jamhuri ya Muungano kwa ajili ya kufanikisha mahusiano na jumuiya au
taasisi ya kimataifa au kikanda, na Serikali ya Jamhuri Muungano inaweza
kutoa ushirikiano kwa mshirika huyo kwa namna itakavyohitajika.
Mahusiano
kati ya
Washirika
wa
Muungano
63.-(1) Kila Mshirika wa Muungano anaweza, katika kutekeleza
majukumu yake katika maeneo mbalimbali, kutekeleza majukumu hayo
kwa misingi ya kushirikiana na kushauriana na Mshirika wa Muungano
mwingine au baina ya Mshirika wa Muungano na Serikali ya Jamhuri ya
Muungano kwa lengo la kukuza na kulinda maslahi ya Taifa na maendeleo
ya wananchi.
(2) Washirika wa Muungano na Serikali ya Jamhuri ya Muungano
wanaweza kushauriana na kushirikiana katika mambo ya uongozi, utawala,
vyombo vya uwakilishi na kimahakama.
(3) Utendaji wa Serikali za Washirika wa Muungano au wa chombo
chochote kati ya vyombo vya serikali hizo na uendeshaji wa shughuli,
utatekelezwa kwa kuzingatia umoja wa Jamhuri ya Muungano na nia na
umuhimu wa haja ya kukuza umoja wa kitaifa na kudumisha heshima ya
Taifa.
Mawaziri
Wakaazi
64.-(1) Kila Mshirika wa Muungano atateua Waziri Mkaazi
atakayeratibu na kusimamia mahusiano baina ya Serikali za Washirika na
kati ya Serikali ya Mshirika na Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
(2)Mawaziri Wakaazi watakuwa na ofisi zao na watafanya kazi
wakiwa Makao Makuu ya Serikali ya Muungano.
(3) Pamoja na majukumu mengine watakayopangiwa na Serikali
za Washirika wa Muungano, Mawaziri Wakaazi watakuwa na majukumu
yafuatayo:
‐ 25 ‐
Wajibu wa
kulinda
Muungano
66.-(1) Bila ya kuathiri wajibu wa kila raia kwa mujibu wa Katiba
hii, viongozi wakuu wenye mamlaka ya utendaji katika Jamhuri ya
Muungano waliotajwa katika Ibara ndogo ya (3) watawajibika, kila mmoja
wao katika kutekeleza madaraka waliyopewa kwa mujibu wa Katiba hii au
Katiba za Washirika wa Muungano kuhakikisha kuwa analinda, kuimarisha
na kudumisha Muungano.
(2) Kwa madhumuni ya masharti ya Ibara ndogo ya (1), kila
mmojawapo wa viongozi wakuu waliotajwa katika Ibara ndogo ya (3),
kabla ya kushika madaraka yake ataapa kuutetea na kuudumisha
Muungano kwa mujibu wa Katiba hii.
(3) Viongozi Wakuu wanaohusika na masharti ya Ibara hii ni:
(a) Rais wa Jamhuri ya Muungano;
(b) Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano;
(c) Rais wa Tanzania Bara; na
(d) Rais wa Zanzibar.
SURA YA SABA
SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO
SEHEMU YA KWANZA
SERIKALI, RAIS NA MAKAMU WA RAIS
(a) Serikali
Serikali ya
Jamhuri ya
Muungano
67.-(1) Kutakuwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania ambayo itaundwa na Rais, Makamu wa Rais na Mawaziri wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
(2) Serikali ya Jamhuri ya Muungano itakuwa na mamlaka juu
ya mambo yote ya Muungano katika Jamhuri ya Muungano.
(3) Mamlaka ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano yatahusu
utekelezaji na hifadhi ya Katiba hii na pia mambo mengine ambayo
(a) kushughulikia mambo yasiyo ya Muungano yanayohusu
ushirikiano au mahusiano ya kimataifa; na
(b) kuwa kiungo baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano na
Serikali za Washirika wa Muungano na baina ya Serikali za
Washirika wa Muungano.
Mamlaka ya
wananchi
65.-(1) Serikali ya Jamhuri ya Muungano itapata mamlaka yake
kutoka kwa wananchi kupitia uchaguzi wa kidemokrasia utakaoendeshwa
na kusimamiwa na chombo kitakachopewa mamlaka na Katiba hii, na
vilevile, Serikali ya Tanzania Bara na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
zitapata mamlaka kupitia uchaguzi wa kidemokrasia utakaoendeshwa na
kusimamiwa na vyombo vitakavyopewa mamlaka chini ya Katiba zao.
(2) Serikali za Washirika wa Muungano, katika kutekeleza
mamlaka zao, zitawajibika kustawisha mamlaka ya wananchi kwa kugatua
madaraka kwa serikali za mitaa zitakazoanzishwa kwa mujibu wa Katiba
ya Tanzania Bara au Katiba ya Zanzibar, kama itakavyokuwa.
‐ 26 ‐
yameainishwa katika sheria za nchi.
(4) Madaraka ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano
yatatekelezwa na Rais mwenyewe, au kwa kukasimu madaraka hayo
kwa Makamu wa Rais au watu wengine wenye madaraka katika
utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
(5) Ifahamike kwamba masharti yaliyomo katika Ibara hii
hayatahesabiwa kwamba:
(a) yanahamishia kwa Rais madaraka yoyote ya kisheria
yaliyowekwa na sheria mikononi mwa mtu au mamlaka
yoyote ambayo si Rais; au
(b) yanalizuia Bunge kukabidhi madaraka yoyote ya kisheria
mikononi mwa mtu au watu au mamlaka nyingine yoyote
ambayo si Rais.
(b) Rais
Rais wa
Jamhuri
ya
Muungano
68.-(1) Kutakuwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano.
(2) Rais wa Jamhuri ya Muungano atakuwa Mkuu wa Nchi,
Kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu na:
(a) atakuwa alama na taswira ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na watu wake;
(b) atakuwa alama ya umoja na uhuru wa nchi na mamlaka
yake;na
(c) atakuwa na dhamana ya kukuza na kuhifadhi umoja wa
kitaifa.
Madaraka
na
majukumu
ya Rais
69.-(1)Rais akiwa Mkuu wa Nchi, atakuwa na madaraka na
majukumu yafuatayo:
(a) kuisimamia na kuilinda Katiba;
(b) kulinda utaifa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
(c) kuhutubia na kufungua rasmi Bunge Jipya na kulivunja
Bunge baada ya kumaliza muda wake;
(d) kuhutubia na kufungua rasmi Kalenda ya Mwaka ya
Mahakama;
(e) kuidhinisha uwasilishaji Bungeni makisio ya mapato na
matumizi ya Serikali, Bunge na Mahakama katika mwaka
wa fedha;
(f) kuweka saini katika Muswada wa Sheria uliyopitishwa na
Bunge;
(g) kutunuku nishani za heshima kwa niaba ya Watu wa
Jamhuri ya Muungano kwa ujumla;
(h) kuteua Mabalozi,Watu watakaoiwakilisha Tanzania nje ya
nchi na wawakilishi wa nchi katika taasisi mbalimbali za
kimataifa;
(i) kupokea hati za utambulisho za Mabalozi wa nchi za nje
nchini;
(j) kutoa msamaha kwa mtu yeyote anayetumikia adhabu
‐ 27 ‐
iliyotolewa na Mahakama kwa mujibu wa sheria za nchi; na
(k) kuidhinisha utekelezaji wa adhabu ya kifo iliyotolewa kwa
mujibu wa sheria za nchi.
(2) Rais akiwa Amiri Jeshi Mkuu, atakuwa na madaraka na
majukumu yafuatayo:
(a) kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Ulinzi na Usalama wa
Taifa;
(b) kuamuru Majeshi ya Ulinzi kwenda vitani au kusitisha vita;
(c) kutia saini makubaliano ya amani au kusitisha vita;
(d) kutangaza hali ya hatari au hali ya kuzingirwa eneo fulani;
(e) kuteua Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama; na
(f) kuwapandisha vyeo maofisa wa vyombo vya ulinzi na
usalama katika ngazi mbalimbali na kutoa kamisheni kwa
maofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania.
(3) Akiwa Kiongozi wa Serikali, Rais wa Jamhuri ya Muungano
atakuwa na madaraka na majukumu yafuatayo:
(a) kuongoza vikao vya Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya
Muungano;
(b) kupanga, kuelekeza, kusimamia na kuratibu majukumu ya
wizara na taasisi za serikali;
(c) kuwateua Mawaziri na Naibu Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri
ya Muungano;
(d) kumteua Katibu Mkuu Kiongozi na Makatibu Wakuu;
(e) kumteua Mwanasheria Mkuu na Naibu Mwanasheria Mkuu wa
Serikali; na
(f) kuwateua makamishna wa Tume mbalimbali zilizoanzishwa
kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.
(4) Katika kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Ibara hii,
Rais ataepuka kujinasibisha, kwa namna yoyote ile, na chama chochote cha
siasa au kundi lolote kwa namna ambayo inaathiri umoja wa wananchi.
Utekelezaji
wa
madaraka
ya Rais
70.-(1) Katika utekelezaji wa madaraka ya Rais kwa mujibu wa
Sura hii na kwa kuzingatia masharti ya Ibara ndogo ya (3), Rais ana
mamlaka ya kuanzisha au kufuta nafasi za madaraka katika utumishi wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
(2)Rais atakuwa na madaraka ya kuteua watu wa kushika nafasi za
madaraka ya viongozi wanaowajibika kuweka sera za idara na taasisi za
Serikali, na watendaji wakuu wanaowajibika kusimamia utekelezaji wa
sera za idara na taasisi hizo katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya
Muungano.
(3) Katika utekelezaji wa madaraka kama ilivyoainishwa katika
Ibara ndogo ya (1) na (2), Rais atazingatia masharti kuhusu uthibitisho wa
Bunge katika nafasi za madaraka na vile vile ushauri wa mamlaka za
Serikali, Bunge au Mahakama zilizopewa madaraka ya kumshauri katika
kufanya uteuzi, kuanzisha au kufuta nafasi za madaraka katika utumishi wa
Serikali.
(4) Mamlaka ya kuwateua watu wengine wote wasiokuwa
viongozi wala watendaji wakuu, kushika nafasi za madaraka katika
‐ 28 ‐
utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano, na mamlaka ya
kuwapandisha vyeo watu hao, kuwaondoa katika madaraka, kuwafukuza
kazi, kuwasimamisha kazi na mamlaka ya kudhibiti nidhamu ya watu
waliokabidhiwa madaraka, yatakuwa mikononi mwa Tume za Utumishi na
mamlaka za nchi zilizotajwa na kupewa madaraka hayo na sheria za nchi.
(5) Masharti ya Ibara ndogo ya (2) na ya (3) hayazuii Rais
kuchukua hatua za kudhibiti nidhamu ya watumishi na utumishi katika
Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
Rais
kuzingatia
ushauri
71.-(1) Mbali na kuzingatia masharti yaliyomo katika Katiba hii,
na sheria za nchi, Rais atakuwa na wajibu wa kufuata na kuzingatia
ushauri atakaopewa na mamlaka za nchi, na endapo hakubaliani na
ushauri aliopewa sharti atoe sababu katika Baraza la Mawaziri kuhusu
sababu ya kutokubaliana na ushauri aliopewa.
(2) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (1), Rais hatalazimika
kuufuata ushauri aliopewa ambao unakwenda kinyume au kukiuka
masharti ya Katiba au haukuzi wala kuhifadhi maslahi ya taifa na wananchi
walio wengi.
Rais
kushindwa
kumudu
majukumu
yake
72.-(1) Endapo Baraza la Mawaziri litaona kuwa Rais hawezi
kumudu kazi zake kwa sababu ya maradhi ya mwili au akili, linaweza
kuwasilisha kwa Jaji Mkuu azimio la kumwomba Jaji Mkuu athibitishe
kwamba Rais, kwa sababu ya maradhi ya mwili au ya akili, hawezi
kumudu kazi zake.
(2) Baada ya kupokea azimio lililowasilishwa kwa mujibu wa Ibara
ndogo ya (1), Jaji Mkuu atateua bodi ya utabibu ambayo itachunguza suala
hilo na kumshauri Jaji Mkuu ipasavyo.
(3) Jaji Mkuu anaweza, baada ya kutafakari ushauri na ushahidi wa
kitabibu, kuwasilisha kwa Spika hati ya kuthibitisha kwamba kutokana na
maradhi ya mwili au akili, Rais ameshindwa kumudu kazi zake, na iwapo
Jaji Mkuu hatabatilisha hati hiyo ndani ya siku saba kutokana na Rais
kupata nafuu na kurejea kazini, basi itahesabiwa kwamba kiti cha Rais ki
wazi, na masharti yaliyomo katika Ibara ndogo ya (5) na (6) yatatumika.
(4) Bodi ya utabibu itakayoteuliwa kwa mujibu wa Ibara ndogo ya
(3) itajumuisha watu wasiopungua watatu watakaoteuliwa kutoka
miongoni mwa madaktari bingwa wanaotambuliwa na sheria inayohusu
madaktari ya Tanzania.
(5) Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki
dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi, kutomudu kazi zake kutokana
na maradhi ya mwili au akili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za
Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na kushika madaraka ya Rais kwa
muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano na kwa masharti
yaliyoelezwa katika Ibara ya 76.
(6) Mara tu baada ya kuapishwa, au kwa vyovyote vile ndani ya
kipindi kisichozidi siku kumi na nne tangu alipoapishwa, Rais:
(a) baada ya kushauriana na chama cha siasa anachotoka;au
(b) baada ya kushauriana na Baraza la Ulinzi naUsalama wa Taifa,
kwa Rais aliyetokana kwa utaratibu wa mgombea huru,
atapendekeza jina la mtu atakayekuwa Makamu wa Rais na uteuzi huo
‐ 29 ‐
utathibitishwa na Bunge kwa kura zaidi ya asilimia hamsini ya Wabunge
wote.
Utekelezaji
wa
majukumu
ya Rais
akiwa
hayupo
73.-(1) Ikitokea kwamba kiti cha Rais kiko wazi kutokana na
masharti yaliyomo katika Ibara ya 72 au endapo kiti cha Rais kiko wazi
kutokana na sababu nyingine yoyote, na endapo Rais atakuwa hayupo
katika Jamhuri ya Muungano, kazi na shughuli za Rais zitatekelezwa na
mmoja wapo wa wafuatao, kwa kufuata orodha kama ilivyopangwa, yaani–
(a) Makamu wa Rais au kama nafasi yake iko wazi au kama naye
hayupo au ni mgonjwa, basi;
(b) Waziri Mwandamizi; au
(c) kamaWaziri Mwandamizi nafasi yake iko wazi au kama naye
hayupo au ni mgonjwa, basi Waziri mwingine yeyote
atakayeteuliwa na Baraza la Mawaziri.
(2) Endapo yeyote kati ya watu waliotajwa katika aya ya (a), (b) na
(c) za Ibara ndogo ya (1) atatekeleza kazi na shughuli za Rais kutokana na
sababu kwamba mtu mwingine anayemtangulia katika orodha hiyo hayupo,
basi mtu huyo ataacha kutekeleza kazi na shughuli hizo mara tu mtu huyo
mwingine anayemtangulia atakaporejea na akashika na kuanza kutekeleza
kazi na shughuli za Rais.
(3) Mtu yoyote atakayekaimu nafasi ya madaraka ya Rais, kwa
namna yoyote ile, hatakuwa na madaraka katika mambo yafuatayo:
(a) kuteua aukumuondoa madarakani kiongozi yoyote yule
aliyeteuliwa na Rais kwa mujibu wa Katiba hii; au
(b) jambo jingine lolote kama litakavyoainishwa na Rais katika hati
ya kukasimu madaraka yake.
(4) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (2) na (3), Rais atakasimu
madaraka yake kwa hati maalumu aliyotia saini yake.
(c) Uchaguzi wa Rais
Uchaguzi
wa Rais
74.-(1) Rais atachaguliwa na wananchi kwa mujibu wa masharti ya
Katiba hii na kwa mujibu wa sheria za nchi.
(2) Nafasi ya madaraka ya Rais itakuwa wazi na uchaguzi wa Rais
utafanyika baada ya Rais kumaliza muda wake wa kuwa madarakani kwa
mujibu wa Katiba hii.
(3) Endapo kutatokea jambo lolote kati ya mambo yafuatayo,
hakutakuwa na Uchaguzi wa Rais na badala yake nafasi hiyo itajazwa na
Makamu wa Rais kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii, yaani:
(a) Rais kujiuzulu;
(b) Rais kupoteza sifa za kuchaguliwa katika nafasi ya
madaraka ya Rais;
(c) Rais kushtakiwa Bungeni na kuondolewa katika madaraka kwa
mujibu wa Katiba hii;
(d) ikithibitika kwamba Rais hawezi kumudu nafasi ya madaraka
ya Rais; au
(e) Rais kufariki dunia.
Sifa za
Rais
75. Mtu atakuwa na sifa ya kuchaguliwa kushika nafasi ya
‐ 30 ‐
madaraka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano ikiwa:
(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa
Katiba hii na sheria za nchi;
(b) ni mwenye akili timamu;
(c) angalau mmoja kati ya wazazi wake ni raia wa kuzaliwa wa
Jamhuri ya Muungano;
(d) wakati wa kugombea, ana umri usiopungua miaka arobaini;
(e) anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri
ya Muungano kwa mujibu wa Katiba hii;
(f) anayo angalau shahada ya kwanza ya chuo kikuu
kinachotambuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi;
(g) ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha
siasa au mgombea huru;
(h) sera zake au sera za chama chake si za mrengo wa kuligawa
Taifa kwa misingi ya ukabila, udini, rangi au jinsia;
(i) ni mwadilifu na anafuata maadili ya Taifa;
(j) mwenendo wake binafsi hautiliwi shaka na jamii;
(k) hajatiwa hatiani kwa kosa lolote la jinailinalohusu kukosa
uaminifu; na
(l) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi
Mkuu hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa
kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.
Haki ya
kuchaguli
wa tena
76.-(1) Mtu ambaye ni Rais anaweza kuchaguliwa tena kushika kiti
hicho kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
(2) Mtu hatakuwa na sifa ya kugombea na kuchaguliwa zaidi ya
vipindi viwili katika nafasi ya madaraka ya Rais.
(3) Mtu aliyewahi kuwa Rais wa Tanzania Bara au Zanzibar
hatapoteza sifa za kugombea na kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya
Muungano kwa sababu aliwahi kushika nafasi ya madaraka ya Rais wa
Tanzania Bara au Rais wa Zanzibar.
(4) Endapo mtu aliyekuwa anashika nafasi ya madaraka ya
Makamu wa Rais, atashika nafasi ya madaraka ya Rais kwa mujibu wa
masharti ya Ibara ya 72 kwa kipindi kisichozidi miezi thelathini na sita, mtu
huyo anayo haki ya kugombea nafasi ya madaraka ya Rais katika uchaguzi
wa Rais utakaofuata.
(5) Mtu aliyechaguliwa kushika nafasi ya madaraka ya Rais kwa
mujibu wa masharti ya Ibara ndogo ya (4), atahesabiwa kuwa ameshika
nafasi ya madaraka ya Rais katika vipindi viwili na hataruhusiwa kugombea
nafasi ya madaraka ya Rais katika kipindi kingine.
Utaratibu
wa
Uchaguzi
wa Rais
77.-(1) Katika Uchaguzi wa Rais, kila chama cha siasa
kinachopenda kushiriki katika uchaguzi wa Rais kitawasilisha kwa
Tume Huru ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano, kwa mujibu wa sheria za
nchi, jina la mwanachama mmoja anayependekezwa kwa nafasi ya
madaraka ya Rais.
(2) Endapo ni Mgombea huru, kwa kuzingatia sifa zilizoainishwa
katika Katiba hii, atawasilisha jina lakekwenye Tume Huru ya Uchaguzi.
(3) Mapendekezo ya majina ya wagombea katika uchaguzi wa Rais
‐ 31 ‐
yatawasilishwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi katika siku na kwa utaratibu
uliyoainishwa katika sheria za nchi.
(4) Endapo itafika saa na siku iliyotajwa kwa ajili ya
kuwasilisha mapendekezo ya majina ya wagombea, ni mgombea mmoja tu
ambaye anapendekezwa kuwa halali, Tume Huru ya Uchaguzi itawasilisha
jina lake kwa wananchi, nao watapiga kura ya kumkubali au
kumkataa kwa mujibu wa masharti yaliyoainishwa katika sheria za
nchi.
(5) Uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano utafanyika siku
itakayoteuliwa na Tume Huru ya Uchaguzi kwa mujibu wa sheria za nchi.
(6) Mgombea wa nafasi ya madaraka ya Rais atatangazwa kuwa
amechaguliwa kuwa Rais iwapo atapata kura zinazozidi asilimia
hamsini ya kura zote zilizopigwa kwa nafasi ya madaraka ya Rais.
(7) Endapo katika Uchaguzi wa Rais hakuna mgombea
aliyekidhi masharti ya Ibara ndogo ya (6), basi uchaguzi utarudiwa
ndani ya siku sitini kwa wagombea walioshika nafasi ya kwanza na ya
pili.
Malalamiko
kuhusu
uhalali wa
uchaguzi
wa Urais
78.-(1) Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ndogo ya (2), endapo
mtu yeyote aliyeshiriki kama mgombea nafasi ya madaraka ya Rais
katika Uchaguzi wa Rais hakuridhika na matokeo ya uchaguzi huo,
anaweza kuwasilisha malalamiko katika Mahakama ya Juu kupinga
matokeo wa Rais yaliyotangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi.
(2) Malalamiko ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Rais
yatawasilishwa Mahakama ya Juu ndani ya muda wa siku saba baada ya
siku ya kutangazwa kwa matokeo ya Uchaguzi wa Rais.
(3) Mahakama ya Juu itasikiliza na kutoa uamuzi wa shauri la
kupinga matokeo ya uchaguzi wa Rais katika kipindi cha siku kumi na
nne tangu kupokea malalamiko yaliyowasilishwa kwa mujibu wa Ibara
ndogo ya (2) na uamuzi huo utakuwa wa mwisho.
(4) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (3), Mahakama ya Juu
inaweza kutoa uamuzi bila kutoa sababu za uamuzi na sababu hizo
zikatolewa ndani ya kipindi kisichozidi siku thelathini tangu siku ya
kutoa uamuzi.
(5) Iwapo Mahakama ya Juu itaamua kuwa matokeo ya Uchaguzi
wa Rais si halali, Uchaguzi wa Rais utarudiwa ndani ya siku sitini baada
ya uamuzi kutolewa.
Kiapo cha
Rais
79.-(1) Rais Mteule ataapishwa na Jaji Mkuu na atashika nafasi
ya madaraka ya Rais mapema iwezekanavyo baada ya kutangazwa
kwamba amechaguliwa kuwa Rais, lakini kwa hali yoyote, hatashika
madaraka kabla ya kupita siku thelathini kutoka siku matokeo ya Uchaguzi
wa Rais yalipotangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi au siku ya kuthibitishwa
na Mahakama ya Juu.
(2) Isipokuwa kama atajiuzulu au atafariki mapema zaidi, Rais
Mteule atashika nafasi ya madaraka ya Rais kwa muda wa miaka mitano
tangu siku alipochaguliwa kuwa Rais.
(3) Rais atashika nafasi ya madaraka ya Rais hadi-
(a) siku ambapo Rais mteule ataapa kushika nafasi ya madaraka
‐ 32 ‐
ya Rais;
(b) siku ambapo atafariki dunia;
(c) siku atakapojiuzulu; au
(d) atakapoacha kushika nafasi ya madaraka ya Rais kwa mujibu
wa masharti ya Katiba hii.
(d) Masharti Mahsusi kuhusu Rais
Madaraka
ya
kutangaza
vita
80.-(1) Kwa kuzingatia masharti ya Ibara hii, Rais atakuwa na
mamlaka ya kutangaza kuwepo kwa vita kati ya Jamhuri ya Muungano na
nchi nyingine au kundi lolote lile baada ya kupata idhini ya Bunge.
(2)Bila kujali masharti ya Ibara ndogo ya (1), endapo Jamhuri ya
Muungano itakuwa imevamiwa au kundi lolote limeanzisha vita ndani ya
Jamhuri ya Muungano basi, Rais anaweza, baada ya kushauriana na Baraza
la Ulinzi na Usalama la Taifa, kutangaza kuwepo kwa vita katika Jamhuri ya
Muungano.
(3) Baada ya kutoa tangazo kwa mujibu wa Ibara ndogo ya
(2), Rais atalitaarifu Bunge kwa kupeleka nakala ya tangazo hilo kwa
Spika wa Bunge ambaye, ndani ya siku kumi na nne kuanzia tarehe
ya tangazo, ataitisha Mkutano wa Bunge ili kulijulisha Bunge kuhusu
tangazo lililotolewa na Rais.
Madaraka
ya Rais
kutangaza
hali ya
hatari
81.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, au sheria
iliyotungwa na Bunge kwa ajili hiyo, Rais anaweza, baada ya kushauriana
na Baraza la Ulinzi na Usalama wa Taifa, kutangaza hali ya hatari au hali
ya kuzingirwa kwa eneo fulani la Jamhuri ya Muungano au katika sehemu
yake yoyote.
(2) Rais anaweza tu kutangaza kuwa kuna hali ya hatari iwapo-
(a) Jamhuri ya Muungano iko katika vita;
(b) kuna hatari hasa kwamba Jamhuri ya Muungano inakaribia
kuvamiwa na kuingia katika hali ya vita;
(c) kuna hali halisi ya kuvurugika kwa amani katika jamii au
kutoweka kwa usalama wa jamii katika Jamhuri ya Muungano
au sehemu yake yoyote kiasi kwamba ni lazima kuchukua hatua
za pekee ili kurejesha amani na usalama;
(d) kuna hatari dhahiri na kubwa, kiasi kwamba amani katika jamii
itavurugika na usalama wa raia kutoweka katika Jamhuri ya
Muungano au sehemu yake yoyote ambayo haiwezi kuepukika
isipokuwa kwa kutumia mamlaka ya pekee;
(e) karibu kutatokea tukio la hatari au tukio la balaa au la baa ya
kimazingira ambalo linatishia jamii au sehemu ya jamii katika
Jamhuri ya Muungano; au
(f) kuna aina nyingineyo ya hatari ambayo kwa dhahiri ni tishio
kwa usalama wa nchi.
(3) Endapo inatangazwa kwamba kuna hali ya hatari katika Jamhuri
ya Muungano au eneo lolote la Jamhuri ya Muungano, Rais atawasilisha
nakala ya tangazo hilo kwa Spika wa Bunge ambaye, ndani ya siku
zisizozidi kumi na nne tangu kutolewa kwa tangazo hilo, ataitisha mkutano
‐ 33 ‐
wa Bunge ili kulijulisha Bunge juu ya taarifa ya hali ya hatari
iliyotangazwa na Rais.
(4) Bunge linaweza kutunga sheria itakayoweka masharti kuhusu
nyakati na taratibu ambazo zitawawezesha baadhi ya watu wenye
kusimamia utekelezaji wa mamlaka ya Serikali katika sehemu mahsusi za
Jamhuri ya Muungano kumuomba Rais kutumia madaraka aliyopewa na
Ibara hii kuhusiana na yoyote kati ya sehemu hizo endapo katika sehemu
hizo, kunatokea lolote kati ya hali zilizotajwa katika aya ya (c), (d) na (e)
za Ibara ndogo ya (2) na hali hiyo haivuki mipaka ya sehemu hizo, na pia,
kwa ajili ya kufafanua utekelezaji wa mamlaka ya Serikali wakati wa hali
ya hatari.
(5) Tangazo la hali ya hatari lililotolewa na Rais kwa mujibu wa
Ibara hii litakoma kutumika iwapo litafutwa na Rais.
(6) Kwa madhumuni ya kuondoa mashaka juu ya ufafanuzi au
utekelezaji wa masharti ya Ibara hii, masharti ya sheria iliyotungwa na
Bunge na ya sheria nyingine yoyote inayohusu utangazaji wa hali ya hatari
kama ilivyotajwa katika Ibara hii, yatatumika tu katika sehemu ya Jamhuri
ya Muungano ambapo hali hiyo ya hatari imetangazwa.
Mamlaka
ya Rais
kutoa
msamaha
82.-(1) Rais kwa mamlaka ya Mkuu wa Nchi, anayo mamlaka ya:
(a) kutoa msamaha kwa mtu yeyote aliyepatikana na hatia kwa
kosa lolote mbele ya Mahakama dhidi ya Jamhuri ya
Muunganokwa masharti maalum kama yatakavyoainishwa
katika sheria iliyotungwa na Bunge; au
(b) kubatilisha adhabu ya kifo kuwa adhabu ya kifungo cha
maisha.
(2) Masharti ya Ibara hii yatatumika kwa mtu aliyehukumiwana
kuadhibiwa akiwa Zanzibar na kwa adhabu zilizotolewa Zanzibar kwa
mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge inayotumika Zanzibar, hali
kadhalika, masharti hayo yatatumika kwa mtu aliyehukumiwa na
kuadhibiwa Tanzania Bara kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge
inayotumika Tanzania Bara.
(3) Kwa madhumuni ya Ibara hii, kutakuwa na Kamati ya Taifa ya
Ushauri ambayo itakuwa na wajibu wa kumshauri Rais kuhusu kutoa
msamaha kwa mtu yeyote aliyepatikana na hatia mahakamani na anatumikia
adhabu.
(4) Utaratibu wa namna ya utekelezaji wa madaraka kwa mujibu
wa Ibara hii, muundo, majukumu na utendaji kazi wa Kamati ya Taifa ya
Ushauri vitaainishwa na sheria itakayotungwa na Bunge.
Kinga
dhidi ya
mashtaka
ya Rais
83.-(1) Wakati Rais akiwa madarakani, hatashitakiwa wala mtu
yeyote hataendesha mashtaka ya aina yoyote dhidi yake mahakamani kwa
ajili ya kosa lolote la jinai.
(2) Wakati Rais ameshika madaraka kwa mujibu wa Katiba hii,
haitaruhusiwa kufungua mahakamani shauri la madai kuhusu jambo lolote
alilolitenda au alilokosa kulitenda yeye binafsi kama raia ama kabla au
baada ya kushika madaraka ya Rais, ila tu kama angalau siku thelathini
kabla ya shauri kufunguliwa mahakamani, Rais atapewa au ametumiwa
taarifa ya madai kwa maandishi kwa kufuata utaratibu uliowekwa kwa
‐ 34 ‐
mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge, na taarifa hiyo ikiwa inatoa maelezo
kuhusu chanzo cha shauri hilo, kiini cha madai yenyewe, jina lake na anwani
ya mahali anapoishi huyo mdai na jambo hasa analodai.
(3) Isipokuwa kama ataacha kushika madaraka ya Rais kutokana
na kura ya kutokuwa na imani na Rais, haitakuwa halali kwa mtu
kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la madai
dhidi ya mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya kuacha
madaraka hayo kutokana na jambo alilofanya wakati alipokuwa bado
anashika madaraka ya Rais.
Bunge
kumshtaki
Rais
84.-(1) Bunge linaweza kupitisha azimio la kumuondoa Rais
madarakani endapo itatolewa hoja ya kumshtaki Rais na ikapitishwa kwa
mujibu wa masharti ya Ibara hii.
(2) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya Ibara hii, hoja
yoyote ya kumshtaki Rais haitatolewa isipokuwa tu kama itadaiwa
kwamba Rais ametenda mojawapo ya makosa yafuatayo:
(a) ukiukwaji mkubwa wa masharti ya Katiba hii;
(b) makosa makubwa ya jinai;
(c) kuzuia kwa namna yoyote ile yeyekuchunguzwa kwa mujibu
wa Ibara hii;
(d) uhaini;
(e) rushwa;
(f) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha nafasi ya madaraka ya
Rais wa Jamhuri ya Muungano;
(g) kupuuza au kukataa kutekeleza uamuzi au amri halali za
Mahakama; au
(h) ametenda vitendo ambavyo vinakiuka kanuni zamaadili au miiko
ya uongozi;
(3) Bunge halitapitisha hoja ya kumshtaki Rais isipokuwa tu kama-
(a) haitatolewa hoja ya namna hiyo ndani ya miezi kumi na miwili
tangu hoja kama hiyo ilipotolewa na ikakataliwa na Bunge; na
(b) taarifa ya maandishi, iliyotiwa saini na kuungwa mkono na
Wabunge wasiopungua asilimia ishirini na tano ya Wabunge
wote itawasilishwa kwa Spika siku kumi na nne kabla ya
kikao ambapo hoja hiyo inakusudiwa kutolewa Bungeni.
(4) Taarifa itakayowasilishwa kwa mujibu wa Ibara ndogo ya
(3)(b) itafafanua makosa aliyoyatenda Rais, na itapendekeza kuwa Tume
ya Uchunguzi iundwe ili ichunguze tuhuma zilizotolewa dhidi ya Rais.
(5) Wakati wowote baada ya kupokea taarifa iliyotiwa saini na
Wabunge na kujiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajili ya
kuwasilisha hoja yametimizwa, Spika atamruhusu mtoa hoja
kuiwasilisha mbele ya Bunge na kisha Spika atalitaka Bunge, bila ya
kufanya majadiliano, lipige kura juu ya hoja ya kuunda Kamati ya
Uchunguzi.
(6) Endapo hoja ya kuunda Kamati ya Uchunguzi itaungwa
mkono na Wabunge wasiopungua asilimia sabini na tano ya Wabunge
wote, Spika atatangaza majina ya wajumbe wa Kamati ya Uchunguzi.
‐ 35 ‐
(7) Kamati ya Uchunguzi, kwa madhumuni ya Ibara hii, itakuwa na
wajumbe wafuatao:
(a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, ambaye atakuwa
Mwenyekiti wa Kamati;
(b) Jaji Mkuu wa Tanzania Bara;
(c) Jaji Mkuu wa Zanzibar; na
(d) wajumbe wengine sita watakaoteuliwa na Spika.
(8) Endapo Bunge litapitisha hoja ya kuunda Kamatiya Uchunguzi,
Rais atahesabiwa kuwa hayupo kazini na nafasi ya madaraka ya Rais
yatatekelezwa na Makamu wa Rais hadi Spika atakapomfahamisha Rais juu
ya Azimio la Bunge kuhusiana na mashtaka yaliyotolewa dhidi yake.
(9) Ndani ya siku saba baada ya Kamati ya Uchunguzi kuundwa,
itachunguza na kuchambua mashtaka dhidi ya Rais, pamoja na kumpatia
Rais fursa ya kujieleza, kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Kanuni za
Kudumu za Bunge.
(10) Mapema iwezekanavyo, na kwa vyovyote vile katika muda
usiozidi siku tisini, Kamati ya Uchunguzi itatoa taarifa yake kwa Spika.
(11) Baada ya Spika kupokea taarifa ya Kamati ya Uchunguzi,
taarifa hiyo itawasilishwa Bungeni kwa kufuata utaratibu uliowekwa na
Kanuni za Kudumu za Bunge.
(12) Baada ya taarifa ya Kamati ya Uchunguzi kuwasilishwa,
Bunge litaijadili taarifa hiyo na kutoa fursa kwa Rais kujieleza, na kisha,
kwa kura za Wabunge wasiopungua asilimia sabini na tano ya Wabunge
wote, Bunge litapitisha azimio kuwa mashtaka dhidi ya Rais ama
yamethibitika au hayakuthibitika.
(13) Endapo Bunge litapitisha azimio kuwa mashtaka dhidi ya Rais
yamethibitika na kwamba hastahili kuendelea kushika nafasi ya madaraka
ya Rais, Spika atamfahamisha Rais na juu ya Azimio la Bunge na Rais
atakuwa ameondolewa madarakani na Makamu wa Rais ataapishwa mara
moja kushika madaraka ya Rais.
(14) Endapo Rais ataacha kushika nafasi ya madaraka ya Rais
kutokana na mashtaka dhidi yake kuthibitika, hatakuwa na haki ya kupata
malipo yoyote ya uzeeni, posho wala kupata haki au nafuu nyingine
anazopewa Rais au mtu aliyekuwa Rais kwa mujibu wa Katiba au sheria za
nchi.
Maslahi
ya Rais
85.-(1) Rais atalipwa mshahara na malipo mengineyo kama
yatakavyoainishwa na Tume ya Utumishi wa Umma na atakapostaafu
atapokea malipo ya uzeeni na stahili nyingine kutoka Mfuko Mkuu wa
Hazina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
(2) Mshahara na malipo mengineyo yote ya Rais
hayatapunguzwa wakati Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka
yake kwa mujibu wa Katiba hii.
‐ 36 ‐
(e) Makamu wa Rais
Makamu
wa Rais wa
Jamhuri ya
Muungano
86.-(1) Kutakuwa na Makamu wa Rais ambaye atakuwa ndiye
Msaidizi Mkuu wa Rais kuhusu mambo yote ya Jamhuri ya Muungano kwa
jumla na:
(a) atafanya kazi zote atakazoagizwa na Rais;
(b) atakuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mahusiano ya Serikali; na
(c) atafanya kazi zote za Rais kama Rais hayuko kazini au yuko nje
ya nchi.
(2) Katika utekelezaji wa madaraka yake, Makamu wa Rais
atatekeleza au kusababisha utekelezaji wa jambo lolote au mambo yoyote
ambayo Rais ataagiza kwamba yatekelezwe.
(3) Bila kuathiri masharti ya Katiba hii, Makamu wa Rais
atawajibika kwa Rais kuhusu utekelezaji wa majukumu yake.
87.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 72,Makamu wa Rais
atapatikana kwa kuchaguliwa katika uchaguzi pamoja na Rais, baada ya
kupendekezwa na chama chake au mgombea huru wakati ule ule
anapopendekezwa mgombea nafasi ya madaraka yaRais na watapigiwa kura
kwa pamoja.
(2) Endapo mgombea wa nafasi ya madaraka ya Rais atachaguliwa
basi na Makamu wa Rais atakuwa amechaguliwa.
(3) Mtu atateuliwa kugombea nafasi ya madaraka ya Makamu wa
Rais kwa kufuata kanuni kwamba endapo mgombea nafasi ya madaraka ya
Rais wa Jamhuri ya Muungano atatoka sehemu moja ya Washirika wa
Muungano, basi Makamu wa Rais atakuwa ni mtu anayetoka sehemu ya pili
ya Washirika Muungano.
Sifa za
Makamu
wa Rais
88.-(1) Mtu hatateuliwa kugombea au kushika nafasi ya madaraka ya
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano isipokuwa tu kama anazo sifa
za kuchaguliwa kama Rais.
(2) Chama chochote au mtu yoyote anayekusudia kugombea kiti cha
Urais kama mgombea huru hatazuiwa kumpendekeza mtu yeyote kuwa
mgombea nafasi ya madaraka ya Makamu wa Rais kwa sababu tu kwamba
mtu huyo kwa wakati huo ameshika kiti cha Rais wa Zanzibar au Rais wa
Tanzania Bara.
(3) Makamu wa Rais hatakuwa na wadhifa mwingine wowote wa
kiserikali uliotajwa katika Katiba hii au sheria iliyotungwa na Bunge.
(4) Endapo mtu ambaye ni Rais wa Tanzania Bara au Rais wa
Zanzibar anateuliwa au kuchaguliwa kuwa Makamu wa Rais ataacha kiti cha
Rais wa Tanzania Bara au cha Rais wa Zanzibar, kadri itakavyokuwa.
Kiapo cha
Makamu
wa
Rais
89. Makamu wa Rais, kabla ya kushika madaraka yake ataapishwa
na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, kiapo cha uaminifu na pia kiapo
kingine chochote kinachohusika na utendaji wa kazi yake kitakachowekwa
kwa mujibu wa Sheria iliyotungwa na Bunge.
‐ 37 ‐
Wakati
wa
Makamu
wa
Rais
kushika
madaraka
90.-(1) Makamu wa Rais atashika nafasi yamadaraka ya Makamu wa
Rais siku hiyo hiyo Rais anaposhika madaraka.
(2) Makamu wa Rais aliyeteuliwa kwa mujibu wa Ibara ya 72 ataapa
na kushika madaraka yake baada ya uteuzi wake kuthibitishwa na Bunge.
(3) Isipokuwa kama atajiuzulu au atafariki mapema zaidi, mtu
aliyechaguliwa, au kuteuliwa kwa mujibu wa Ibara ya 72 kuwa Makamu wa
Rais, bila ya kuathiri masharti mengine ya Ibara hii, atashika kiti cha
Makamu wa Rais kwa muda wa miaka mitano tangu alipochaguliwa kuwa
Makamu wa Rais.
(4) Makamu wa Rais atashika kiti hicho hadi-
(a) muda wake utakapokwisha;
(b) akifariki dunia akiwa katika madaraka;
(c) atakapojiuzulu;
(d) atakapoapishwa kuwa Rais baada ya nafasi ya madaraka ya Rais
kuwa wazi;
(e) atakapotiwa hatiani kwa kosa lolote la jinai linaloonyesha utovu
wake wa uaminifu;
(f) atakapoapishwa Rais mwingine kushika nafasi ya madaraka ya
Rais pamoja na Makamu wake;
(g) atakapoondolewa madarakani baada ya kushtakiwa Bungeni kwa
mujibu wa masharti ya Katiba hii;
(h) atakapoacha kushika nafasi ya madaraka ya Makamu wa Rais
vinginevyo kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.
Bunge
kumuondoa
Makamu
wa Rais
91.-(1) Bunge litakuwa na madaraka ya kumshtaki Makamu wa Rais
kwa utaratibu unaotumika kumshtaki Rais kwa mujibu wa Katiba hii,
isipokuwa kwamba, hoja yoyote ya kumshtaki Makamu wa Rais itatolewa tu
iwapo:
(a) Rais amewasilisha hati kwa Spika inayoeleza kwamba Makamu
wa Rais ameacha au ameshindwa kutekeleza kazi za madaraka
ya Makamu wa Rais;
(b) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha nafasi ya madaraka ya
Rais wa Jamhuri ya Muungano au kiti cha Makamu wa Rais; au
(c) anadaiwa kutenda kosa lolote kati ya makosa yanayoweza
kusababisha Rais kushtakiwa na Bunge kwa mujibu wa Katiba
hii,
isipokuwa kwamba, haitatolewa hoja ya namna hiyo ndani ya miezi kumi na
miwili tangu hoja hiyo ilipotolewa na ikakataliwa na Bunge.
(2) Masharti mengine kuhusu utaratibu wa kumshtaki Rais
yatatumika wakati wa kumuondoa madarakani Makamu wa Rais.
(3) Ikitokea kwamba kiti cha Makamu wa Rais ki wazi kutokana na
masharti yaliyomo katika Ibara ndogo ya (1), kifo au kujiuzulu basi mapema
iwezekanavyo na kwa vyovyote ndani ya siku zisizozidi kumi na nne baada
ya kushika madaraka yake, Rais atamteua mtu atakayekuwa Makamu wa
Rais na uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura za Wabunge walio
wengi.
‐ 38 ‐
(4) Masharti mengine yote ya Ibara ya 84 yatatumika pia kuhusiana
na Makamu wa Rais isipokuwa tu kwamba Makamu wa Rais aliyeondolewa
tena madarakani chini ya Ibara ndogo ya (3), hatakuwa na sifa tena za
kushika nafasi ya Rais, Makamu wa Rais, Rais wa Tanzania Bara wala Rais
wa Zanzibar.
(5) Endapo Makamu wa Rais ataacha kushika nafasi ya madaraka
ya Makamu waRais kutokana na mashtaka dhidi yake kuthibitika,
hatakuwa na haki ya kupata malipo yoyote ya uzeeni, posho wala kupata
haki au nafuu nyinginezo anazopewa Makamu wa Rais au mtu aliyekuwa
Makamu wa Rais kwa mujibu wa Katiba au sheria za nchi.
SEHEMU YA PILI
BARAZA LA MAWAZIRI LA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO
(a) Baraza la Mawaziri
Kuundwa
kwa
Baraza la
Mawaziri
92.-(1) Kutakuwa na Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano
litakalokuwa na wajumbe wafuatao:
(a) Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano; na
(b) Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
(2) Mwanasheria Mkuu wa Serikali atahudhuria vikao vya Baraza la
Mawaziri lakini hatakuwa na haki ya kupiga kura.
(3) Baraza la Mawaziri ndicho chombo kikuu cha kumshauri Rais
kuhusu mambo yanayohusu utekelezaji wa madaraka na matumizi ya
mamlaka ya Rais.
(4) Bunge naMahakama hazitakuwa na uwezo wa kisheria
kuchunguza kama ushauri wowote au ushauri wa aina gani ulitolewa na
Baraza la Mawaziri kwa Rais.
Uteuzi wa
Mawaziri
na Naibu
Mawaziri
93.-(1) Kutakuwa na Mawaziri na Naibu Mawaziri wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano watakaoteuliwa na Rais kwa kushauriana na Makamu
wa Rais na baadaye kuthibitishwa na Bunge.
(2) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (1), idadi ya Mawaziri wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano haitozidi kumi na tano.
(3) Serikali ya Jamhuri ya Muungano itakuwa na Wizara kwa
kuzingatia mamlaka ya Serikali kwa mujibu wa Katiba hii.
(4) Uteuzi wa Mawaziri na Naibu Waziri wa Serikali ya Jamhuri ya
Muungano utazingatia uwakilishi na uwiano wa Washirika wa Muungano.
(5) Majukumu ya Waziri na Naibu Waziri yatakuwa kama
yatakavyoainishwa na Rais kwenye Hati ya Uteuzi.
Sifa za
Mawaziri
na Naibu
Mawaziri
94.-(1) Mtu atateuliwa kuwa Waziri au Naibu Waziri wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano ikiwa:
(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa
Sheria za nchi;na
(b) angalau ana shahada ya kwanza ya Chuo Kikuu
kinachotambulika kwa mujibu wa Sheria za nchi.
‐ 39 ‐
(2) Watu wafuatao hawatakuwa na sifa ya kuteuliwa kuwa
Mawaziri au Naibu Mawaziri katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano:
(a) Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Wabunge wa
Bunge la Tanzania Bara, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi la
Zanzibar au madiwani kutoka Washirika waMuungano;
(b) mtu aliyewahi kutiwa hatiani kwa makosa ya ubadhirifu wa
mali za umma, ama katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano,
Serikali ya Tanzania Bara au Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar.
Kiapo,
muda na
masharti
ya kazi ya
Waziri na
Naibu
Waziri
95.-(1) Waziri au Naibu Waziri hatashika nafasi ya madaraka mpaka
awe ameapa mbele ya Rais kiapo cha uaminifu na pia kiapo kingine
chochote kinachohusika na utendaji wa kazi yake kitakachowekwa na
sheria za nchi.
(2) Muda wa kushika nafasi ya madaraka ya Waziri au Naibu Waziri
utaanza tarehe ambayo Waziri au Naibu Waziri anayehusika ataapishwa.
(3) Kila Waziri anawajibika binafsi na kwa pamoja kwa Rais
katika utekelezaji wa majukumu na katika kutumia nafasi ya madaraka ya
Waziri.
(4) Waziri au Naibu Waziri atashika nafasi ya madaraka kwamuda
wote isipokuwa kama:
(a) atajiuzulu au kufariki;
(b) Rais atatengua uteuzi au kumwachisha kazi; au
(c) saa ishirini na nne zimetimia kabla ya Rais mteule kushika
madaraka ya Rais.
Utekelezaji
wa
shughuli
za
Serikali
Bungeni
96.-(1) Mawaziri na Naibu Mawaziri hawatakuwa na haki ya
kuhudhuria vikao vya Bunge isipokuwa tu:
(a) endapo kutakuwa na hoja mahsusi ambayo Bunge linahitaji
ufafanuzi kwa Waziri husika; au
(b) endapo Serikali au Waziri ataomba na kuruhusiwa kuwasilisha
au kuitolea ufafanuzi hoja yoyote Bungeni.
(2) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (2), Waziri
atakayeruhusiwa kuhudhuria kikao cha Bunge anaweza kulihutubia Bunge.
(3) Serikali ya Jamhuri ya Muungano, chini ya mamlaka ya Rais,
ndiyo itakuwa na uwezo wa kufanya maamuzi juu ya sera za Serikali kwa
jumla, na Mawaziri, watawajibika kwa pamoja Bungeni kuhusu utekelezaji
wa sera nashughuli za Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
(4) Kila Waziri atahudhuria vikao vya Kamati za Bunge kila
atakapohitajika na kutoa maelezo au ufafanuzi wa suala lolote linalohusu
utendaji katika nafasi ya madaraka yake.
(5) Kwa kuzingatia masharti mengine ya jumla ya Katiba hii,
Mawaziri watatoa maelezo au taarifa ambazo zinahitajika kutolewa
Bungeni kwa mujibu wa sheria za nchi.
‐ 40 ‐
(b) Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Mwanasheria
Mkuu wa
Serikali
97.-(1) Kutakuwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye katika Katiba hii atatajwa tu
kwa kifupi kama "Mwanasheria Mkuu" ambaye atateuliwa na Rais na
kuthibitishwa na Bunge.
(2) Mtu anayestahili kuwa Mwanasheria Mkuu sharti awe na sifa
zifuatazo:
(a) awe ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano;
(b) awe na shahada ya Sheria ya Chuo Kikuu
kinachotambuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi;
(c) awe ni mweledi na mwenye sifa ya kuteuliwa kuwa
wakili wa Mahakama;
(d) awe ni mtumishi mwandamizi katika utumishi wa umma
au taasisi zake;
(e) awe ni mtu ambaye amedumu na sifa hizo kwa muda
usiopungua miaka kumi na tano; na
(f) ana tabia njema na mwenendo usiotiliwa shaka na jamii.
(3) Mwanasheria Mkuu atakuwa ndiye mshauri mkuu wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano kuhusu mambo ya sheria na, kwa ajili hiyo,
atawajibika kutoa ushauri kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano kuhusu
mambo yote ya kisheria, na kutekeleza shughuli nyinginezo zozote
zenye asili au kuhusiana na sheria zitakazopelekwa kwake au
atakazoagizwa na Rais kuzitekeleza.
(4) Mwanasheria Mkuu atatekeleza kazi au shughuli nyingine
zilizokabidhiwa kwake na Katiba hii au sheria za nchi.
(5) Katika kutekeleza kazi zake, Mwanasheria Mkuu atakuwa na
haki ya kuhudhuria na kusikilizwa na Mahakama katika Jamhuri ya
Muungano na Mahakama Kuu za Washirika wa Muungano.
(c) Katibu Mkuu Kiongozi na Makatibu Wakuu
Katibu
Mkuu
Kiongozi
98.-(1) Kutakuwa na Katibu Mkuu Kiongozi atakayeteuliwa na
Rais kutoka miongoni mwa watumishi waandamizi na kuthibitishwa na
Bunge.
(2) Katibu Mkuu Kiongozi atakuwa Katibu wa Baraza la Mawaziri,
Mwenyekiti wa Vikao vya Kamati Maalum ya Makatibu Wakuu na Mkuu
wa Utumishi wa Umma.
(3) Akiwa Mkuu wa Utumishi wa Umma, Katibu Mkuu Kiongozi
atakuwa na mamlaka ya kutoa maelekezo ya mara kwa mara kuhusiana na
masuala ya utumishi wa umma.
(4) Katika wadhifa wake wa Katibu wa Baraza la Mawaziri, Katibu
Mkuu Kiongozi atakuwa Mtendaji Mkuu katika Ofisi ya Baraza la
Mawaziri, na atatekeleza shughuli zifuatazo kwa kufuata maagizo ya jumla
au maalum atakayopewa na Rais, yaani:
(a) kuandaa ratiba ya mikutano na kutayarisha orodha ya shughuli
za Baraza la Mawaziri;
(b) kuandika na kuweka kumbukumbu za mikutano;
‐ 41 ‐
(c) kutoa taarifa na maelezo ya uamuzi wa Baraza la Mawaziri
kwa kila mtu au chombo cha umma kinachohusika na
uamuzi uliotolewa; na
(d) kutekeleza kazi na shughuli nyingine zozote ambazo Rais
ameagiza.
Makatibu
Wakuu
99.-(1) Kutakuwa na Makatibu Wakuu watakaoteuliwa na Rais
kutoka miongoni mwa Watumishi Waandamizi katika utumishi wa umma
kama watakavyopendekezwa na Tume ya Utumishi wa Umma.
(2) Kila Katibu Mkuu atakuwa kiongozi na Mtendaji Mkuu wa
Wizara ya Serikali aliyopangiwa na Rais na atashika nafasi ya madaraka
ya Katibu Mkuu na kutekeleza majukumu yake kama itakavyoainishwa
katika sheria za nchi.
(3) Rais anaweza, kwa mapendekezo ya Tume ya Utumishi wa
Umma, kumteua mtumishi mwandamizi katika Utumishi wa Umma
kuwa Naibu Katibu Mkuu.
(4) Kila Katibu Mkuu atakuwa mshauri wa mwisho kwa Waziri
kwa masuala yote ya utendaji na atatoa ushauri kwa Baraza la
Mawaziri katika vikao na Kamati zitakazoitishwa na Katibu wa Baraza
la Mawaziri.
(5) Katibu Mkuu Kiongozi, Katibu Mkuu na Naibu Katibu
Mkuu hatashika madaraka yake mpaka kwanza aape mbele ya Rais
kiapo cha utii na uaminifu au kiapo kingine chochote kinachohusu
utendaji wa kazi zake.
(d) Utendaji Kazi wa Baraza la Mawaziri
Kamati
Maalumu
ya
Makatibu
Wakuu
100. Kutakuwa na Kamati Maalum ya Makatibu Wakuu
itakayoongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi ambayo itakuwa na
majukumu ya kuchambua na kulishauri Baraza la Mawaziri juu ya
masuala mbalimbali kabla ya kuwasilishwa na kufanyiwa uamuzi na
Baraza hilo na itatekeleza majukumu mengine kama itakavyopangiwa
na Baraza la Mawaziri.
Sekretarieti
ya
Baraza la
Mawaziri
101.-(1) Kutakuwa na Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri
ambayo itakuwa na jukumu la kuhudumia Baraza la Mawaziri, Kamati
Maalum ya Makatibu Wakuu na kutekeleza majukumu mengine kama
itakavyopangiwa na Baraza la Mawaziri.
(2) Bunge linaweza kutunga sheria kuhusu utaratibu na
utekelezaji wa shughuli za Serikali.
SURA YA NANE
URATIBU WA MAHUSIANO YA WASHIRIKA WA MUUNGANO
Tume ya
Mahusiano
ya
Uratibu
wa
Serikali
102.(1)Kutakuwa na Tume ya kusimamia na kuratibu
mahusiano baina ya Serikali ya Muungano na Serikali za Washirika wa
Muungano na kusimamia na kuratibu mahusiano baina ya Serikali za
Washirika wa Muungano, ambayo itajulikana kwa kifupi kama “Tume
ya Mahusiano na Uratibu wa Serikali”.
‐ 42 ‐
(2) Tume ya Mahusiano na Uratibu wa Serikali itaundwa na
wajumbe wafuatao:
(a) Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ambaye
atakuwa Mwenyekiti;
(b) Rais wa Tanzania Bara;
(c) Rais wa Zanzibar;
(d) Mawaziri Wakaazi;
(e) Waziri mwenye dhamana ya mambo ya nje wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano.
Malengo
ya Tume
103. Tume ya Mahusiano na Uratibu wa Serikali itakuwa na
malengo yafuatayo:
(a) kuweka utaratibu borana endelevu wa mashauriano na
mashirikiano baina ya Serikali ya Muungano na Serikali za
Washirika wa Muungano;
(b) kukuza na kuwezesha uratibu na mashirikiano miongoni
mwa Washirika wa Muungano kuhusu masuala yasiyo ya
Muungano kwa lengo la kuwezesha kufanana kwa kiwango
cha utoaji huduma kwa wananchi wote;
(c) kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya Serikali ya
Muungano na Serikali za Washirika wa Muungano kujadili
juu ya utekelezaji wa mambo ya Muungano na yasiyo ya
Muungano kwa manufaa na ustawi wa wananchi wote; na
(d) kuweka mazingira mazuri ya utatuzi wa migogoro baina ya
Serikali ya Muungano na Washirika wa Muungano.
Majukum
u ya
Tume
104.-(1) Tume ya Mahusiano na Uratibu ya Serikali itakuwa na
jukumu maalumu la kuwezesha uratibu na ushirikiano katika
kutekeleza masharti ya Katiba hii, sera, sheria, mipango na mikakati
baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali za Washirika
wa Muungano na baina ya Serikali za Washirika na pia itakuwa
chombo maalumu kwa ajili ya:
(a) mashauriano na mashirikiano baina ya:
(i) Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali za
Washirika wa Muungano; na
(ii) Serikali za Washirika wa Muungano zenyewe
katikamasuala yasiyo ya Muungano;
(b) kusimamia, kuratibu na kuhakikisha kwamba kuna kuwiana
kwa sera na sheria za Washirika wa Muungano katika masuala
yasiyo ya Muungano;
(c) mashauriano na ushirikiano baina ya Jamhuri ya Muungano na
taasisi za kimataifa kwa niaba ya nchi;
(d) usimamizi na ukuzaji wa masuala yenye maslahi kwa Taifa;
(e) usuluhishi na utatuzi wa migogoro baina ya:
(i) Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali za
Washirika wa Muungano; na
(ii) Serikali za Washirika wa Muungano katika masuala
yasiyo ya Muungano;
(2) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (1)(e), endapo upande
‐ 43 ‐
wowote katika mgogoro hautaridhika na uamuzi wa Tume ya
Mahusiano na Uratibu wa Serikali, unaweza kukata rufani katika
Mahakama ya Juu na uamuzi wa Mahakama hio utakuwa ni wa
mwisho.
(3) Bunge linaweza kutunga sheria kwa ajili ya:
(a) kusimamia mahusiano na uratibu baina ya Serikali za
Washirika wa Muungano na kati yaSerikali ya Jamhuri ya
Muungano na Serikali za Washirika wa Muungano; na
(b) kuweka utaratibu wa utatuzi wa migogoro kwa mujibu wa
Ibara hii.
SURA YA TISA
BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO
SEHEMU YA KWANZA
KUUNDWA KWA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO
Bunge la
Jamhuri ya
Muungano
105.-(1) Kutakuwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano.
(2) Wajumbe wa Bunge watakuwa wa aina zifuatazo:
(a) Wabunge waliochaguliwa kuwakilisha majimbo ya
uchaguzi;
(b) Wabunge watano watakaoteuliwa na Rais kutoka miongoni
mwa watu wenye sifa za kuchaguliwa kuwa wabunge
kuwakilisha watu wenye ulemavu kwa kuzingatia uwiano wa
Washirika wa Muungano.
(3) Kwa madhumuni ya Ibara ya ndogo (2)(a), kila mkoa kwa
upande wa Tanzania Bara na wilaya kwa upande wa Zanzibar, itakuwa ni
jimbo la uchaguzi.
(4) Katika kila Jimbo la Uchaguzi kutakuwa na nafasi mbili za
ubunge, moja kwa ajili ya mwanamke na moja kwa ajili ya mwanamme.
(5) Wabunge wote katika kila Jimbo la Uchaguzi watapatikana kwa
kupigiwa kura na wananchi kwa mujibu wa masharti ya Katiba hiina sheria
inayoweka utaratibu kuhusu mambo ya uchaguzi.
Muda wa
Bunge
106.-(1) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya Katiba hii, maisha
ya kila Bunge yatakuwa ni muda wa miaka mitano.
(2) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (1), maneno "maisha ya
Bunge" maana yake ni muda wote unaoanzia tarehe ambapo Bunge Jipya
litaitishwa kukutana kwa mara ya kwanza baada ya uchaguzi wa wabunge
na kuishia tarehe ya kuvunjwa kwa Bunge kwa ajili ya kuwezesha
uchaguzi mwingine kufanyika.
Madaraka
ya Bunge
107.-(1) Bunge ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano
chenye madaraka, kwa niaba ya wananchi, kuisimamia Serikali ya Jamhuri
ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu
yake kwa mujibu wa Katiba hii.
(2)Katika kutekeleza majukumu yake, Bunge litakuwa na madaraka
yafuatayo:
(a) kujadili na kutoa ushauri katika mambo yote yenye maslahi
‐ 44 ‐
kwa taifa na umma wa Watanzania;
(b) kumuuliza Waziri yeyote suala lolote kuhusu mambo ya umma
katika Jamhuri ya Muungano ambayo yako katika wajibu wake;
(c) kujadili mgawanyo na kuidhinisha matumizi ya fedha kwa
Wizara, taasisi na mashirika ya Serikali;
(d) kujadili utekelezaji wa kila Wizara wakati wa Mkutano wa
Bunge wa kila mwaka wa bajeti;
(e) kujadili na kuidhinisha mpango wowote wa muda
mrefu au wa muda mfupi unaokusudiwa kutekelezwa na
Serikali katika Jamhuri ya Muungano;
(f) kutunga sheria ya kusimamia utekelezaji wa mpango
wowote wa muda mrefu au muda mfupi;
(g) kujadili na kuridhia mikataba ya kimataifa inayohusu
Jamhuriya Muungano na ambayo kwa masharti yake
inahitajikuridhiwa; na
(h) kujadili na kuridhia mikataba yote inayohusisha rasilimali na
maliasili zinazosimamiwa na Serikali ya Jamhuri ya
Muungano.
(3) Bunge litaisimamia Serikali kwa kuangalia mwenendo wa
utendaji wa Rais, Makamu wa Rais, Mawaziri na watendaji wakuu katika
utumishi wa umma.
Mipaka
ya Bunge
katika
kutumia
madaraka
yake
108.-(1) Katika kutekeleza madaraka ya kuisimamia Serikali kwa
mujibu wa Katiba hii, wajibu wa Bunge itakuwa nikuishauri Serikali na
endapo Bunge halitaridhishwa na hatua zilizochukuliwa na Serikali katika
utekelezaji wa suala lililotolewa ushauri, basi Bunge litakuwa na haki ya
kuiwajibisha Serikali kwa mujibu wa madaraka iliyopewa katika Katiba
hii.
(2) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (1), Bunge halitachukua
hatua yoyote ya kiutendaji ambayo, kwa desturi ni shughuli za Serikali, na
halitatoa maagizo yoyote ya kiutendaji kwa Serikali na Watumishi wa
Umma, isipokuwa Bunge litashauri kuhusu suala lolote lililo katika
dhamana ya Waziri anayehusika.
Madaraka
ya
Bunge
kutunga
sheria
109.-(1) Mamlaka ya kutunga sheria juu ya mambo yote
yanayohusu Jamhuri ya Muungano yatakuwa chini yaBunge.
(2) Mamlaka ya kutunga sheria katika Tanzania Bara na
Zanzibar juu ya mambo yote yasiyo ya Muungano yatakuwa chini ya
Bunge la Tanzania Bara na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar.
(3) Endapo sheria iliyotungwa na Bunge inahusu jambo lolote
ambalo liko chini ya mamlaka ya Bunge la Tanzania Bara au Baraza la
Wawakilishi la Zanzibar, sheria hiyo itakuwa batili na itatenguka.
(4) Endapo sheria iliyotungwa na Bunge la Tanzania Bara au
Baraza la Wawakilishi la Zanzibar inahusu jambo lolote ambalo liko
chini ya mamlaka ya Bunge la Jamhuri ya Muungano, sheria hiyo
itakuwa batili na itatenguka.
(5)Bila ya kuathiri kutumika kwa Katiba ya Tanzania Bara na
‐ 45 ‐
Katiba ya Zanzibar, Katiba hii itakuwa na nguvu ya sheria katika
Jamhuri ya Muungano kwa mambo yanayohusu Muungano na endapo
sheria nyingine yoyote itakiuka masharti yaliyomo katika Katiba hii, basi
sheria hiyo nyingine, kwa kiasi kinachokiuka Katiba hii, itakuwa batili.
Utaratibu
wa
kutunga
sheria
110.-(1) Bunge litatumia madaraka yake ya kutunga sheria kwa
kujadili na kupitisha Muswada wa Sheria ambao utawekwa saini na Rais.
(2) Bila kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (3), Muswada wa
Sheria unaweza kuandikwa na Serikali, Kamati ya Bunge au kikundi cha
Wabunge.
(3) Wakati wa kuandaa muswada wa sheria kuhusu jambo lolote la
Muungano, Serikali ya Jamhuri ya Muungano itahakikisha kwamba
inawashirikisha wananchi kwa ajili ya kupata maoni na mapendekezo juu
ya muswada huo.
(4) Bunge litatunga Kanuni za Kudumu zitakazoweka utaratibu
wa:
(a) kuwasilisha, kujadili na kupitisha Muswada wa Sheria; na
(b) utekelezaji bora wa masharti ya Ibara ndogo ya (3).
Utaratibu
wa
Kubadilisha
Katiba hii
na
baadhi ya
sheria
111.-(1) Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 110,Bunge linaweza
kutunga Sheria kwa ajili ya kubadilisha masharti yoyote ya Katiba hii kwa
kufuata Kanuni kwamba, Muswada wa Sheria kwa ajili ya kubadilisha
masharti yoyote ya Katiba hii utaungwa mkono kwa kura zisizopungua
theluthi mbiliya kura za Wabunge wote kutoka kila upande wa Muungano.
(2) Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya Ibara ndogo ya
(1) kubadilisha masharti ya Katiba hii au masharti ya sheria,maana yake ni
pamoja na kurekebisha au kusahihisha masharti haya au kufuta na kuweka
masharti mengine badala yake au kusisitiza au kubadilisha matumizi ya
masharti hayo.
Utaratibu
wa
kubadilisha
masharti
mahusus
112. Bunge halitaweza kufanya mabadiliko ya Katiba kwa lengo la:
(a) kuongeza au kupunguza jambo lolote la Muungano; na
(b) uwepo wa Jamhuri ya Muungano,
mpaka kwanza mabadiliko hayo yaungwe mkono na wananchi wa
Washirika wa Muungano kwa Kura ya Maoni itakayoendeshwa na
kusimamiwa na Tume Huru ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kwa mujibu wa sheria itakayotungwa na Bunge.
Utaratibu
wa
kutunga
sheria
kuhusu
mambo
ya fedha
113.-(1) Bunge halitashughulikia jambo lolote kati ya mambo
yanayohusika na Ibara hii isipokuwa kama Rais amependekeza kwamba
jambo hilo lishughulikiwe na Bunge na pendekezo hilo la Rais liwe
limewasilishwa kwenye Bunge na Waziri.
(2) Mambo yanayohusika na Ibara hii ni yafuatayo:
(a) Muswada wa Sheria kwa ajili ya jambo lolote kati ya mambo
yafuatayo:
‐ 46 ‐
(i) kutoza kodi au kubadilisha kodi kwa namna
nyingine yoyote isipokuwa kupunguza;
(ii) kuagiza kwamba malipo au matumizi ya fedha
yafanywe kutokana na Mfuko Mkuu wa Hazina ya
Serikali au mfuko mwingine wowote wa Serikali au
kubadilisha kiwango hicho na namna nyingine
yoyote isipokuwa kupunguza;
(b) kuagiza kwamba malipo au matumizi ya fedha yafanywe
kutokana na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali au mfuko
mwingine wowote wa Serikali wakati ikifahamika kwamba
fedha iliyomo katika mifuko hiyo haikupangiwa itolewe kwa
ajili ya malipo au matumizi hayo, au kuagiza kwamba malipo
au matumizi yanayofanywa kutokana na mifuko hiyo
yaongezwe;
(c) kufuta au kusamehe deni lolote linalotakiwa lilipwe kwa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano; au
(d) hoja au mabadiliko yoyote ya hoja kwa ajili ya lolote kati ya
mambo yaliyoelezwa katika aya ya (a) ya Ibara hii ndogo.
Madaraka
ya Mkuu
wa Nchi
kuhusu
Muswada
wa Sheria
114.-(1) Muswadawa Sheria uliopitishwa na Bunge sharti kupata
saini ya Rais, ili kuthibitisha kukubaliwa kwake na Rais.
(2) Muswada wa Sheria uliyowasilishwa kwa Rais kwa ajili ya
kupata kibali utawekewa saini na Rais ndani ya siku zisizozidi thelathini
kutoka siku ambayo Muswada huo uliwasilishwa na kupokelewa na
Katibu wa Baraza la Mawaziri.
(3) Baada ya Muswada wa Sheria kuwasilishwa kwa Rais kwa
ajili ya kupata kibali chake, Rais anaweza kuukubali au kukataa kukubali
Muswada huo, na iwapo Rais atakataa kukubali Muswada huo basi
ataurudisha Bungeni pamoja na maelezo ya sababu za kukataa kukubali
Muswada huo.
(4) Baada ya Muswada wa Sheria kurudishwa Bungeni na Rais
kwa mujibu wa masharti ya Ibara hii, hauwezi kupelekwa tena kwa Rais
kwa ajili ya kupata kibali chake kabla kumalizika muda wa siku sitini tangu
uliporudishwa;
(5) Endapo katika kujadiliwa tena Bungeni kabla haujapelekwa
tena kwa Rais, Muswada uliorudishwa Bungeni na Rais umeungwa mkono
na Wabunge ambao idadi yao haipungui theluthi mbiliya Wabunge wote
basi, Muswada huo unaweza kuwasilishwa mapema zaidi kwa Rais.
(6) Iwapo Muswada uliorudishwa Bungeni na Rais na katika
kujadili ukaungwa mkono na Wabunge ambao idadi yao haipungui theluthi
mbiliya Wabunge wote na kupelekwa tena kwa Rais kwa ajili ya kupata
kibali chake, basi Rais atatakiwa kuweka saini kukubali Muswada wa
sheria husika kabla ya kumalizika muda wa siku sitini na endapo siku
sitini zitapita tangu Muswada huo ulipowasilishwa tena kwa Rais pasipo
Rais kuweka saini, itahesabika kwamba Muswada huo umepata kibali cha
Rais na utakuwa sheria ya nchi.
Kupitishwa
kwa hoja
za Serikali
115.-(1) Endapo Bunge halitaridhishwa na mchanganuo au
mgawanyo wa hoja ya Bajeti iliyowasilishwa na serikali, Bunge linaweza
‐ 47 ‐
kurudisha hoja kuhusu Bajeti ya Serikali pamoja na mapendekezomahsusi
kuhusiana na upungufuuliobainika.
(2) Serikali itawajibika kuyafanyia kazi mapendekezo ya Bunge kwa
kadri itakavyowezekana na kisha kuwasilisha tena Bungeni hoja husika
pamoja na maelezo ya utekelezaji wa maelekezo ya Bunge na endapo Bunge
litakataa kwa mara ya pili hoja kuhusu Bajeti ya Serikali, basi hoja hiyo
itahesabika kuwa imepitishwa na Bunge.
SEHEMU YA PILI
WABUNGE
(a) Uchaguzi wa Wabunge
Uchaguzi
wa
Wabunge
116.-(1) Kila baada ya Bunge kumaliza muda wake wa kipindi cha
miaka mitano, kutakuwa na uchaguzi wa Wabunge katika Majimbo ya
uchaguzi kama itakavyotangazwa na Tume Huru ya Uchaguzi
utakaofanyika kwa mujibu wa sheria itakayotungwa na Bunge.
(2) Kutakuwa na uchaguzi wa Mbunge katika jimbo la uchaguzi
ikiwa:
kiti cha Mbunge aliyechaguliwa kuwakilisha jimbo la uchaguzi kwa
utaratibu wa mgombea huru, kitakuwa wazi kwa sababu nyingine yoyote
isiyohusika na Bunge kumaliza muda wake.
(3) Endapo tarehe ya Bunge kumaliza muda wake imetangazwa au
inafahamika, hakutakuwa na uchaguzi mdogo wa mbunge ndani ya kipindi
cha miezi kumi na minane kabla ya tarehe hiyo.
(4) Endapo Mbunge anayetokana na chama cha siasa atapoteza sifa
za kuwa mbunge kwa sababu yoyote isiyokuwa ya Bunge kumaliza muda
wake, Tume Huru ya Uchaguzi ya Jamhuri, kwa mujibu wa masharti
yatakayowekwa na sheria itakayotungwa na Bunge kwa ajili hiyo, itamteua
na kumtangaza kuwa mbunge mtumwingine kutoka kwenye orodha ya
majina ya wagombea iliyowasilishwa na chama hicho kwa mujibu wa Ibara
ndogo ya (5).
(5) Orodha ya majina ya wagombea kutoka kila chama cha siasa
iliyowasilishwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano
katika Uchaguzi Mkuu ndiyo itakayotumiwa na Tume Huru ya Uchaguzi ya
Jamhuri ya Muungano baada ya kushauriana na chama cha siasa
kinachohusika, kwa madhumuni ya kujaza nafasi ya Mbunge inapotokea
kuwa wazi, wakati wowote wa Maisha ya Bunge.
Sifa za
kuchaguliwa
kuwa
Mbunge
117.-(1) Bila ya kuathiri masharti yaliyomo katika Ibara hii, mtu
yeyote atakuwa na sifa za kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge
endapo:
(a) ni raia wa Jamhuri ya Muungano aliyetimiza umri wa miaka
ishirini na tano wakati wa kugombea;
(b) anajua kusoma na kuandika lugha ya Kiswahili au Kiingereza
na ana elimu isiyopungua kidato cha nne;
(c) ni mwanachama aliyependekezwa na chama cha siasa au
mgombea huru;
(d) ni mwadilifu na anayeheshimu haki za binadamu na
asiyedharau wala kubagua watu kwa misingi ya kabila, dini,
‐ 48 ‐
jinsi, maumbile au hali zao katika jamii; na
(e) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya uchaguzi
hakuwahi kutiwa hatiani katika mahakama kwa kosa la
kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.
(2) Mtu hatakuwa na sifa za kugombea kuchaguliwa kuwa
Mbunge-
(a) ikiwa mtu huyo aliwahi kuwa Mbunge kwa vipindi vitatu
vya miaka mitano; au
(b) ikiwa imethibitishwa rasmi kwamba mtu huyo ana ugonjwa
wa akili;
(c) ikiwa mtu huyo amehukumiwa na Mahakama yoyote katika
Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu ya kifo au ya
kufungwa gerezani kwa muda unaozidi miezi sita kwa
kukutwa na hatia ya kosa lolote, vyovyote linavyoitwa,
linaloambatana na kukosa uaminifu; au
(d) ikiwa katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya
uchaguzi amepata kuhukumiwa na kupewa adhabu ya
kifungo kwa kosa linaloambatana na kukosa uaminifu au
kwa kuvunja sheria inayohusiana na Maadili ya Viongozi
wa Umma;
(e) ikiwa mtu huyo ana maslahi yoyote katika mkataba wa
Serikali wa aina yoyote aliyowekewa miiko maalum kwa
mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge, na iwapo amekiuka
miiko hiyo;
(f) ikiwa mtu huyo anashika madaraka ya ofisa mwandamizi
katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano au
Washirika wa Muungano; au
(g) ikiwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge
inayoshughulikia makosa yanayohusika na uchaguzi wa
aina yoyote, mtu huyo amezuiliwa kujiandikisha kama
mpiga kura au kupiga kura katika uchaguzi wa Wabunge.
(3) Bunge linaweza kutunga sheria kwa ajili ya kuweka masharti
yatakayomzuia mtu asichaguliwe kuwa Mbunge wa kuwakilisha Jimbo la
Uchaguzi ikiwa mtu huyo ni mwenye madaraka yanayohusika na shughuli
za kuongoza au kusimamia uchaguzi wa Wabunge au shughuli za
uandikishaji wa wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa Wabunge.
(4) Katika aya ya (e) ya Ibara ndogo ya (2) ya Ibara hii "mkataba
wa Serikali" maana yake ni mapatano yoyote ya mkataba ambayo
mmojawapo wa walioshiriki ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano au
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar au Serikali ya Tanzania Bara, Idara au
Taasisi yoyote ya Serikali yoyote kati ya hizo au mtumishi yeyote wa
Serikali aliyeshiriki katika majadiliano ya mkataba husika kwa niaba ya
Serikali yoyote miongoni mwa hizo.
(5) Watu wenye nyadhifa zifuatazo katika Utumishi wa Umma
hawatakuwa na sifa ya kuwa Wabunge:
(a) Rais na Makamu wa Rais;
(b) Rais wa Tanzania Bara na Rais wa Zanzibar na Makamu
wao;
(c) Spika na Naibu Spika wa Bunge;
‐ 49 ‐
(d) Waziri na Naibu Waziri;
(e) Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Naibu Mwanasheria
Mkuu wa Serikali;
(f) Katibu wa Baraza la Mawaziri na Makatibu Wakuu;
(g) viongozi na watumishi wa vyombo vya ulinzi na usalama;
(h) mtu ambaye ameajiriwa katika vyombo vya dola kama
askari;
(i) Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Serikali;
(j) Jaji Mkuu, Jaji au Hakimu wa Mahakama, Wakili wa
Serikali na Ofisa Sheria Katika Serikali ya Jamhuri ya
Muungano au Serikali za Washirika;
(k) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali;
(l) Mjumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi; na
(m) mtu yeyote aliyeajiriwa, kuteuliwa au kuchaguliwa katika
utumishi wa umma.
(6) Kwa madhumuni ya kutoa fursa ya kukata rufani kwa mtu
yeyote:
(a) aliyethibitishwa rasmi kisheria kuwa ana ugonjwa wa akili;
(b) aliyehukumiwa na kupewa adhabu ya kifo au kufungwa
gerezani au chuo cha mafunzo; au
(c) aliyepatikana na hatia ya kosa lolote lililotajwa katika sheria
kwa mujibu wa Ibara ndogo ya (2),
mamlaka ya nchi itaweka utaratibu wa sheria kwa ajili ya kuweka masharti
kwamba hukumu inayopingwa haitakuwa na nguvu kwa ajili ya utekelezaji
wa masharti ya Ibara ndogo ya (2) hadi upite muda uliotajwa katika sheria
hiyo.
Watu
wenye
madaraka
Serikalini
kukoma
utumishi
118. Iwapo mtu mwenye madaraka katika utumishi wa umma ya
aina iliyotajwa katika sheria itakayotungwa na Bungeataamua-
(a) kugombea nafasi ya kisiasa ya aina yoyote chini ya Katiba hii; au
(b) kugombea uongozi wa ngazi yoyote katika chama cha siasa,
mtu huyo atahesabiwa kuwa utumishi wake umekoma tangu siku ya
kuteuliwa kuwa mgombea wa nafasi ya kisiasa au kugombea uongozi
katika chama cha siasa.
Utaratibu
wa
uchaguzi
wa
Wabunge
119.-(1) Wabunge wanaowakilisha majimbo ya uchaguzi
watachaguliwa na wananchi kwa kufuata masharti ya Katiba hii na vile vile
masharti ya sheria iliyotungwa na Bunge kwa mujibu wa Katiba hii,
inayoweka masharti kuhusu uchaguzi wa Wabunge.
(2) Wagombea uchaguzi katika majimbo ya Uchaguzi watatakiwa
kuwasilisha majina yao kwa Tume Huru ya Uchaguzi ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na sheria
iliyotungwa na Bunge.
Kiapo cha
Wabunge
120. Kila Mbunge atatakiwa kuapishwa katika Bunge kiapo cha
uaminifu kabla hajaanza kushiriki katika shughuli za Bunge, lakini
Mbunge anaweza kushiriki katika uchaguzi wa Spika hata kabla
hajaapishwa.
‐ 50 ‐
Masharti
ya kazi ya
Wabunge
121. Wabunge watashika madaraka yao kwa mujibu wa Katiba hii,
na watalipwa mshahara, posho na malipo mengine kama yatakavyopangwa
na Tume ya Utumishi wa Umma kwa mujibu wa sheria za nchi.
Muda wa
Wabunge
kushika
madaraka
122.-(1) Mbunge atakoma kuwa Mbunge ikiwa litatokea lolote kati
ya mambo yafuatayo:
(a) tukio lolote ambalo, kama asingekuwa Mbunge lingemfanya
asiwe au apoteze sifa za kuchaguliwa au kuteuliwa kwa mujibu
wa masharti ya Katiba hii;
(b) atakosa kuhudhuria vikao vya Mikutano ya Bunge mitatu
mfululizo bila ya ruhusa ya Spika;
(c) itathibitishwa kwamba amevunja masharti ya Sheria ya
Maadili ya Viongozi wa Umma;
(d) atashindwa kufanya kazi za Mbunge kwa muda wa miezi sita
mfululizo kutokana na ugonjwa wa akili au afya ya mwili au
kizuizi ndani ya gereza;
(e) ikiwa atashindwa kutoa tamko rasmi kuhusu sifa za kuwa
Mbunge au taarifa rasmi kuhusu mali kwa mujibu wa
masharti ya Katiba hii katika muda uliowekwa mahsusi na
sheria za nchi;
(f) ikiwa atajiuzulu ubunge; au
(g) ikiwa ataondolewa madarakani kwa mujibu wa masharti ya
Katiba hii.
(2) Mbunge anaweza kukata rufani, kwa mujibu wa sheria za nchi
kupinga hukumu ya kuthibitishwa kwake kuwa ni mtu mwenye ugonjwa
wa akili au kupinga adhabu ya kufungwa gerezani, au kupinga kupatikana
kwake na hatia kwa kosa la aina iliyotajwa katika Ibara ndogo ya (1).
Uwajibikaji
wa
Wabunge
123.-(1) Mbunge atashika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba
hii, na wakati wote atawajibika moja kwa moja kwa wapiga kura wake na
chama chake cha siasa ikiwa mbunge huyo ametokana na chama cha siasa.
(2) Mbunge aliyependekezwa na chama cha siasa, hatapoteza
Ubunge wake ikiwa Mbunge huyo atafukuzwa au kuvuliwa uanachama wa
chama chake.
(3) Endapo mbunge, kwa ridhaa yake atajiondoa au kujivua
uanachama kutoka chama chake cha siasa, Mbunge huyo atapoteza sifa za
kuwa Mbunge na atasita kuwa Mbunge.
Haki ya
wapiga
kura
kumwajibisha
Mbunge.
124.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya123 ya Katiba hii,
wananchi watakuwa na haki ya kumuondoa Mbunge wao madarakani,
endapo Mbunge atafanya mojawapo au zaidi ya mambo yafuatayo:
(a) kuunga mkono sera ambazo zinaenda kinyume na maslahi ya
wapiga kura au kinyume na maslahi ya Taifa;
(b) kushindwa kuwasilisha au kutetea kwa dhati hoja zinazotokana na
kero za wapiga kura wake;
(c) kuacha kuishi au kuhamisha makaazi yake kutoka eneo la Jimbo la
‐ 51 ‐
Uchaguzi kwa zaidi ya miezi sita bila sababu za msingi;
(d) kutohudhuria vikao vya Bunge vitatu mfululizo bila ya ruhusa ya
Spika;
(e) kuajiriwa au kufanya kazi nyingine na kuacha kuzingatia kazi yake
ya kuonana na wapiga kura wake;
(f) kufanya biashara, kumiliki makampuni au kuwa na hisa katika
makampuni ambayo yana mikataba au mahusiano ya kibiashara na
taasisi za umma kwa namna ambayo inaleta mgongano wa
kimaslahi;
(g) kutiwa hatiani kwa kosa linalohusiana na rushwa au kosa jingine la
jinai;
(h) kutenda kitendo ambacho ni kinyume na maadili au kukosa
uaminifu; au
(i) mambo mengine yatakayoainishwa kwenye sheria ya Bunge.
(2) Bunge litatunga sheria kuweka masharti ya namna ya kuendesha
uchunguzi kwa Mbunge atakayeshindwa kutekeleza majukumu yake kwa
wapiga kura wake na utaratibu wa kumuondoa mbunge.
Uamuzi
wa
suala
kama
mtu ni
Mbunge
125.-(1) Kila shauri kwa ajili ya kupata uamuzi juu ya suala-
(a) kama uchaguzi wa Mbunge ulikuwa halali au sivyo; au
(b) kama Mbunge amekoma kuwa Mbunge na nafasi ya madaraka
katika Bunge iko wazi au hapana,
litafunguliwa na kusikilizwa kwanza katika Mahakama Kuu.
(2) Bunge laweza kutunga sheria kwa ajili ya kuweka masharti
kuhusu mambo yafuatayo-
(a) watu wanaoweza kufungua shauri katika Mahakama Kuu kwa ajili
ya kupata uamuzi juu ya suala lolote kwa mujibu wa masharti ya
Ibara hii;
(b) sababu na nyakati za kufungua shauri la namna hiyo, utaratibu wa
kufungua shauri na masharti yanayotakiwa yatimizwe kwa kila
shauri kama hilo; na
(c) kutaja mamlaka ya Mahakama Kuu juu ya shauri kama hilo na
kueleza utaratibu wa kusikiliza shauri lenyewe.
Tamko
rasmi la
Wabunge
kuhusu
maadili
ya
Viongozi
126.-(1) Kila Mbunge kabla ya kumalizika siku thelathini tangu
aapishwe kushika nafasi yamadaraka ya Mbunge sharti awasilishe kwa
Tume ya Maadili ya Uongozi na Uwajibikaji nakala mbili za tamko
rasmi kwamba hajapoteza sifa za kuwa mbunge kwa mujibu wa masharti
ya Katiba hii.
(2) Tamko rasmi lililotajwa katika Ibara ndogo ya (1),
litatolewa katika fomu maalum itakayowekwa kwa mujibu wa sheria
za nchi.
Wabunge
kutoa
taarifa ya
mali
127.-(1) Kila Mbunge atawasilisha kwa Katibu wa Bunge nakala
mbili za taarifa rasmi katika fomu maalum maelezo ya mali yake na kadri
itakavyokuwa, mali ya mke au mume wake.
‐ 52 ‐
(2) Katibu wa Bunge atawasilisha kwa Tume ya Maadili ya
Uongozi na Uwajibikaji nakala moja ya kila taarifa rasmi iliyowasilishwa
kwake kwa mujibu wa masharti ya Ibara hii.
SEHEMU YA TATU
UONGOZI WA BUNGE
(a) Spika na Naibu Spika
Spika na
mamlaka
yake
128.-(1) Kutakuwa na Spika wa Bunge ambaye atachaguliwa na
Wabunge na ambaye atakuwa ndiye Kiongozi wa Bunge na atawakilisha
Bunge katika vyombo na vikao vingine vyote nje ya Bunge.
(2) Waziri, Naibu Waziri, Mbunge au mtu mwenye madaraka ya
aina nyingine yoyote yatakayotajwa na Sheria iliyotungwa na Bunge kwa
madhumuni ya Ibara hii, hataweza kuchaguliwa kuwa Spika.
(3) Mtu yeyote atakayechaguliwa kuwa Spika atatakiwa, kabla ya
kumaliza siku thelathini tangu kuchaguliwa kwake, kuwasilisha kwa Tume
ya Maadili ya Viongozi na Uwajibikaji tamko rasmi kwamba hajapoteza
sifa za uchaguzi kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii, tamko hilo
litatolewa katika fomu maalum itakayowekwa kwa mujibu wa sheria
iliyotungwa na Bunge.
(4) Spika atatakiwa kuwasilisha kwa Rais nakala mbili za taarifa
rasmi ya maelezo ya mali yake, kadri itakavyokuwa, mali ya mke au mume
wake.
Ukomo
wa
mamlaka
ya Bunge
129.-(1) Spika atakoma kuwa Spika na ataacha nafasi ya madaraka
ya Spika litokeapo lolote kati ya mambo yafuatayo-
(a) atachaguliwa kuwa Mbunge;
(b) kutatokea jambo lolote ambalo, kama asingekuwa Spika,
lingemfanya mtu huyo asiwe na sifa za uchaguzi au apoteze
sifa za uchaguzi wa Spika;
(c) ataondolewa kwenye madaraka ya Spika kwa Azimio la
Bunge lililoungwa mkono na Wabunge ambao idadi yao
haipungui theluthi mbili ya Wabunge wote; au
(d) atashindwa kuwasilisha kwa Rais tamko rasmi kwa mujibu
wa masharti ya Katiba hii; au
(e) atapatikana na hatia kwa kosa la kutoa habari za uongo, kwa
kiapo kinyume cha sheria kuhusu tamko rasmi lolote
lililotolewa kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii; au
(f) atashindwa kuwasilisha taarifa ya mali kwa mujibu wa
masharti ya Katiba hii kabla ya kumalizika muda uliowekwa
kwa ajili hiyo;au
(g) itathibitika kuwa amevunja masharti ya Sheria inayohusu
Maadili ya Viongozi wa Umma.
(2) Isipokuwa shughuli ya kumchagua Spika, hakuna shughuli
yoyote itakayotekelezwa katika Bunge wakati wowote ambao nafasi ya
madarakaya Spika itakuwa wazi.
‐ 53 ‐
Naibu
Spika
130.-(1) Kutakuwa na Naibu Spika wa Bunge ambaye atachaguliwa
na Wabunge.
(2) Waziri, Naibu Waziri, Mbunge au mtu mwenye madaraka ya
aina nyingine yoyote yatakayotajwa na Sheria iliyotungwa na Bunge kwa
madhumuni ya Ibara hii, hataweza kuchaguliwa kuwa Naibu Spika.
(3) Wabunge watamchagua Naibu Spika nyakati zifuatazo-
(a) Bunge litakapokutana kwa mara ya kwanza baada ya Uchaguzi
Mkuu au mapema iwezekanavyo baada ya wakati huo; na
(b) katika kikao cha kwanza cha Bunge baada ya nafasi ya
madaraka yaNaibu Spika, kuwa wazi kwa sababu yoyote
isiyohusika na Bunge kuvunjwa au mapema iwezekanavyo
baada ya kikao hicho.
(4) Naibu Spika, atakoma kuwa Naibu Spika na ataacha nafasi ya
madaraka ya Naibu Spika litokeapo lolote kati ya mambo yafuatayo-
(a) atachaguliwa kuwa Mbunge;
(b) kutatokea jambo lolote ambalo kama asingekuwa Naibu Spika,
lingemfanya mtu huyo asiwe na sifa za uchaguzi au apoteze sifa
za uchaguzi wa Naibu Spika; au
(c) ataondolewa kwenye madaraka ya Naibu Spika kwa Azimio la
Bunge.
Utaratibu
wa
kumchagua
Spika na
Naibu
Spika
131.-(1) Kutakuwa na uchaguzi wa Spika katika kikao cha kwanza
cha Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya, na katika kikao cha kwanza
chochote mara baada ya kutokea nafasi ya madaraka ya Spika kuwa wazi.
(2) Kutakuwa na uchaguzi wa Naibu Spika wakati wowote katika
Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya na vile vile katika kikao cha kwanza
cha Bunge kitakachofuata mara baada ya kutokea nafasi ya madaraka ya
Naibu Spika kuwa wazi.
(3) Uchaguzi wa Spika na Naibu Spika, utafanywa kwa kura ya siri,
na utaendeshwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Kanuni za Bunge.
(4) Spika na Naibu Spika watachaguliwa kwa masharti kwamba,
endapo Spika atatoka upande mmoja wa Washirika wa Muungano, Naibu
Spika atatoka upande wa pili wa Washirika wa Muungano.
(5) Isipokuwa kama ataacha madaraka yake, Spika na Naibu Spika
watakaa madarakani kwa vipindi visivyozidi viwili vya miaka mitano.
(6) Mtu yeyote atakayechaguliwa kuwa Spika au Naibu Spika
atatakiwa, kabla ya kuanza kutekeleza madaraka yake, kuapishwa katika
Bunge kiapo cha uaminifu.
Sifa za
mtu
anayefaa
kuchaguliwa
kuwa
Spika au
Naibu
Spika.
132. Mtu atastahili kuchaguliwa kuwa Spika au Naibu Spika
endapo atakuwa na sifa zifuatazo-
(a) angalau awe na elimu ya Chuo Kikuu kinachotambulika kwa
mujibu wa sheria za nchi;
(b) awe na sifa za kumuwezesha kuchaguliwa kuwa Mbunge;
(c) wakati wa kugombea, awe mwenye umri usiopungua miaka
arobaini; na
‐ 54 ‐
(d) asiwe kiongozi au amewahi kuwa kiongozi wa juu wa chama
cha siasa katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya
kuomba kuchaguliwa kushika nafasi ya madaraka ya Spika
au Naibu Spika.
(b) Ofisi ya Bunge
Katibu wa
Bunge
133.-(1) Kutakuwa na Katibu wa Bunge ambaye atateuliwa na
Tume ya Utumishi ya Bunge kutoka miongoni mwa watu wenye madaraka
ya juu katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
(2) Katibu wa Bunge atakuwa ndiye Mtendaji Mkuu wa Ofisi ya
Bunge na atawajibika kwa utendaji bora wa shughuli za Bunge kwa
kuzingatia masharti ya Katiba hii na sheria za nchi.
Sekretarieti
ya Bunge
134.(1) Kutakuwa na Sekretarieti ya Bunge itakayokuwa na
watumishi kutoka sehemu zote Washirika wa Muungano kwa kuzingatia
ngazi za utumishi kwa mujibu wa mahitaji ya shughuli za Bunge kama
itakavyoamuliwa na Tume ya Utumishi ya Bunge.
(2) Sekretarieti ya Bunge chini ya uongozi wa Katibu wa Bunge,
itatekeleza kazi na shughuli zote zilizowekwa au zitakazokuwa ni muhimu
kwa ajili ya kuhakikisha utekelezaji bora wa shughuli za Bunge, Wabunge
na madaraka ya Bunge.
SEHEMU YA NNE
UTARATIBU WA SHUGHULI BUNGENI
Kanuni za
Kudumu
za
Bunge
135.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, Bunge linaweza
kutunga Kanuni za Kudumu kwa ajili ya kuweka utaratibu wa kutekeleza
shughuli zake.
(2) Kanuni za Kudumu zilizotungwa kwa mujibu wa Ibara hii,
zinaweza kuweka utaratibu wa Mawaziri kuiwakilisha Serikali ndani ya
Bunge, kusimamia utekelezaji wa shughuli za Sekretarieti ya Bunge,
utekelezaji wa Shughuli za Bunge ndani ya Bunge, Kamati na Kamati
Ndogo za Bunge.
Rais
kulihutubia
Bunge
136.-(1) Rais atalihutubia Bunge Jipya katika Mkutano wa Kwanza
na kulifungua rasmi.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), Rais anaweza
wakati wowote kulihutubia Bunge au kupeleka kwenye Bunge taarifa
ambayo itasomwa na Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni.
(3) Rais anaweza kulihutubia Bunge katika kila kikao cha mwisho
wa mwaka kuelezea utekelezaji wa majukumu mbalimbali kwa mujibu wa
Katiba hii.
Mikutano
ya
Bunge
137.-(1) Bunge litafanya mikutano yake mahali ambapo ni desturi
kufanya Mikutano hiyo au mahali pengine popote katika Jamhuri ya
Muungano patakapotajwa na Spika kwa ajili hiyo.
(2) Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya katika Maisha ya Bunge
‐ 55 ‐
utaitishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano na utaanza siku ile ambayo
Bunge limegizwa kukutana, na kila Mkutano unaofuata utaanza siku
yoyote itakayopangwa na Bunge au siku yoyote itakayopangwa kwa
mujibu wa Kanuni za Bunge.
(3) Rais anaweza kuitisha Mkutano wa Bunge wakati wowote kwa
mujibu wa masharti ya Katiba hii.
Uongozi
na
vikao vya
Bunge
138. Kila kikao cha Bunge kitaongozwa na mmoja wapo wa watu
wafuatao-
(a) Spika; au
(b) ikiwa Spika hayupo, Naibu Spika; au
(c) ikiwa Spika na Naibu Spika wote hawapo, Mbunge yeyote
aliyechaguliwa na Bunge kwa ajili hiyo.
Akidi ya
vikao vya
Bunge.
139.-(1) Akidi ya kila kikao cha Bunge ni nusu ya Wabunge wote,
isipokuwa kama imeelezwa vinginevyo katika Katiba hii.
(2) Kila suala litakalowasilishwa kwa ajili ya kupata uamuzi wa
Bunge litaamuliwa kwa kufuata wingi wa kura za Wabunge waliohudhuria
na kupiga kura.
(3) Spika, Naibu Spika au mtu mwingine atakayeongoza kikao cha
Bunge, hatakuwa na kura ya kawaida bali atakuwa na kura ya uamuzi
kukitokea usawa wa kura.
Kamati za
Bunge
140.-(1) Bunge linaweza kuunda Kamati za Bunge za namna
mbalimbali kadri litakavyoona inafaa kwa ajili ya utekelezaji bora wa
madaraka yake.
(2) Kanuni za Bunge zinaweza kufafanua muundo na shughuli za
Kamati za Bunge zitakazoundwa kwa mujibu wa masharti ya Ibara hii.
SEHEMU YA TANO
MADARAKA NA HAKI ZA BUNGE
Uhuru wa
majadilia
no
Bungeni
141.-(1) Wabunge wakiwa Bungeni, watakuwa na uhuru wa kutoa
mawazo, maoni na majadiliano na uhuru huo hautavunjwa wala kuhojiwa
na chombo chochote katika Jamhuri ya Muungano, au katika Mahakama au
mahali pengine nje ya Bunge.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii au sheria nyingine
yoyote, Bunge litakuwa na uhuru wa maoni na Mbunge yeyote akiwa
Bungeni kwa vyovyote itakavyokuwa, hatatakiwa kutoa kauli za uongo,
kuudhi au kumuumiza Mbunge au mtu mwingine yeyote katika jamii.
(3)Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (2), Mbunge yeyote
hatashtakiwa kwa kosa la jinai au kufunguliwa shauri la madai
mahakamani kutokana na jambo lolote alilolisema ndani ya Bunge.
(4) Bunge linaweza kutunga sheria kwa ajili ya kuweka masharti ya
kuwezesha mahakama na sheria kuhifadhi na kutilia nguvu uhuru wa
mawazo, majadiliano na utaratibu wa shughuli katika Bunge.
‐ 56 ‐
Mipaka
ya
majadiliano
Bungeni
142.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii yanayolinda na
kuhifadhi uhuru wa mawazo na majadiliano katika Bunge, ni marufuku
kusema uongo Bungeni na kwa sababu hiyo, Mbunge anapokuwa
akizungumza ndani ya Bunge ana wajibu wa kuhakikisha kwamba
anatoa kauli au maelezo kuhusu jambo au suala ambalo yeye mwenyewe
anaamini kuwa ni la kweli na siyo jambo la kubuni au la kubahatisha tu.
(2) Mbunge anapokuwa akizungumza Bungeni hatahesabika wala
kutafsiriwa kuwa anasema uongo iwapo anafanya rejea ya habari kuhusu
jambo lililotangazwa au lililoandikwa na vyombo vya habari au nyaraka
nyingine yoyote ambayo chanzo chake kinafahamika au kitaelezwa na
Mbunge huyo.
SURA YA KUMI
MAHAKAMA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
SEHEMU YA KWANZA
MISINGI YA UTOAJI HAKI NA UHURU WA MAHAKAMA
Kuanzishwa
kwa
Mahakama
ya
Tanzania
143.-(1) Kutakuwa na Mahakama ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania.
(2) Mahakama ya Jamhuri ya Muunganokupitia Katiba hii,
itakuwa na mamlaka kutoka kwa wananchi na itatekeleza mamlaka
yake kupitia Mahakama ya Juu na Mahakama yaRufani.
(3) Mahakama ya Jamhuri ya Muunganoitakuwa ni chombo
chenye mamlaka ya mwisho ya utoaji haki katika Jamhuri ya
Muungano.
Misingi
ya utoaji
haki
144. Katika kutoa uamuzi wa mashauri ya madai na jinai kwa
kuzingatia sheria, Mahakama ya Jamhuri ya Muunganoitafuata kanuni
zifuatazo, yaani:
(a) kutenda haki kwa wote bila kujali hali ya mtu kijamii,
kisiasa, kiutamaduni au kiuchumi;
(b) kutochelewesha haki bila sababu ya kimsingi;
(c) kutoa fidia ipasayo kwa watu wanaoathirika kutokana na
makosa ya watu wengine, na kwa mujibu wa sheria za
nchi zilizotungwa mahususi kwa ajili hiyo;
(d) kukuza na kuendeleza usuluhishi baina ya wanaohusika
katika migogoro; na
(e) kutenda haki bila kufungwa na masharti ya kiufundi
yanayoweza kuchelewesha au kukwamisha haki
kutendeka.
Uhuru wa
Mahakama
145.-(1) Katika kutekeleza mamlaka ya utoaji haki, Mahakama
ya Jamhuri ya Muunganoitaongozwa na masharti ya Katiba hii na
haitaingiliwa ama kwa kudhibitiwa, kushinikizwa au kupewa maelekezo
na mtu au chombo chochote.
(2) Nafasi ya madaraka ya Jaji wa Mahakama ya Juu au
Mahakama ya Rufani haitafutwa wakati wowote ule ikiwa kuna mtu
ambaye kwa wakati huo anashikilia nafasi hiyo.
‐ 57 ‐
(3) Mishahara na malipo mengine ya Majaji wa Mahakama ya
Juu na Mahakama ya Rufani yatalipwa kutoka katika Mfuko Mkuu wa
Hazina ya Serikali.
(4) Mshahara na malipo mengine yanayolipwa kwa Jaji wa
Mahakama ya Juu au wa Mahakama ya Rufani hayatabadilishwa kwa
maana ya kumuondolea faida Jaji husika.
(5) Malipo ya mafao ya kustaafu ya Jaji wa Mahakama ya Juu au
Jaji wa Mahakama ya Rufani hayatabadilishwa kwa maana ya
kumuondolea faida Jaji husika wakati wote wa uhai wake.
(6) Mtumishi yeyote wa Mahakama hatoshtakiwa kwa jambo
lolote alilolifanya au kutolifanya kwa nia njema katika utekelezaji wa
shughuli ya utoaji haki kwa mujibu wa Sheria.
SEHEMU YA PILI
MUUNDO WA MAHAKAMA
(a) Mahakama za Jamhuri ya Muungano
Muundo
wa
Mahakama
146.-(1) Bila ya kuathiri masharti yoyote yaliyotangulia katika
Sehemu hii, kutakuwa na Muundo wa Mahakama katika Jamhuri ya
Muungano utakaokuwa kama ifuatavyo:
(a) Mahakama ya Juu; na
(b) Mahakama ya Rufani.
(2)Mahakama Kuu ya Tanzania Bara na Mahakama Kuu ya
Zanzibar zitakuwa na mamlaka sawa ya kusikiliza katika ngazi ya awali,
mashauri ya madai na jinai kuhusu Mambo ya Muungano katika maeneo
ya utawala ya Washirika wa Muungano.
(b) Mahakama ya Juu ya Jamhuri ya Muungano
Mahakama
ya Juu
147.-(1)Kutakuwa na Mahakama ya Juu ya Jamhuri ya
Muungano au kwa kifupi itaitwa “Mahakama ya Juu” ambayo itakuwa
na:
(a) Jaji Mkuu ambaye atakuwa Rais wa Mahakama ya Juu;
(b) Naibu Jaji Mkuu ambaye atakuwa Makamu wa Rais wa
Mahakama ya Juu; na
(c) Majaji wengine wa Mahakama ya Juu wasiopungua saba.
(2)Uteuzi wa Majaji wa Mahakama ya Juu utazingatia sifa
zitakazoainishwa katika Katiba hii na uwakilishi wa sehemu mbili za
Washirika waMuungano.
Akidi ya
vikao vya
Mahakama
ya Juu
148.-(1)Akidi ya kikao cha Mahakama ya Juu itakuwa ni Majaji
wa Mahakama ya Juu watano.
(2) Akidi ya Majaji katika vikao vya Mahakama ya Juu kwa
madhumuni ya kusikiliza shauri linalohusu masuala yaliyoainishwa
katika Ibara ya 149(1) (a), (b), (c) na (e) itazingatia uwakilishi wa
sehemu mbili za Muungano.
(3) Kila shauri na rufani inayohitaji uamuzi wa Mahakama ya
Juu itaamuliwa kwa kufuata kauli ya walio wengi kati ya Majaji wa
‐ 58 ‐
Mahakama ya Juu waliosikiliza shauri au rufani hiyo.
Madaraka
ya
Mahakama
ya Juu
149.-(1) Mahakama ya Juu itakuwa ni ngazi ya mwisho ya rufani
katika Jamhuri ya Muungano na itakuwa na madaraka ya:
(a) pekee na ya awali ya kusikiliza na kuamua mashauri
yanayohusu matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano;
(b) kusikiliza na kuamua mashauri yanayoletwa na Serikali ya
Muungano au Serikali za Washirika kuhusu tafsiri ya Katiba
hii;
(c) kusikiliza na kuamua migogoro baina ya Washirika wa
Muungano au baina wa Mshirika wa Muungano na Serikali
ya Muungano;
(d) kusikiliza na kuamua rufani kutoka Mahakama ya Rufani;
(e) kutoa maoni ya kiushauri kwa Serikali ya Muungano au
Serikali za Washirika; na
(f) kusikiliza na kuamua shauri lolote litakalowasilishwa mbele
yake kwa mujibu wa Katiba hii au sheria nyingine yoyote
itakayoipa Mahakama hiyo mamlaka.
(2) Mahakama ya Jamhuri ya Muungano pamoja na mahakama
za Washirika wa Muungano, isipokuwa Mahakama ya Juu zitabanwa na
maamuzi ya Mahakama ya Juu.
(3) Mahakama ya Juu itaandaa Kanuni kwa ajili ya utekelezaji
wa mamlaka yake.
(4) Bunge linaweza kutunga sheria itakayoweka masharti zaidi
kuhusu uendeshaji wa Mahakama ya Juu.
Madaraka
ya Majaji
wa
Mahakama
ya Juu
150.-(1) Jaji yeyote wa Mahakama ya Juu hatakuwa na mamlaka
ya kusikiliza na kuamua shauri lolote katika Mahakama ya Rufani au
katika Mahakama ya ngazi yoyoteiliyo chini ya mamlaka ya Washirika
wa Muungano.
(2) Bila kujali masharti ya Ibara ndogo ya (1) iwapo Jaji wa
Mahakama ya Juu, kabla ya kuteuliwa kwake alikuwa Jaji wa
Mahakama ya Rufani au Mahakama ya Washirika wa Muungano
aunyingine yoyote, Jaji huyo anaweza kuendelea kufanya kazi zake
katika Mahakama aliyotoka mpaka amalize kutayarisha na kutoa
hukumu au mpaka akamilishe shughuli nyingine yoyote inayohusika na
mashauri ambayo alikwishaanza kuyasikiliza kabla hajateuliwa kuwa
Jaji wa Mahakama ya Juu.
(3) Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ndogo ya (2), itakuwa ni
halali kwa Jaji wa Mahakama ya Juu kutoa hukumu au uamuzi
mwingine wowote unaohusika kwa kutumia na kutaja nafasi ya
madaraka aliyokuwa akishika kabla ya kuteuliwa kuwa Jaji wa
Mahakama ya Juu na endapo hukumu hiyo au uamuzi huo utapingwa
kwa njia ya rufani itakayofikishwa mbele ya Mahakama ya Juu, Jaji
huyo hatakuwa na mamlaka ya kusikiliza rufani hiyo.
‐ 59 ‐
(c)Uteuzi wa Majaji wa Mahakama ya Juu
Uteuzi wa
Jaji Mkuu
151.-(1) Jaji Mkuu atateuliwa na Rais kutoka miongoni mwa
majina ya watu watatu yaliyopendekezwa na Tume ya Utumishi wa
Mahakama na kabla ya kuapishwa jina lake litawasilishwa Bungeni kwa
ajili ya kuthibitishwa na Bunge.
(2) Jaji Mkuu ndiye atakuwa Mkuu wa Mhimili wa Mahakama
katika Jamhuri ya Muungano.
(3) Mtu ataweza kuteuliwa kuwa Jaji Mkuu endapo atakuwa
amefikisha umri wa miaka arobaini na tano au zaidi na mwenye sifa ya
uadilifu, tabia njema, uaminifu na:
(a) awe na shahada ya sheria kutoka katika chuo
kinachotambuliwa na mamlaka inayoshughulikia elimu ya juu
katika Jamhuri ya Muungano;
(b) awe amefanya kazi ya uhakimu, ujaji, utumishi wa umma au
uanataaluma akiwa na sifa ya kufanya kazi ya uwakili au ni
wakili wa kujitegemea;
(c) awe na sifa ya kusajiliwa kuwa wakili,
na amekuwa na sifa hizo mfululizo kwa muda usiopungua miaka kumi na
mitano.
Uteuzi wa
Naibu Jaji
Mkuu
152.-(1) Naibu Jaji Mkuu atateuliwa na Rais kutoka miongoni
mwa majina ya watu watatu yatakayopendekezwa na Tume ya Utumishi
wa Mahakama na kabla ya kuapishwa jina lake litawasilishwa Bungeni
kwa ajili ya kuthibitishwa na Bunge.
(2) Mtu atateuliwa kuwa Naibu Jaji Mkuu endapo atakuwa na sifa
zilizoainishwa katika Ibara ya 151 na kwa kufuata kanuni kwamba endapo
Jaji Mkuu atatoka sehemu moja ya Muungano, basi Naibu Jaji Mkuu
atatoka sehemu ya pili ya Muungano.
(3) Naibu Jaji Mkuu atakuwa ndiye Msaidizi Mkuu wa Jaji Mkuu
katika utekelezaji wa majukumu yake kama Mkuu wa Mhimili wa
Mahakama.
Uteuzi wa
Majaji wa
Mahakama
ya Juu
153.-(1) Majaji wa Mahakama ya Juu watateuliwa na Rais kutoka
miongoni mwa majina yatakayopendekezwa na Tume ya Utumishi wa
Mahakama na wataapishwa na Rais.
(2) Mtu ataweza kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Juu endapo
atakuwa na sifa ya uadilifu, tabia njema na uaminifu na:
(a) awe na shahada ya sheria kutoka katika chuo
kinachotambuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi;
(b) awe amefanya kazi ya uhakimu, ujaji, utumishi wa umma au
uanataaluma akiwa na sifa ya kufanya kazi ya uwakili au ni
wakili wa kujitegemea; na
(c) awe na sifa ya kusajiliwa kuwa wakili,
na amekuwa na sifa hizo mfululizo kwa muda usiopungua miaka kumi.
(3) Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ndogo ya (2), iwapo Rais
ataridhika kwamba japokuwa:
(a) mtu mwenye sifa mojawapo ya hizo sifa zilizoainishwa
katika Ibara ndogo ya (2) hakuwa nayo sifa hiyo kwa muda
‐ 60 ‐
unaopungua miaka kumi; na
(b) mtu huyo ana uwezo, ujuzi na kwa kila hali anafaa
kukabidhiwa madaraka ya Jaji wa Mahakama ya Juu;
(c) kuna sababu za kumfanya mtu huyo kustahili kukabidhiwa
nafasi ya madaraka hayo,
basi Rais anaweza kutengua sharti la kuwa na sifa kwa muda usiopungua
miaka kumi, na baada ya kushauriana na Tume ya Utumishi wa
Mahakama, kumteua mtu huyo kuwa Jaji wa Mahakama ya Juu.
Kiapo cha
Majaji wa
Mahakama
ya Juu
154. Jaji Mkuu, Naibu Jaji Mkuu au Jaji wa Mahakama ya Juu
atashika madaraka yake mara tu atakapokuwa ameapishwa na Rais kiapo
cha uaminifu na kiapo kingine chochote kinachohusika na utendaji wa
kazi kitakachowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.
Muda wa
kuwa
madarakani
kwa
Jaji Mkuu,
Naibu Jaji
Mkuu na
Majaji
wengine
155.-(1) Jaji Mkuu na Naibu Jaji Mkuu watashika madaraka yao
mpaka watakapofikisha umri wa miaka sabini, isipokuwa tu kama:
(a) watajiuzulu;
(b) nafasi ya madaraka ya Jaji Mkuu itakuwa wazi kutokana na
maradhi au kifo; au
(c) atavuliwa wadhifa wa Jaji Mkuu kwa mujibu wa Katiba hii.
(2) Masharti ya Ibara ndogo ya (1) yatatumika pia kwa Naibu Jaji
Mkuu na Jaji wa Mahakama ya Juu.
(3) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1) na (2), Jaji
Mkuu, Naibu Jaji Mkuu na Jaji wa Mahakama ya Juualiyetimiza umri wa
kustaafu atalazimika kuendelea kufanya kazi baada ya kutimiza umri huo
mpaka amalize kutayarisha na kutoa hukumu au mpaka akamilishe
shughuli nyingine yoyote inayohusika na mashauri ambayo alikwishaanza
kuyasikiliza kabla hajatimiza umri wa kustaafu.
Utaratibu
wa
kukaimu
katika
Mahakama
ya Juu
156.-(1) Iwapo itatokea kwamba:-
(a) nafasi ya madaraka ya Jaji Mkuu itakuwa wazi;
(b) Jaji Mkuu hayupo katika Jamhuri ya Muungano; au
(c) Jaji Mkuu atashindwa kumudu kutekeleza kazi zake kwa
sababu yoyote,
Naibu Jaji Mkuu atatekeleza kazi za Jaji Mkuu mpaka atakapoteuliwa Jaji
Mkuu mwingine au mpaka Jaji Mkuu ambaye alikuwa hayupo au alikuwa
hamudu kazi zake atakaporejea kazini.
(2) Ikitokea kwamba nafasi ya madaraka ya Jaji wa Mahakama ya
Juuitakuwa wazi au endapo Jaji wa Mahakama ya Juu yeyote ameteuliwa
kutekeleza kazi za Naibu Jaji Mkuu au kama Jaji waMahakama ya Juu
atashindwa kutekeleza kazi zake kwa sababu yoyote, au Jaji Mkuu
atamshauri Rais kuwa kazi za Mahakama ya Juu zilivyo kwa wakati huo
zinahitaji ateuliwe Kaimu Jaji wa Mahakama ya Juu, basi Rais anaweza
kumteua Kaimu Jaji wa Mahakama ya Juu kutoka miongoni mwa watu
wanaoweza kuteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama ya Juu kama
‐ 61 ‐
watakaopendekezwa na Tume ya Utumishi wa Mahakama.
(3) Mtu atakayeteuliwa kuwa Kaimu Jaji wa Mahakama ya Juu
atafanya kazi kama Kaimu Jaji wa Mahakama ya Juu kwa muda wote
utakaotajwa kwenye hati ya kuteuliwa kwake.
(4) Bila kujali masharti ya Ibara ndogo ya (2), mtu aliyeteuliwa
kuwa Kaimu Jaji wa Mahakama ya Juu ataendelea kufanya kazi kama
Kaimu Jaji wa Mahakama ya Juu mpaka amalize kutayarisha na kutoa
hukumu au mpaka amalize shughuli nyingine yoyote inayohusika na
rufani au mashauri mengine ambayo alikwishaanza kuyasikiliza kabla ya
muda wake wa uteuzi haujamalizika au uteuzi wake haujafutwa.
(5) Kwa madhumuni ya kuondoa mashaka, Kaimu Jaji
waMahakama ya Juu atakuwa na mamlaka kamili ya Jaji wa Mahakama
ya Juu na atatekeleza kazi zote za Jaji wa Mahakama ya Juu na kwamba
idadi ya Majaji wa Mahakama ya Juuiliyotajwa katika Ibara ya
147haitaathirika kwa sababu tu mmoja au zaidi ya Majaji wa Mahakama
ya Juu katika kikao chochote ni Kaimu Jaji wa Mahakama ya Juu.
Utaratibu
wa
kushughulikia
nidhamu
ya Majaji
wa
Mahakama
ya Juu
157.-(1) Utaratibu wa kushughulikia nidhamu ya Majaji wa
Mahakama ya Juu, mbali na sababu zilizoainishwa katika Ibara ndogo ya
(2), utakuwa kama utakavyoelezwa na sheria itakayotungwa na Bunge.
(2) Jaji wa Mahakama ya Juu anaweza kuondolewa madarakani
kwa sababu ya kushindwa kutekeleza madaraka yake ama kutokana na
maradhi au sababu nyingine yoyote au kwa sababu ya tabia mbaya
inayoathiri maadili ya kazi ya Jaji au Sheria ya Maadili ya Viongozi wa
Umma; na hataweza kuondolewa kazini ila kwa mujibu wa masharti ya
Ibara ndogo ya (4).
(3) Endapo Rais anaona kuwa suala la kumuondoa Jaji kazini
linahitaji kuchunguzwa, basi katika hali hiyo utaratibu utakuwa kama
ufuatavyo:
(a) Rais anaweza, baada ya kushauriana na Jaji Mkuu,
kumsimamisha kazi Jaji huyo;
(b) Rais atateua Tume ambayo itakuwa na Mwenyekiti na
Wajumbe wengine wasiopungua wawili; na angalau nusu ya
wajumbe hao wawe ni Majaji wa Mahakama ya Juu au
Mahakama ya Rufani kutoka nchi yoyote iliyomo kwenye
Jumuiya ya Madola; na
(c) Tume hiyo itachunguza shauri lote kisha itatoa taarifa kwa
Rais kuhusu maelezo ya shauri hilo na itamshauri Rais kama
Jaji huyo anayehusika aondolewe kazini kwa mujibu wa
masharti ya Ibara hii kwa sababu ya kushindwa kufanyakazi
kutokana na maradhi au sababu nyingine yoyote au kwa
sababu ya tabia mbaya.
(4) EndapoTume iliyoteuliwa kwa mujibu wa masharti ya Ibara
ndogo ya (3) itamshauri Rais kwamba Jaji ambaye mwenendo wake
umechunguzwa na Tume hiyo aondolewe kazini kwa sababu ya
kushindwa kufanyakazi kutokana na maradhi au sababu nyingine yoyote
au kwa sababu ya tabia mbaya, Rais atamuondoa kazini Jaji huyo na
utumishi wake utakuwa umekoma.
‐ 62 ‐
(5) Ikiwa suala la kumuondoa Jaji kazini limepelekwa kwenye
Tume kwa ajili ya uchunguzi kwa mujibu wa masharti ya Ibara ndogo ya
(3), Rais anaweza kumsimamisha kazi Jaji huyo anayehusika, na Rais
anaweza wakati wowote kufuta uamuzi huo wa kumsimamisha kazi Jaji
huyo, na kwa hali yoyote uamuzi huo utabatilika ikiwa Tume itamshauri
Rais kwamba Jaji huyo asiondolewe kazini.
(6) Masharti ya Ibara hii hayatawahusu watu walioteuliwa
kukaimu nafasi ya Ujaji.
(d)Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano
Mahakama
ya Rufani
158.-(1) Kutakuwa na Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya
Muungano,itakayojulikana kwa kifupi kama “Mahakama ya Rufani” na
ambayo itakuwa na:
(a) Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani; na
(b) Majaji wengine wasiopungua kumi na saba.
(2) Majaji wa Mahakama ya Rufani watateuliwa kwa kuzingatia
sifa zitakazoainishwa katika Katiba hii na uwiano wa uwakilishi wa
sehemu mbili za Washirika waMuungano.
(3) Sheria zitakazotungwa kwa mujibu wa Katiba za Washirika wa
Muungano zitaweka masharti kuhusu utaratibu wa kuwasilisha rufani
mbele ya Mahakama ya Rufani, nyakati na sababu za kukata rufani.
Akidi ya
vikao vya
Mahakama
ya Rufani
159.-(1) Akidi ya kila kikao cha Mahakama ya Rufani itakuwa ni
Majaji wa Mahakama ya Rufani wasiopungua watatu.
(2) Kila shauri na rufani inayohitaji uamuzi wa Mahakama ya
Rufani itaamuliwa kwa kufuata kauli ya walio wengi kati ya Majaji wa
Mahakama ya Rufani waliosikiliza shauri au rufani husika.
Mamlaka
ya
Mahakama
ya
Rufani
160.-(1) Mahakama ya Rufani itakuwa na:
(a) mamlaka ya kusikiliza na kuamua juu ya kila rufani
inayowasilishwa mbele ya mahakama ya Rufani kutokana na
hukumu au uamuzi wowote wa Mahakama Kuu au mahakama
yoyote ya chini iliyopewa mamlaka maalum ya kuwa
Mahakama Kuu hizo;
(b) mamlaka ya kufanya mapitio ya maamuzi ya Mahakama Kuu;
na
(c) mamlaka nyinginekama itakavyoainishwa kwenye sheria
itakayotungwa na Bunge.
(2)Mahakama ya Rufani itaandaa Kanuni kwa ajili ya utekelezaji
wa mamlaka yake.
(3)Bunge linaweza kutunga sheria itakayoweka masharti zaidi
kuhusu uendeshaji wa Mahakama ya Rufani.
‐ 63 ‐
Mamlaka
ya Majaji
wa
Mahakama
ya Rufani
161.-(1) Jaji yeyote wa Mahakama ya Rufani hatakuwa na
mamlaka ya kusikiliza na kuamua shauri lolote katika Mahakama ya ngazi
yoyote isipokuwa Mahakama ya Rufani.
(2) Bila yakujali masharti ya Ibara ndogo ya (1), iwapo Jaji wa
Mahakama ya Rufani kabla ya kuteuliwa kwake alikuwa Jaji wa
Mahakama ya Kuu za Washirika wa Muungano au hakimu wa mahakama
nyingine yoyote ya Washirika wa Muungano, Jaji huyo anaweza
kuendelea kufanya kazi katikamahakama aliyotoka mpaka amalize
kutayarisha na kutoa hukumu au mpaka akamilishe shughuli nyingine
yoyote inayohusika na mashauri ambayo alikwishaanza kuyasikiliza kabla
hajateuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.
(3) Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ndogo ya (2), itakuwa ni
halali kwa Jaji wa Mahakama ya Rufani kutoa hukumu au uamuzi
mwingine wowote unaohusika kwa kutumia na kutaja nafasi ya madaraka
aliyokuwa akishika kabla ya kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani
na endapo hukumu hiyo au uamuzi huo utapingwa kwa njia ya rufani
itakayowasilishwa mbele ya Mahakama ya Rufani, Jaji huyo hatakuwa na
mamlaka ya kusikiliza rufani hiyo.
(e)Uteuzi wa Majaji wa Mahakama ya Rufani
Uteuzi wa
Mwenyekiti
wa
Mahakama
ya Rufani
162.-(1) Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani atateuliwa na Rais
kutoka miongoni mwa majina ya watu watatu yatakayopendekezwa na
Tume ya Utumishi wa Mahakama.
(2) Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani atakuwa ndiye Mkuu wa
Mahakama ya Rufani na msaidizi wa Jaji Mkuu katika utendaji wa kazi
katika Mahakama ya Rufani, na katika madaraka hayo, Mwenyekiti wa
Mahakama ya Rufani atatekeleza kazi na shughuli atakazopangiwa mara
kwa mara na Jaji Mkuu.
(3) Mtu anaweza kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Mahakama ya
Rufani endapo atakuwa amefikisha umri wa miaka arobaini na tano au
zaidi na mwenye sifa ya uadilifu, tabia njema na uaminifu na:
(a) awe na Shahada ya Sheria kutoka katika Chuo Kikuu
kinachotambuliwa na mamlaka inayoshughulikia elimu ya juu
katika Jamhuri ya Muungano;
(b) awe amefanya kazi ya uhakimu, ujaji, utumishi wa umma au
uanataaluma akiwa na sifa ya kufanya kazi ya uwakili au ni
Wakili wa Kujitegemea; na
(c) awe na sifa ya kusajiliwa kuwa wakili,
na amekuwa na sifa hizo mfululizo kwa muda usiopungua miaka kumi.
(4) Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ndogo ya (2), iwapo Rais
ataridhika kwamba japokuwa:
(a) mtu mwenye sifa mojawapo ya hizo sifa zilizoainishwa
katika Ibara ndogo ya (2) hakuwa nayo sifa hiyo kwa muda
usiopungua miaka kumi;
(b) mtu huyo ana uwezo, ujuzi na kwa kila hali anafaa
kukabidhiwa madaraka ya Jaji wa Mahakama ya Rufani;
‐ 64 ‐
(c) kuna sababu za kumfanya mtu huyo astahili kukabidhiwa
madaraka hayo,
basi Rais anaweza kutengua sharti la kuwa na sifa kwa muda usiopungua
miaka kumi, na baada ya kushauriana na Tume ya Utumishi wa
Mahakama, Rais anaweza kumteua mtu huyo kuwa Jaji wa Mahakama ya
Rufani.
Uteuzi wa
Majaji wa
Mahakama
ya Rufani
163.-(1) Majaji wa Mahakama ya Rufani watateuliwa na Rais
kutoka miongoni mwa majina yatakayopendekezwa na Tume ya Utumishi
wa Mahakama.
(2) Mtu anaweza kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani
endapo atakuwa na sifa ya uadilifu, tabia njema na uaminifu na:
(a) awe na shahada ya sheria kutoka katika chuo kinachotambuliwa na
mamlaka inayoshughulikia elimu ya juu katika Jamhuri ya
Muungano;
(b) awe amefanya kazi ya uhakimu, ujaji, utumishi wa umma au
uanataaluma akiwa na sifa ya kufanya kazi ya uwakili au ni wakili
wa kujitegemea; na
(c) awe na sifa ya kusajiliwa kuwa wakili,
na amekuwa na sifa hizo mfululizo kwa muda usiopungua miaka kumi.
Kiapo cha
Majaji wa
Mahakama
ya Rufani
164.-Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani, au Jaji wa Mahakama
ya Rufani atashika madaraka yake mara tu atakapoapishwa na Rais kiapo
cha uaminifu na kiapo kingine chochote kinachohusika na utendaji wa
kazi kitakachowekwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.
Muda wa
kuwa
madarakani
kwa
Mwenyekiti
na Majaji
wengine wa
Mahakama
ya Rufani
165.-(1) Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani atashika nafasi
yamadaraka ya Ofisi ya Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani mpaka
atakapofikisha umri wa miaka sabini, isipokuwa kama:
(a) atajiuzulu;
(b) kiti chake kitakuwa wazi kutokana na maradhi au kifo; au
(c) atavuliwa wadhifa wa Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani
kwa mujibu wa Katiba hii.
(2) Naibu Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani au Jaji wa
Mahakama ya Rufani atashika madaraka mpaka atakapotimiza umri wa
miaka sabini, isipokuwa kama:
(a) atajiuzulu;
(b) nafasi ya madaraka ya Mwenyekiti wa mahakama ya
Rufaniitakuwa wazi kutokana na maradhi au kifo; au
(c) atavuliwa wadhifa wake kwa mujibu wa Katiba hii.
(3) Bila ya kujali masharti ya Ibara ya ndogo ya (1)na (2), Jaji
aliyetimiza umri wa kustaafu atalazimika kuendelea kufanya kazi baada ya
kutimiza umri huo mpaka amalize kutayarisha na kutoa hukumu au mpaka
akamilishe shughuli nyingine yoyote inayohusika na mashauri ambayo
alikwishaanza kuyasikiliza kabla hajatimiza umri wa kustaafu.
‐ 65 ‐
Utaratibu
wa
kukaimu
katika
Mahakama
ya Rufani
166.-(1) Iwapo itatokea kwamba:-
(a) nafasi ya madaraka ya Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani
ipo wazi;
(b) Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani hayupo katika Jamhuri
ya Muungano;
(c) Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani atashindwa kutekeleza
kazi yake kwa sababu yoyote,
Jaji Mkuu anaweza kumteua Jaji wa Mahakama ya Rufani yoyote
kutekeleza kazi za Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani mpaka
atakapoteuliwa Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani mwingine au mpaka
Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani ambaye alikuwa hayupo Tanzania
au alikuwa hawezi kumudu kazi zake kutokana na maradhi atakaporejea
kazini.
(2) Ikitokea kwamba kiti cha Jaji wa Mahakama ya Rufani
kitakuwa wazi au endapo Jaji wa Rufani yeyote ameteuliwa kutekeleza
kazi za Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani au Jaji wa Mahakama ya
Rufani atashindwa kutekeleza kazi zake kwa sababu yoyote, Jaji Mkuu
atamshauri Rais kuwa ufanisi wa kazi za Mahakama ya Rufani unahitaji
ateuliwe Kaimu Jaji wa Mahakama ya Rufani.
(3) Endapo Rais akiridhika na ushauri wa Jaji Mkuu, atamteua
Kaimu Jaji wa Mahakama ya Rufani kutoka miongoni mwa watu
wanaoweza kuteuliwa kuwa Majaji wa Mahakama ya Rufani.
(4) Mtu atakayeteuliwa kuwa Kaimu Jaji wa Rufani atafanya kazi
kama Kaimu Jaji wa Rufani kwa muda wote utakaotajwa wakati wa
kuteuliwa kwake, au kama muda haukutajwa, basi mpaka uteuzi
utakapofutwa na Rais.
(5) Bila kujali masharti ya Ibara ndogo ya (4), mtu aliyeteuliwa
kuwa Kaimu Jaji wa Rufani ataendelea kufanya kazi kama Kaimu Jaji wa
Mahakama ya Rufani mpaka amalize kutayarisha na kutoa hukumu au
mpaka amalize shughuli nyingine yoyote inayohusika na rufani au
mashauri mengine ambayo alikwishaanza kuyasikiliza kabla ya muda
wake wa kazi haujamalizika au uteuzi wake haujafutwa.
(6) Kwa madhumuni ya kuondoa shaka, Kaimu Jaji wa Mahakama
ya Rufani atakuwa na mamlaka kamili ya Jaji wa Mahakama ya Rufani na
atatekeleza kazi zote za Jaji wa Mahakama ya Rufani na kwamba idadi ya
Majaji iliyotajwa katika Ibara ya 158 haitaathirika kwa sababu tu akidi ya
Majaji wa Mahakama ya Rufani katika kikao chochote ni pamoja
naKaimu Jaji wa Mahakama ya Rufani.
Utaratibu
wa
kushughulikia
nidhamu
ya Majaji
wa
Mahakama
ya Rufani
167.-(1) Utaratibu wa kushughulikia nidhamu ya Majaji wa
Mahakama ya Rufani, kwa sababu ambazo ni tofauti na zilizoainishwa
katika nafasi ya Ibara ndogo ya (2), utakuwa kama utakavyoelezwa katika
Sheria itakayotungwa na Bunge.
(2) Jaji wa Mahakama ya Rufani anaweza kuondolewa katika
nafasi ya madaraka yaJaji kwa sababu ya kushindwa kutekeleza kazi yake
kutokana na:
‐ 66 ‐
(a) maradhi ya akili au mwili;
(b) kukiuka Kanuni za Maadili ya Majaji wa Mahakama ya Rufani
zilizotungwa kwa mujibu wa sheria;
(c) kutokuwa na uwezo wa kumudu kazi za nafasi ya Jaji; au
(d) tabia mbaya au mwenendo usiofaa unaoathiri Sheria ya Maadili
ya Viongozi wa Umma.
(3) Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani, Naibu Mwenyekiti wa
Mahakama ya Rufani na Jaji wa Rufani wataweza kuondolewa katika
nafasi ya madaraka ya Jaji kwa kufuata utaratibu unaofanana na ule
uliowekwa kwa ajili ya kumuondoa kazini Jaji Mkuu, Naibu Jaji Mkuu na
Jaji wa Mahakama ya Juu kama ilivyoelezwa.
(f)Usimamizi wa Shughuli za Mahakama
Msajili wa
Mahakama
168.-(1)Kutakuwa na Msajili wa Mahakama atakayeteuliwa na
Rais kufuatia mapendekezo ya Tume ya Utumishi wa Mahakama na baada
kuidhinishwa na Bunge.
(2) Mtu hatateuliwa kushika nafasi ya Msajili wa Mahakama
isipokuwa tu kama:
(a) ana shahada ya sheria kutoka katika chuo kinachotambuliwa kwa
mujibu wa Sheria za nchi;
(b) awe amefanya kazi ya uhakimu, utumishi wa umma au
mwanataaluma akiwa na sifa ya kufanya kazi ya uwakili wa
Serikali au ni wakili wa kujitegemea;
(c) awe na sifa ya kusajiliwa kuwa wakili; na
(d) ni mwadilifu na mwenye tabia na mwenendo mwema,
na amekuwa na sifa hizo mfululizo kwa muda usiopungua miaka kumi.
Majukumu
ya Msajili
wa
Mahakama
169.-(1) Msajili wa Mahakama atakuwa na majukumu yafuatayo:
(a) kusimamia utekelezaji wa shughuli za kimahakama;
(b) kuratibu masuala ya kimahakama; na
(c) majukumu mengine atakayopangiwa na Jaji Mkuu.
(2) Katika kutekeleza majukumu yake, Msajili wa Mahakama
atawajibika kwa Tume ya Utumishi wa Mahakama.
Mtendaji
Mkuu wa
Mahakama
170.-(1) Kutakuwa na Mtendaji Mkuu wa Mahakama
atakayeteuliwa na Rais kutoka miongoni mwa Watumishi wa Umma
kufuatia mapendekezo ya Tume ya Utumishi wa Mahakama na
kuidhinishwa na Bunge.
(2) Mtu hatateuliwa kushika nafasi ya Mtendaji Mkuu wa
Mahakama isipokuwa tu kama ni:
(a) mtumishi wa umma mwandamizi;
(b) ana weledi na uzoefu katika masuala ya utawala na mambo ya
fedha; na
(c) mwadilifu na mwenye tabia na mwenendo mwema.
‐ 67 ‐
Majukumu
ya
Mtendaji
Mkuu wa
Mahakama
171.-(1) Mtendaji Mkuu wa Mahakama atakuwa na majukumu
yafuatayo:
(a) Katibu wa Tume ya Utumishi wa Mahakama;
(b) Afisa Masuuli wa Mahakama;
(c) msimamizi mkuu wa Mfuko wa Mahakama;
(d) msimamizi wa masuala ya utawala ya Mahakama; na
(e) atatekeleza majukumu mengine atakayopangiwa na Jaji Mkuu.
(2) Katika kutekeleza majukumu yake, Mtendaji Mkuu wa
Mahakama atawajibika kwa Tume ya Utumishi wa Mahakama.
SEHEMU YA TATU
TUME YA UTUMISHI WA MAHAKAMA NA MFUKO WA MAHAKAMA
(a) Tume ya Utumishi wa Mahakama
Tume ya
Utumishi
wa
Mahakama
172.-(1) Kutakuwa na Tume ya Utumishi wa Mahakama ambayo
itaundwa na wajumbe tisa watakaoteuliwa na Rais kama ifutavyo:
(a) Jaji Mkuu ambaye atakuwa ni Mwenyekiti;
(b) Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano;
(c) Jaji mmoja wa Mahakama ya Juu;
(d) Jaji mmoja wa Mahakama ya Rufani;
(e) Mwakilishi wa Chama cha Wanasheria wa Tanzania Bara;
(f) Mwakilishi wa Chama cha Wanasheria wa Zanzibar;
(g) Wakuu Wawili wa vitivo vya sheria kutoka vyuo vikuu, mmoja
kutoka Tanzania Bara na moja kutoka Zanzibar
watakaopendekezwa na Jaji Mkuu; na
(h) Mtendaji Mkuu wa Mahakama ambaye atakuwa Katibu wa
Tume ya Utumishi wa Mahakama.
(2) Tume inaweza kumualika mtu mwingine yoyote mwenye
utaalamu mahususi kushiriki kikao chochote cha Tume, isipokuwa mtu
huyo hatakuwa nahaki ya kupiga kura.
(3) Tume itaweka utaratibu wa kuendesha vikao vyake.
Majukumu
ya Tume
ya
Utumishi
wa
Mahakama
173.-(1) Tume ya Utumishi wa Mahakama itakuwa na wajibu wa
kuendeleza na kuwezesha uhuru na uwajibikaji wa Mahakama na utoaji
haki wenye ufanisi, mafanikio na uwazi.
(2) Tume ya Utumishi wa Mahakama itakuwa na wajibu wa:
(a) kupendekeza kwa Rais majina ya watu wanaofaa kuteuliwa
kuwa Majaji wa Mahakama ya Juu na Mahakama ya Rufani;
(b) kupitia na kupendekeza masharti ya utumishi wa Majaji na
watumishi wengine wa mahakama ikiwemo masuala
yanayohusu nidhamu na maslahi yao;
(c) kuteua wasajili na kuajiri watumishi wengine wa Mahakama,
kupokea malalamiko dhidi yao na kuwachukulia hatua za
kinidhamu ikiwemo kuwafukuza kazi kwa mujibu wa Sheria
itakayotungwa na Bunge;
(d) kuandaa na kutekeleza mipango ya kujiendeleza kielimu kwa
Majaji na watumishi wengine wa Mahakama;
‐ 68 ‐
(e) kupendekeza Serikalini maboresho ya Mahakama ili kuongeza
ufanisi katika utoaji haki;
(f) kutoa fursa ya majadiliano kuhusu utekelezaji wa majukumu
ya Mahakama ya Jamhuri ya Muunganona hivyo kumsaidia
Jaji Mkuu katika kutekeleza majukumu yake kwa malengo ya
kuleta ufanisi na mafanikio katika utoaji haki; na
(g) kutekeleza majukumu yoyote itakayopewa kwa mujibu wa
Katiba hii au sheria zingine.
(3) Katika kutekeleza majukumu yake, Tume itazingatia:
(a) uwazi katika mchakato wa uteuzi wa Majaji na ajira ya
watumishi wengine wa Mahakama ya Jamhuri ya
Muungano;
(b) uwakilishi wa sehemu mbili za Washirika wa Muungano; na
(c) uwakilishi wa kijinsia.
(4) Katika kutekeleza majukumu yake, Tume inaweza kukasimu
madaraka yake kwa kamati mbalimbali zitakazoundwa kwa mujibu wa
sheria itakayotungwa na Bunge.
(5) Bunge litatunga sheria itakayoweka masharti ya utekelezaji wa
majukumu ya Tume.
Uanachama
katika
vyama vya
siasa
174. Itakuwa ni marufuku kwa Jaji wa Mahakama ya Juu, Jaji wa
Mahakama ya Rufani au Msajili wa Mahakama ya ngazi yoyote kuwa
mwanachama wa chama chochote cha siasa, isipokuwa atakuwa na haki
ya kupiga kura ya kuchagua viongozi katika vyombo vya uwakilishi.
(b) Mfuko wa Mahakama
Mfuko wa
Mahakama
175.-(1) Kutakuwa na mfuko utakaojulikana kama Mfuko wa
Mahakama ya Jamhuri ya Muungano ambao utakuwa chini ya usimamizi
wa Mtendaji Mkuu wa Mahakama.
(2) Mfuko wa Mahakama ya Jamhuri ya Muungano utatumika kwa
ajili ya kugharamia shughuli za utawala na uendeshaji wa Mahakama ya
Jamhuri ya Muungano na shughuli zingine muhimu katika utekelezaji wa
majukumu ya Mahakama.
(3) Serikali itahakikisha kwamba katika kila bajeti ya mwaka wa
fedha wa Serikali, inatenga kwa kiwango kinachotosha fedha ambazo
zitaingizwa katika Mfuko wa Mahakama ya Jamhuri ya Muungano.
(4) Bunge litatunga sheria itakayoweka masharti kuhusu
uendeshaji wa Mfuko wa MahakamayaJamhuri ya Muungano.
SURA YA KUMI NA MOJA
UTUMISHI WA JAMHURI YA MUUNGANO
Misingi
mikuu ya
Utumishi
wa Umma
176.-(1) Utumishi wa umma katika Jamhuri ya Muungano
utazingatia misingi na kanuni zifuatazo:
(a) utumishi wa umma ni dhamana kutoka kwa wananchi na hivyo
mtumishi anatakiwa kutumikia wananchi kwa uadilifu,
‐ 69 ‐
uaminifu na unyenyekevu;
(b) kudumisha na kukuza viwango vya juu vya maadili ya
kitaaluma;
(c) kuhamasisha matumizi bora na yenye tija ya raslimali;
(d) kutoa huduma kwa umma kwa njia ya haki, usawa na bila
upendeleo;
(e) kuhamasisha wananchi kushiriki kwenye maandalizi ya sera
mbalimbali za nchi;
(f) kuitikia matakwa na mahitaji ya watu kwa haraka na kwa
wakati unaofaa;
(g) kujitolea katika utekelezaji wa sera na mipango ya kitaifa;
(h) uwajibikaji wa viongozi kwa makosa yanayofanyika chini yao;
(i) kuhamasisha sera ya uwazi katika kutoa habari za kweli kwa
umma na kwa wakati ufaao; na
(j) kuhakikisha kwamba watu watateuliwa katika nafasi
mbalimbali kwa kuzingatia uwezo wa kitaaluma, weledi,
maarifa, ujuzi na uzoefu wao katika eneo husika.
(2) Misingi na Kanuni za Utumishi wa Umma zilizoainishwa katika
Ibara hii zitazingatiwa na kutumika katika uteuzi wa kushika nafasi za
madaraka ya uongozi katika:
(a) mamlaka katika mihimili yote ya Dola;
(b) taasisi na idara zote za Serikali; na
(c) mashirika yote ya Serikali.
(3) Bunge litatunga sheria kuweka masharti ya utekelezaji wa
misingi ya utumishi iliyoainishwa katika Ibara ndogo ya (1).
Masharti
kuhusu
utumishi
katika
Jamhuri ya
Muungano
177. Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, utumishi wa umma na
uongozi katika Jamhuri ya Muungano utazingatia misingi kwamba utoaji wa
ajira na uteuzi wa viongozi utakuwa kwa uwiano baina ya Washirika wa
Muungano, kwa kuzingatia weledi na taaluma katika eneo au nyanja husika.
Tume ya
Utumishi
wa Umma
178.-(1) Kutakuwa na Tume ya Utumishi wa Umma itakayokuwa
na Mwenyekiti na wajumbe wengine sita watakaoteuliwa na Rais na
kuidhinishwa na Bunge.
(2) Katika kuteua wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Umma, Rais
atazingatia Kanuni za Utumishi wa Umma zilizoainishwa katika Katiba
hii.
(3) Kutakuwa na Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma ambaye
atakuwa ndiye Mtendaji Mkuu na mtekelezaji wa majukumu ya kila siku
ya Tume.
(4) Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma atateuliwa na Rais
baada ya kuidhinishwa na Bunge kutoka miongoni mwa watumishi
waandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
Mamlaka
na
Majukumu
ya Tume
179.-(1) Tume ya Utumishi wa Umma itakuwa ni chombo cha juu
katika Utumishi wa Umma chenye mamlaka ya kusimamia na kuratibu
mambo yote kuhusu Utumishi wa Umma.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), majukumu ya
‐ 70 ‐
Tume ya Utumishi wa Umma yatakuwa ni:
(a) kumshauri Rais juu ya uteuzi wa viongozi katika nafasi
mbalimbali kwa mujibu wa Katiba hii;
(b) kutoa miongozo mbalimbali na kusimamia mchakato wa ajira
katika utumishi wa umma kwa kuzingatia vigezo stahiki;
(c) bila kuathiri masharti ya Katiba hii, kuteua watu kuhudumu au
kushikilia ofisi kwa muda katika idara ya utumishi wa umma,
kuidhinisha uteuzi na kudhibiti nidhamu na kuwaondoa
watumishi wanaohudumu au kushikilia ofisi hizo;
(d) kusimamia na kuhamasisha utekelezaji wa misingi na kanuni za
utumishi katika sekta zote za utumishi wa umma;
(e) kushughulikia rufani zinazowasilishwa na watumishi wa umma
dhidi ya uamuzi wa mamlaka mbalimbali za nidhamu katika
utumishi wa umma;
(f) kutekeleza majukumu mengine yoyote kama
yatakavyoainishwa katika sheria itakayotungwa na Bunge juu
masuala ya utumishi wa umma na sheria nyingine za nchi;
(g) kuunda na kudurusu mishahara na marupurupu ya watumishi
wa umma, ikiwemo viongozi wa juu wa nchi, viongozi wa
kisiasa, watumishi waliopo chini ya utumishi wa Mahakama,
Bunge na Serikali; na
(h) kusawazisha mishahara na marupurupu ya maafisa wote wa
Serikali, Bunge, Mahakama na maofisa wa umma pamoja na
maofisa wa majeshi ya ulinzi na usalama.
SURA YA KUMI NA MBILI
UCHAGUZI KATIKA VYOMBO VYA UWAKILISHI
NA VYAMA VYA SIASA
SEHEMU YA KWANZA
UWAKILISHI WA WANANCHI
Ushiriki
katika
vyombo vya
uwakilishi
180.-(1) Kila raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
mwenye umri wa miaka kumi na nane au zaidi mwenye akili timamu
ana haki ya kupiga kura na haki ya kuandikishwa kwa ajili ya kupiga
kura katika uchaguzi au kura ya maoni.
(2) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (1), mamlaka ya
uchaguzi itazingatia misingi ifuatayo:
(a) wananchi wanatumia haki ya kisiasa kwa mujibu wa
Katiba hii;
(b) watu wenye ulemavu wanapewa fursa za uwakilishi;
(c) haki ya kila mtu kupiga kura moja kufuatana na utashi
wa uwakilishi na kura sawa; na
(d) uchaguzi ulio huru na ambao -
(i) ni wa kura ya siri;
(ii) hauna matumizi ya nguvu, vitisho, vishawishi
wala rushwa;
(iii) haukuwa na matamshi au vitendo vinavyoashiria
ukabila, ukanda, udini, dharau na kashfa kwa
‐ 71 ‐
jinsia au unyanyapaa kwa walemavu au makundi
madogo katika jamii;
(iv) unaendeshwa na kusimamiwa na chombo huru;
na
(v) unaendeshwa bila upendeleo au kuegemea
upande wowote, uliyo makini na inayoonyesha
uwajibikaji wa watendaji.
(3) Ili kutekeleza masharti ya Ibara ndogo ya (1) na (2),
mamlaka ya nchi itaweka utaratibu wa sheria utakaowezesha:
(a) mamlaka zinazosimamia uchaguzi kutangaza majimbo
kwa madhumuni ya uchaguzi wa wabunge;
(b) uteuzi wa wagombea;
(c) uandikishaji endelevu wa wapiga kura;
(d) kuendesha na kusimamia uchaguzi na kura ya maoni;
(e) kuweka utaratibu wa kuandikisha raia wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania wanaoishi nje ili kuweza
kupiga kura katika uchaguzi au kura ya maoni; na
(f) utaratibu wa kufanya uchaguzi kuwa mwepesi, wazi na
unaozingatia mahitaji ya watu wenye mahitaji maalum.
(4) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (2), kwa lengo la
kukuza demokrasia, kulinda Katiba na kuhakikisha panakuwepo
uchaguzi huru, kila mpiga kura ana haki ya kufungua shauri
Mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi isipokuwa matokeo ya
uchaguzi wa Rais,anayoamini yamevunja au kukiuka masharti ya
Katiba hii.
SEHEMU YA PILI
TUME HURU YA UCHAGUZI
(a) Muundo wa Tume Huru ya Uchaguzi na Vyama vya
Siasa
Kuundwa
kwa Tume
Huru ya
Uchaguzi
181.-(1) Kutakuwa na Tume Huru ya Uchaguzi ya Jamhuri ya
Muungano kwa ajili ya kusimamia na kuratibu shughuli za uchaguzi na
masuala yanayohusu vyama vya siasa na ambayo pia itaitwa “Tume
Huru ya Uchaguzi”.
(2) Tume Huru ya Uchaguzi itaundwa na Mwenyekiti, Makamu
Mwenyekiti na wajumbe wengine saba watakaoteuliwa na Rais baada ya
kupendekezwa na Kamati ya Uteuzi.
(3) Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe wa Tume
Huru ya Uchaguzi watashika madaraka mara baada ya kuthibitishwa na
Bunge.
(4) Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi
watakuwa na sifa zifuatazo:
(a) awe ni raia wa kuzaliwa na angalau mmoja kati ya wazazi
wake ni raia wa kuzaliwa wa Tanzania;
(b) awe ni mtu aliyewahi kushika wadhifa wa Jaji wa Makakama
ya Juu, Mahakama ya Rufani au Mahakama Kuu na ameshika
‐ 72 ‐
wadhifa huo kwa kipindi kisichopungua miaka mitano;
(c) awe ni mtu mwaminifu, mwadilifu, na mwenye mwenendo
usiotiliwa shaka na jamii;
(d) awe ni mtu ambaye siyo kiongozi, hajawahi kushika wadhifa
wowote wa kisiasa katika chama chochote cha kisiasa; na
(e) awe ni mtu ambaye hajawahi kutiwa hatiani kwa kosa lolote
la jinai linalohusiana na uaminifu.
(5) Mjumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi atakuwa na sifa
zifuatazo:
(a) awe ni raia wa kuzaliwa na angalau mmoja kati ya wazazi
wake ni raia wa kuzaliwa wa Tanzania;
(b) awe ni mtu mwaminifu, mwadilifu, na mwenye mwenendo
usiotiliwa shaka na jamii;
(c) awe ni mtu ambaye siyo kiongozi na hajawahi kushika
wadhifa wowote wa kisiasa katika chama chochote cha
kisiasa;
(d) awe na elimu ya shahada ya chuo kikuu kinachotambuliwa
kwa mujibu wa sheria za nchi; na
(e) awe ni mtu ambaye hajawahi kutiwa hatiani kwa kosa lolote
la jinai linalohusu kukosa uaminifu.
(6) Kwa madhumuni ya Ibarahii, watu wafuatao hawatakuwa na
sifa ya kuwa Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi:
(a) Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Mbunge wa
Bunge la Tanzania Bara, Mwakilishi wa Baraza la
Wawakilishi, Diwani au Sheha katika Serikali ya Tanzania
Bara au Zanzibar mtawalia;
(b) mtu ambaye ni mtumishi wa umma; au
(c) mtu ambaye anashika nafasi ya madaraka katika asasi zisizo
za kiserikali au aliyewahi kushika nafasi ya madaraka katika
asasi zisizo za kiserikali ndani ya muda usiozidi miaka mitano
kabla ya uteuzi kufanyika.
(7) Uteuzi wa Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi utazingatia
uwakilishi na uwiano wa Washirika wa Muungano.
Kamati ya
Uteuzi
182.-(1) Kutakuwa na Kamati ya Uteuzi wa Mwenyekiti,
Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi
itakayokuwa na muundo ufuatao:
(a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ambaye atakuwa ni
Mwenyekiti;
(b) Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano ambaye
atakuwa Makamu Mwenyekiti;
(c) Spika wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar;
(d) Spika wa Bunge la Tanzania Bara;
(e) Jaji Mkuu wa Tanzania Bara;
(f) Jaji Mkuu wa Zanzibar; na
(g) Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu.
(2) Mkurugenzi wa Tume Huru ya Uchaguzi atakuwa Katibu wa
‐ 73 ‐
Kamati ya Uteuzi.
(3) Kamati ya Uteuzi itakuwa na jukumu la kupokea na
kuchambua majina ya watu walioomba kuwa wajumbe wa Tume Huru
ya Uchaguzi kwa mujibu wa utaratibu utakaoainishwa na sheria
iliyotungwa na Bunge.
(4) Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ndogo ya (3), Kamati ya
Uteuzi mara baada ya kuchambua majina ya watu walioomba kuwa
wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi, itapendekeza kwa Rais majina ya
watu wanaofaa kuteuliwa kuwa wajumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.
(5) Rais atateua Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe
wa Tume Huru ya Uchaguzi kutoka miongoni mwa majina
yaliyowasilishwa na Kamati ya Uteuzi na atawasilisha majina hayo
Bungeni kwa ajili ya kuthibitishwa na Bunge.
(6) Bunge litatunga Sheria ambayo pamoja na mambo na
mengine itaweka masharti kuhusu kiapo cha Mwenyekiti, Makamu
Mwenyekiti na Wajumbe wengine wa Tume Huru ya Uchaguzi.
Ukomo wa
kushika
madaraka ya
Tume Huru
ya Uchaguzi
183.-(1) Mjumbe wa Tume atashika madaraka kwa kipindi cha
miaka mitano na anaweza kuteuliwa tena kwa kipindi kingine kimoja cha
miaka mitano.
(2) Mtu atakoma kuwa mjumbe wa Tume endapo litatokea tukio
lolote kati ya matukio yafuatayo:
(a) kifo;
(b) kujiuzulu;
(c) kutokuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa
sababu za kiafya;
(d) kuondolewa kwa makosa ya kukiuka Kanuni za Maadili ya
Uongozi wa Umma;
(e) kutiwa hatiani kwa kosa ambalo adhabu yake ni kifungo
gerezani kwa muda unaozidi siku saba; au
(f) kupoteza sifa ya kuteuliwa kuwa mjumbe.
(2) Kwa madhumuni ya utekelezaji bora wa majukumu ya Tume,
kutakuwa na kanuni za maadili kama zitakazoainishwa na Sheria
itakayotungwa na Bunge.
(3) Mjumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi ambaye atakiuka
masharti ya Kanuni za Maadili ya Tume atapoteza sifa za kuendelea
kuwa mjumbe.
(4) Endapo suala la kumuondoa Mjumbe wa Tume Huru ya
Uchaguzi kwa kukiuka Kanuni za Maadili ya Uongozi wa Umma
litajitokeza, Rais atateua Kamati itakayoundwa na:
(a) Jaji wa Mahakama ya Rufani ambaye atakuwa Mwenyekiti;
(b) Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora;
(c) Mjumbe wa Tume ya Maadili na Uwajibikaji; na
(d) Mawakili, mmoja kutoka Tanzania Bara na mmoja kutoka
Zanzibar watakaopendekezwa na Chama cha Wanasheria
Tanganyika na Chama cha Wanasheria Zanzibar,
na Kamati hiyo itafanya uchunguzi wa suala hilo na kisha kutoa
‐ 74 ‐
mapendekezo kwa Rais.
(5) Endapo, baada ya uchunguzi,Kamati itapendekeza kuwa
mjumbe huyo asiondolewe, suala la kumuondoa mjumbe huyo litasita.
(6) Kamati itaweka utaratibu wa kufanya uchunguzi.
Wajibu wa
Tume Huru
ya Uchaguzi
184.-(1) Tume Huru ya Uchaguzi itakuwa na wajibu wa:
(a) kusimamia na kuendesha shughuli zote za uchaguzi wa
Wabunge na Rais katika Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania;
(b) kusimamia na kuendesha kura ya maoni;
(c) kusimamia na kuratibu uandikishaji wa wapiga kura katika
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
(d) kusimamia na kuratibu uandikishaji na shughuli za vyama
vya siasa kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii na sheria za
nchi;
(e) kutayarisha na kuchapisha ripoti za kila mwaka kuhusu ripoti
za ukaguzi wa fedha wa kila chama cha kisiasa; na
(f) kusimamia fedha za ruzuku za Vyama vya Kisiasa.
(2) Tume Huru ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano itakuwa
pia na wajibu wa kutoa elimu kwa wapiga kura katika uchaguzi au kura
ya maoni na kuratibu na kusimamia wananchi, asasi za kiraia, taasisi,
jumuiya au makundi ya watu yatakaotoa elimu hiyo.
(3) Tume Huru ya Uchaguzi pia ina wajibu wa kuhakikisha
kuwepo kwa:
(a) uhuru wa wananchi katika kutumia haki ya uchaguzi na
kuchaguliwa kupitia vyama vya siasa au mgombea huru;
(b) uwakilishi unaozingatia jinsia;
(c) uwakilishi wa watu wenye ulemavu au mahitaji maalumu
katika jamii;
(d) uzingatiaji wa misingi ya upigaji kura wa mtu mmoja kura
moja kwa kuzingatia uwakilishi wenye usawa; na
(e) uhuru wa uchaguzi wa haki.
(4) Tume Huru ya Uchaguzi inaweza kutekeleza shughuli zake
bila kujali kwamba kuna nafasi ya madaraka ya mjumbe iliyo wazi
miongoni mwa wajumbe au kwamba Mjumbe mmojawapo hayupo,
lakini kila uamuzi wa Tume Huru ya Uchaguzi ni lazima uungwe mkono
na wajumbe walio wengi kati ya Wajumbe wote wa Tume Huru ya
Uchaguzi.
(5) Katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya
Katiba hii, Tume ya Uchaguzi haitalazimika kufuata amri au maagizo ya
mtu yeyote au idara yoyote ya Serikali, au maoni ya chama chochote cha
siasa.
(6) Katika utekelezaji wa madaraka yake kwa mujibu wa Katiba
hii, Tume Huru ya Uchaguzi itashauriana mara kwa mara na Tume ya
Uchaguzi ya Tanzania Bara na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar.
(7) Itakuwa ni marufuku kwa watu wanaohusika na uchaguzi
kujiunga na chama chochote cha siasa, isipokuwa tu kwamba kila mmoja
wao atakuwa na haki ya kupiga kura kuchagua wajumbe katika vyombo
‐ 75 ‐
vya uwakilishi.
(8) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (8), watu wanaohusika na
uchaguzi ni-
(a) Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi;
(b) Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi;
(c) Wajumbe wote wa Tume Huru ya Uchaguzi;
(d) Mkurugenzi wa Uchaguzi pamoja na watumishi wote wa
Tume Huru ya Uchaguzi;
(e) Msajili wa Vyama vya Siasa; na
(f) Wasimamizi wote wa Uchaguzi.
Malalamiko
kuhusu
uchaguzi
185.-(1) Tume Huru ya Uchaguzi itasimamia na kutatua mapema
iwezekanavyo malalamiko yanayohusu kuteuliwa kwa mgombea katika
uchaguzi.
(2) Kesi za malalamiko kuhusu uchaguzi wa Wabunge
zitafunguliwa Mahakama ya Rufaa mapema iwezekanavyo baada ya
Tume Huru ya Uchaguzi kutangaza matokeo na kwa vyovyote vile si
zaidi ya muda ulioainishwa katika sheria za nchi.
(3) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (2) shauri la malalamiko
kuhusu uchaguzi wa Mbunge itasikilizwa na Jaji mmoja wa Mahakama
ya Rufani.
(b) Vyama vya Siasa
Vyama vya
siasa
186.-(1) Jamhuri ya Muungano ni nchi ya kidemokrasia yenye
kufuata mfumo wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa.
(2) Bila ya kujali masharti ya Ibara ndogo ya (1), haitakuwa halali
kwa chombo chochote cha siasa kuandikishwa ambacho kutokana na
Katiba au sera yake-
(a) kinakusudia kukuza au kupigania maslahi ya-
(i) imani au kundi lolote la dini;
(ii) kundi lolote la kikabila, pahala watu watokeapo, rangi au
jinsia;
(iii)eneo fulani tu katika sehemu yoyote ya Jamhuri ya
Muungano;
(b) kinapigania kuvunjwa kwa Jamhuri ya Muungano:
(c) kinakubali au kupigania matumizi ya nguvu au mapambano
kama njia za kufikia malengo yake ya kisiasa;
(d) kinapigania au kinakusudia kuendesha shughuli zake za
kisiasa katika sehemu moja tu ya Jamhuri ya Muungano; au
(e) hakiruhusu uongozi wake kuchaguliwa kwa vipindi na kwa
njia za kidemokrasia.
(3) Bila ya kuathiri sheria za nchi zinazohusika ni marufuku kwa
mtu yeyote kulazimishwa kujiunga na chama chochote au kwa chama
cha siasa kukataliwa kusajiliwa kwa sababu tu ya itikadi au falsafa.
(4) Bunge linaweza kutunga sheria inayoweka masharti
yatakayohakikisha kuwa vyama vya siasa vinazingatia mipaka na vigezo
vilivyowekwa na masharti ya Ibara ndogo ya (2) kuhusu uhuru na haki
ya watu kushirikiana na kujumuika.
(5) Mambo yote yanayohusu uandikishaji na uendeshaji wa
‐ 76 ‐
vyama vya siasa nchini yatasimamiwa kwa mujibu wa masharti ya
Katiba hii na sheria iliyotungwa na Bunge kwa ajili hiyo.
(c) Mkurugenzi wa Uchaguzi na Msajili wa Vyama vya Siasa
Utekelezaji
wa
majukumu
ya Tume
Huru ya
Uchaguzi
187.-(1) Kwa madhumuni ya utekekelezaji wa majukumu yake,
Tume Huru ya Uchaguzi itagawanywa katika sehemu kuu mbili, sehemu
ya uchaguzi na sehemu ya usajili wa vyama vya siasa.
(2) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (1), kutakuwa na:
(a) Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye atakuwa ndiye msimamizi
na mtekelezaji mkuu wa majukumu ya kila siku ya Tume
Huru ya Uchaguzi kuhusiana na masuala ya uchaguzi,
uandikishaji wa wapiga kura na uendeshaji wa kura ya maoni;
na
(b) Msajili wa Vyama vya Siasa ambaye atakuwa ndiye
msimamizi na mtekelezaji mkuu wa majukumu ya Tume
kuhusiana na usajili na usimamizi wa shughuli za vyama vya
siasa.
(3) Mkurugenzi wa Uchaguzi na Msajili wa Vyama vya Siasa
watatekeleza majukumu yao kwa kufuata utaratibu ulioainishwa na
sheria za nchi kuhusu masuala ya uchaguzi na vyama vya siasa.
(4) Mkurugenzi wa Uchaguzi na Msajili wa Vyama vya Siasa
watatekeleza majukumu yao kwa kusaidiwa na watendaji ambao ni
watumishi wa umma kwa kadri ya idadi inayohitajika.
(5) Uteuzi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi na Msajili wa Vyama
vya Siasa utafanywa na Rais baada ya kuthibitishwa na Bunge.
(6) Katika kutekeleza majukumu yao, Mkurugenzi wa Uchaguzi
na Msajili wa Vyama vya Siasa watawajibika kwa Tume Huru ya
Uchaguzi.
SURA YA KUMI NA TATU
TAASISI ZA UWAJIBIKAJI
SEHEMU YA KWANZA
TUME YA MAADILI YA UONGOZI NA UWAJIBIKAJI
Tume ya
Maadili ya
Uongozi na
Uwajibikaji
188.-(1) Kutakuwa na Tume ambayo itaitwa Tume ya Maadili ya
Uongozi na Uwajibikaji itayoundwa na Mwenyekiti na Makamu
Mwenyekiti na wajumbe wengine wasiozidi saba.
(2) Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya
Uongozi na Uwajibikaji watateuliwa na Rais baada ya kupendekezwa na
Tume ya Utumishi wa Umma.
(3) Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti watashika madaraka
yao baada ya kuthibitishwa na Bunge.
(4) Sifa za Mwenyekiti wa Tume zitakuwa kama ifuatavyo:
(a) awe raia;
(b) mtu mwenye shahada ya chuo kikuu kinachotambulika kwa
mujibu wa sheria za nchi;
‐ 77 ‐
(c) mtu mwenye uzoefu katika utumishi wa umma kwa kipindi
kisichopungua miaka kumi; na
(d) mtu mwenye heshima, weledi uaminifu, uadilifu na asiye na
tabia au mienendo yenye kutiliwa shaka.
(5) Sifa za Makamu Mwenyekiti zitakuwa kama inavyoainishwa
katika Ibara ndogo ya (4).
Majukumu
ya jumla ya
Tume
189.-(1) Majukumu ya jumla ya Tume ya Maadili ya Uongozi na
Uwajibikaji yatakuwa ni kufuatilia na kuchunguza tabia na mwenendo
wa viongozi na watumishi wa umma kwa madhumuni ya kusimamia na
kuhakikisha kuwa Maadili ya Uongozi wa Umma na Miiko ya Uongozi
wa Umma inazingatiwa, inalindwa na kuheshimiwa katika utumishi wa
Serikali, Bunge, Mahakama, taasisi na idara nyingine zote za umma.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya jumla ya Ibara ndogo ya (1),
majukumu mahsusi ya Tume yatakuwa ni:
(a) kusimamia maadili na uwajibikaji katika utumishi wa umma;
(b) kufanya upekuzi na kufuatilia kumbukumbu za wanaoomba
nafasi za uongozi wa umma;
(c) kuchunguza tabia na mwenendo wa mtumishi au kiongozi wa
umma na kuchukua hatua pale inapostahili, ikiwa ni pamoja
na kuwafikisha watumishi watakaobainika, kuvunja maadili
na miiko ya kazi katika vyombo vya sheria;
(d) kusimamia sheria itakayotungwa na Bunge kuhusu maadili na
uwajibikaji wa viongozi na watumishi wa umma;
(e) kushughulikia masuala ya ubadhirifu wa fedha na mali za
umma;
(f) kufanya uchambuzi yakinifu kwa viongozi wa umma
wanaopewa dhamana kabla ya kuingia madarakani;
(g) kutoa elimu ya maadili kwa umma kuhusu miiko na maadili
ya viongozi wa umma;
(h) kufanya uchunguzi kwa maamuzi yake yenyewe, au baada ya
kupokea malalamiko kutoka kwa mtu yeyote, kutokana na
kutenda au kutokutenda kwa Kiongozi au mtumishi yeyote
wa umma, au wakala wa Serikali, ikiwa kitendo
kilichotendwa au kutokutendwa ni kinyume cha maadili ya
umma;
(i) kumuelekeza, baada ya kupata malalamiko au itapoona
inafaa, kiongozi au mtumishi wa umma au wakala wa Serikali
au chombo chochote cha umma kufanya tendo lolote au
jambo lolote linalotakiwa na sheria, au kuacha, kuzuia au
kusahihisha utendaji mbaya au usiosahihi wa majukumu
yake;
(j) kutoa maelekezo kuhusu kuchukuliwa hatua kiongozi au
mtumishi yeyote wa umma;
(k) kumuelekeza kiongozi au mtumishi wa umma, kwa mujibu
wa sheria, kutoa nyaraka zinazohusiana na matumizi ya ofisi,
matumizi ya fedha au mali za umma, au kutoa taarifa ya
matumizi mabaya kwa Tume, kwa hatua stahiki.
(l) kuomba msaada au taarifa muhimu kutoka kwa mamlaka
‐ 78 ‐
yoyote ya Serikali au binafsi katika kutekeleza wajibu wake,
na kukagua, kama ni lazima, kumbukumbu muhimu na
nyaraka husika;
(m) kwa kuzingatia sheria, kutangaza kwa umma, mambo yote
yanayohusiana na uchunguzi iliyoufanya, iwapo mazingira
yanaruhusu;
(n) kuchunguza jambo au mazingira yoyote yanayokiuka au
kusababisha ukiukaji wa maadili; na
(o) kuandaa kanuni za taratibu na matumizi ya mamlaka au
utekelezaji wa kazi na majukumu ya Tume kama
itakavyoelekezwa na sheria.
Muda wa
kukaa
madarakani
kwa
Wajumbe
wa Tume
190.Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume
watakaa madarakani kwa vipindi viwili tu vya miaka mitatu kila kimoja,
ikizingatiwa kwamba uteuzi wa wajumbe wa Tume utafanywa kwa
namna ambayo Wajumbe wa Tume hawataanza au kumaliza muda wao
kwa wakati mmoja.
Kuondolewa
madarakani
kwa
Wajumbe
wa Tume
191.-(1) Mwenyekiti wa Tume au mjumbe yeyote wa Tume
anaweza kuondolewa madarakani kwa:
(a) kutokuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake kwa
sababu za kiafya kutokana na matatizo ya akili au kimwili;
(b) kukiuka Kanuni za Maadili ya Viongozi wa Umma;
(c) kukiuka Miiko ya Uongozi;
(d) kukosa weledi; au
(e) utovu wa nidhamu.
(2) Mwenyekiti au mjumbe wa Tume anaweza kuondolewa
madarakani kutokana na mapendekezo ya Tume ya Utumishi wa Umma
au kwa maombi ya mtu yeyote kwa Tume ya Utumishi wa Umma, kwa
masharti kwamba:
(a) maombi hayo yawe ya maandishi; na
(b) yaainishe masuala yanayolalamikiwa.
(3) Baada ya kupokea maombi hayo au endapo malalamiko
yametolewa na Tume yenyewe, Tume itaunda Kamati Maalum
itakayofanya uchunguzi kuhusu malalamiko hayo.
(4) Masuala ya Kamati Maalum yanayohusu:
(a) idadi ya wajumbe;
(b) sifa za wajumbe; na
(c) muda wa kufanya kazi,
yatakuwa kama itakavyoamuliwa na Tume.
(5) Baada ya kupokea taarifa yenye mapendekezo ya Kamati
Maalum, Tume itapeleka mapendekezo ya Kamati Maalum kwa Rais
kwa uamuzi.
Uhuru wa
Tume
192.-(1) Tume itakuwa huru na kwa mantiki hiyo haitaingiliwa na
mtu au mamlaka yoyote katika utekelezaji wa majukumu yake.
(2) Bunge litatunga sheria itakayoweka masharti kuhusu:
‐ 79 ‐
(a) utaratibu wa utekelezaji wa majukumu ya Tume;
(b) utayarishaji na utoaji wa taarifa za Tume;
(c) utaratibu wa utoaji wa mapendekezo na maamuzi ya Tume;
(d) watumishi wa Tume; na
(e) masuala mengine muhimu yanayoihusu Tume.
Uwezeshaji
wa nyenzo
na rasilimali
193. Serikali itahakikisha kuwa Tume ya Maadili ya Uongozi na
Uwajibikaji inapatiwa fedha, nyenzo na rasilimali watu ya kutosha kadri
hali itakavyoruhusu ili kutekeleza kazi na wajibu wake kwa ufanisi.
SEHEMU YA PILI
TUME YA HAKI ZA BINADAMU
Tume ya
Haki za
Binadamu
194.-(1) Kutakuwa na tume itakayoitwa Tume ya Haki za
Binadamu itakayoundwa na Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na
Wajumbewasiozidi saba.
(2) Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za
Binadamu watateuliwa na Rais baada ya kupendekezwa na Tume ya
Utumishi wa Umma.
(3) Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti watashika madaraka yao
baada ya kuthibitishwa na Bunge.
(4) Sifa za Mwenyekiti wa Tume zitakuwa kama ifuatavyo:
(a) awe raia;
(b) mtu mwenye shahada ya sheria;
(c) mtu mwenye uzoefu wa utumishi wa umma kwa kipindi
kisichopungua miaka kumi; na
(d) mtu mwenye heshima,weledi uaminifu, uadilifu na asiye na
tabia au mwenendo wenye kutiliwa shaka na jamii.
(5) Sifa za Makamu Mwenyekiti zitakuwa kama zilivyoainishwa
katika Ibara ndogo ya (4).
Kazi na
majukumu
ya Tume
195. Kazi na majukumu ya Tume ya Haki za Binadamu
yatakuwa kama ifuatavyo:
(a) kuhamasisha hifadhi ya haki za binadamu na wajibu kwa
jamii kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi;
(b) kupokea malalamiko juu ya uvunjaji wa haki za binadamu
kwa ujumla;
(c) kuchunguza uvunjaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa
misingi ya utawala bora;
(d) kufanya utafiti na kutoa elimu kwa umma kuhusu haki za
binadamu na utawala bora;
(e) kufungua mashauri Mahakamani ili kuzuia vitendo vya
uvunjaji wa haki za binadamu au kurekebisha haki
inayotokana na uvunjwaji huo wa haki za binadamu au
ukiukwaji wa misingi ya utawala bora;
(f) kuchunguza mwenendo wa mtu yeyote anayehusika au
taasisi yeyote inayohusika na masharti ya Ibara hii katika
utekelezaji wa kawaida wa madaraka ya kazi au majukumu
‐ 80 ‐
yake au utekelezaji unaokiuka madaraka hayo;
(g) kutoa ushauri kwa Serikali na vyombo vingine vya umma na
vya sekta binafsi kuhusu haki za binadamu na utawala bora;
na
(h) kuchukua hatua zinazostahiki kwa ajili ya kukuza na
kuendeleza usuluhishi na suluhu miongoni mwa watu na
taasisi mbalimbali wanaofika au kufikishwa mbele ya Tume.
Muda wa
kukaa
madarakani
kwa
Wajumbe
wa Tume
196. Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Tume
watakaa madarakani kwa vipindi viwili tu vya miaka mitatu kila kimoja,
ikizingatiwa kwamba uteuzi wa wajumbe wa Tume utafanywa kwa
namna ambayo Wajumbe wa Tume hawataanza au kumaliza muda wao
kwa wakati mmoja.
Kuondolewa
madarakani
kwa
Wajumbe wa
Tume
197.-(1) Mwenyekiti na Makamu wa Mwenyekiti wa Tume au
mjumbe yeyote wa Tume anaweza kuondolewa madarakani kwa:
(a) kutokuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake kutokana
na matatizo ya akili au kimwili;
(b) kukiuka kanuni za maadili ya Viongozi wa Umma;
(c) kukiuka Miiko ya Uongozi;
(d) kukosa weledi; na
(e) utovu wa nidhamu.
(2) Mwenyekiti, Makamu wa Mwenyekiti au mjumbe wa Tume
anaweza kundolewa madarakani kutokana na mapendekezo ya Tume ya
Utumishi wa Umma au kwa maombi ya mtu yeyote kwa Tume ya
Utumishi wa Umma, ambapo:
(a) maombi hayo yawe ya maandishi; na
(b) yaainishe masuala yanayolalamikiwa.
(3) Baada ya kupokea maombi hayo au endapo malalamiko
yametolewa na Tume yenyewe, Tume itaunda Kamati Maalum
itakayofanya uchunguzi kuhusu malalamiko hayo.
(4) Masuala yanayohusu:
(a) idadi ya wajumbe;
(b) sifa za wajumbe; na
(c) muda wa kufanya kazi za Kamati Maalum,
yatakuwa kama itakavyoamuliwa na Tume.
(5) Baada ya kupokea ripoti ya Kamati Maalum, Tume itapeleka
mapendekezo ya Kamati Maalum kwa Rais kwa uamuzi.
Uhuru wa
Tume
198.-(1) Tume itakuwa huru; na kwa mantiki hiyo, haitaingiliwa
na mtu au mamlaka yoyote katika utekelezaji wa majukumu yake.
(2) Bunge litatunga sheria itakayoweka masharti kuhusu:
(a) utaratibu wa utekelezaji wa majukumu ya Tume;
(b) utayarishaji na utoaji wa taarifa za Tume;
(c) utaratibu wa utoaji wa mapendekezo na maamuzi ya Tume;
‐ 81 ‐
(d) watumishi wa Tume; na
(e) masuala mengine muhimu yanayoihusu Tume.
Uwezeshaji
wa nyenzo
na rasilimali
199. Serikali itahakikisha kuwa Tume ya Haki za Binadamu
inapatiwa fedha, nyenzo na rasilimali watu ya kutosha kadri hali
itakavyoruhusu ili kutekeleza kazi na wajibu wake kwa ufanisi.
SEHEMU YA TATU
MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI
Uteuzi wa
Mdhibiti na
Mkaguzi
Mkuu wa
Hesabu za
Serikali
200.-(1) Kutakuwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali ambaye atateuliwa na Rais baada ya kupendekezwa na Tume ya
Utumishi wa Umma.
(2) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Serikali
atashika wadhifa huo mara tu baada ya kuthibitishwa na Bunge la
Jamhuri ya Muungano.
Sifa za
Mdhibiti na
Mkaguzi
Mkuu wa
Hesabu za
Serikali
201. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
atateuliwa kutoka miongoni mwa watumishi wa umma wenye sifa
zifuatazo:
(a) aweamefuzu mafunzo ya juu ya uhasibu na kusajiliwa na
mamlaka husika;
(b) ana uzoefu usiyopungua miaka kumi na tano katika utumishi
wa umma;
(c) ana uzoefu usiyopungua miaka kumi na tano katika masuala
yanayohusu ukaguzi wa hesabu za Serikali; na
(d) ni mtu mwenye heshima, weledi, uaminifu, uadilifu na asiye
na upendeleo unaotiliwa shaka na jamii.
Kazi na
majukumu
yake
202.-(1) Kazi na majukumu ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
Hesabu za Serikali yatakuwa ni:
(a) kuhakikisha kwamba fedha zozote zinazokusudiwa kutolewa
kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali matumizi yake
yameidhinishwa na kwamba zitatolewa kwa mujibu wa
masharti ya Katiba hii, na iwapo atatosheka kwamba masharti
hayo yatatekelezwa ipasavyo, basi ataidhinisha fedha hizo
zitolewe;
(b) kuhakikisha kwamba fedha zote ambazo matumizi yake
yameidhinishwa yatokane na fedha zilizomo katika Mfuko
Mkuu wa Hazina ya Serikali au fedha ambazo matumizi yake
yameidhinishwa na sheria iliyotungwa na Bunge, na
kwambazimetumika kwa ajili ya shughuli zilizohusika na
matumizi ya fedha hizo na matumizi hayo yamefanywa kwa
kufuata idhini iliyotolewa kuhusu matumizi hayo;
(c) angalau, mara moja kila mwaka, kufanya ukaguzi na kutoa
taarifa juu ya ukaguzi wa hesabu za Serikali ya Jamhuri ya
Muungano, hesabu zinazosimamiwa na watumishi wote wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano na hesabu za Mahakama
zote za Jamhuri ya Muungano na zinazosimamiwa na Katibu
‐ 82 ‐
wa Bunge; na
(d) kutayarisha ripoti ya mwaka na kuiwasilisha Bungeni kwa
ajili ya kujadiliwa na kutolewa mapendekezo.
(2) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali atakuwa
huru katika utekelezaji wa kazi na majukumu yake, na kwa mantiki hiyo,
hataingiliwa na mtu au mamlaka yoyote katika utekelezaji wa kazi zake.
(3) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na kila
mtumishi wa Serikali aliyeruhusiwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
wa Hesabu za Serikali atakuwa na haki ya kuchunguza vitabu,
kumbukumbu, hati nyinginezo zote zinazohusika na hesabu za aina
yoyote iliyotajwa katika ibara ndogo ya (2) ya Ibara hii.
(4) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
atawasilisha kwa Rais kila taarifa atakayotoa kwa mujibu wa masharti
ya Katiba hii.
(5) Baada ya kupokea taarifa hiyo, Rais atawaagiza watu
wanaohusika wawasilishe taarifa hiyo kwenye kikao cha kwanza cha
Bunge kitakachofanyika baada ya Rais kupokea taarifa hiyo na itabidi
iwasilishwe katika kikao hicho kabla ya kupita siku saba tangu siku ile
ulipoanza Mkutano huo, na iwapo Rais hatachukua hatua za kuwasilisha
taarifa hiyo kwa Spika wa Bunge, basi Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu
za Serikali atawasilisha taarifa hiyo kwa Spika wa Bunge au kwa Naibu
Spika iwapo nafasi ya madaraka ya Spika iko wazi,ambaye atawasilisha
taarifa hiyo kwa Bunge.
(6) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali atakuwa
pia na jukumu la kutekeleza kazi na shughuli nyingine, na atakuwa na
madaraka mengine ya namna mbalimbali, kama itakavyoelezwa na sheria
kuhusu hesabu za Serikali ya Jamhuri ya Muungano au hesabu za
vyombo vya umma au hesabu za mashirika.
(7) Katika kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti
ya ibara ndogo ya (1), (3), (4) na (5) ya Ibara hii, Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu za Serikali hatalazimika kufuata amri au maagizo ya
mtu mwingine yeyote au idara yoyote ya Serikali,lakini maelezo hayo
ya ibara hii ndogo hayataizuia Mahakama nayo kutumia madaraka yake
kwa ajili ya kuchunguza kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
za Serikali ametekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya
Katiba hii au sivyo.
(8) Bunge linaweza kutunga sheria itakayosimamia, pamoja na
mambo mengine, matumizi ya mamlaka ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
wa Hesabu za Serikali.
Muda wa
kukaa
madarakani
203.-(1) Muda wa kukaa madarakani kwa Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu za Serikali itakuwa ni kipindi kimoja cha miaka saba
mfululizo.
(2) Bila ya kujali masharti ya ibara ndogo ya (1), Mdhibiti na
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali anaweza kujiuzulu wadhifa wake
kwa kutoa taarifa ya siku thelathini kwa Rais.
Kuondolewa
madarakani 204.-(1) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
anaweza kuondolewa madarakani kwa:
‐ 83 ‐
(a) kutokuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake kutokana
na matatizo ya afya ya akili au kimwili;
(b) kukiuka kanuni za Maadili ya Uongozi wa Umma;
(c) kukiuka Miiko ya Uongozi wa Umma;
(d) kukosa weledi; na
(e) utovu wa nidhamu.
(2) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali anaweza
kuondolewa madarakani kutokana na mapendekezo ya Tume ya
Utumishi wa Umma au kwa maombi ya mtu yeyote kwa Tume ya
Utumishi wa Umma, ambapo:
(a) maombi hayo yawe ya maandishi; na
(b) yaainishe masuala yanayolalamikiwa.
(3) Baada ya kupokea maombi hayo au endapo malalamiko
yametolewa na Tume yenyewe, Tume itaunda Kamati Maalum
itakayofanya uchunguzi kuhusu malalamiko hayo.
(4) Masuala yanayohusu:
(a) idadi ya wajumbe;
(b) sifa za wajumbe; na
(c) muda wa kufanya kazi za Kamati,
yatakuwa kama itakavyoamuliwa na Tume.
(5) Baada ya kupokea ripoti ya Kamati Maalum, Tume itapeleka
mapendekezo ya Kamati Maalum kwa Rais kwa uamuzi.
Uwezeshaji
wa nyenzo
na rasilimali
205. Serikali itahakikisha kuwa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu za Serikali inapatiwa fedha, nyenzo na rasilimali watu
ya kutosha ili kulinda uhuru wake katika kutekeleza kazi na majukumu
yake kwa ufanisi.
SURA YA KUMI NA NNE
MASHARTI KUHUSU FEDHA ZA JAMHURI YA MUUNGANO
(a) Mfuko Mkuu wa Hazina na Fedha za
Jamhuri ya Muungano
Mfuko
Mkuu wa
Hazina ya
Serikali ya
Jamhuri ya
Muungano
206. Kutakuwa na Mfuko Mkuu wa Hazina wa Serikali ya Jamhuri
ya Muungano utakaoitwa “Mfuko Mkuu wa Hazina” ambamo fedha zote
zitakazopatikana kwa njia mbalimbali zitawekwa, isipokuwa:
(a) fedha ambazo zimetajwa katika Sheria kuwa zitumike kwa
shughuli maalum au ziwekwe katika mfuko mwingine kwa ajili ya
matumizi maalum; au
(b) fedha ambazo kwa mujibu wa sheria, taasisi za Serikali
zimeruhusiwa kukusanya na kubaki nazo kwa ajili ya kugharamia
uendeshaji wa taasisi hizo.
Masharti ya
kutoa fedha
za matumizi
katika
Mfuko
Mkuu wa
Hazina ya
207.-(1) Fedha zinaweza kutolewa kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina
ya Serikali kwa ajili ya matumizi kwa kuzingatia masharti yafuatayo:
(a) fedha hizo ziwe kwa ajili ya matumizi ambayo
yameidhinishwa kuwa yatokane na fedha zilizomo katika
Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali na idhini hiyo iwe
‐ 84 ‐
Serikali. imetolewa na Katiba hii au sheria nyingine yoyote; na
(b) fedha hizo ziwe kwa ajili ya matumizi ambayo
yameidhinishwa ama na Sheria ya Matumizi ya Serikali
iliyotungwa mahsusi na Bunge au sheria nyingine yoyote
iliyotungwa na Bunge.
(2) Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ndogo ya (1), fedha zilizomo
katika Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali zitatolewa kutoka Mfuko huo
kwa ajili ya matumizi kwa kuzingatia masharti kuwa matumizi hayo yawe
yameidhinishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.
(3) Fedha zilizomo katika mfuko Maalum wowote wa Serikali,
isipokuwa Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali, hazitatolewa kutoka mfuko
huo kwa ajili ya matumizi isipokuwa kwa mujibu wa Sheria inayoidhinisha
matumizi hayo.
Utaratibu wa
kuidhinisha
matumizi ya
fedha
zilizomo
katika
Mfuko
Mkuu wa
Hazina ya
Serikali.
208.-(1) Rais atatoa maagizo kwa watu wanaohusika kutayarishana
kuwasilisha kwenye Bunge katika kila mwaka wa fedha wa Serikali
makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano
kwa ajili ya kipindi cha mwaka wa fedha unaofuata.
(2) Baada ya Bunge kuyakubali Makadirio ya Matumizi
yaliyoainishwa katika Ibarandogo ya (1) kutawasilishwa kwenye Bunge
Muswada wa Sheria ya Matumizi ya Fedha za Serikali, kwa ajili ya
kuidhinisha matumizi ya fedha kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali
zitakazogharamia shughuli mbalimbali za Serikali zinazohusu makadirio
hayo.
(3) ikiwa katika mwaka wa fedha wowote inaonekana kwamba:
(a) fedha za matumizi zilizoidhinishwa na Sheria ya Matumizi ya
Fedha za Serikali kwa ajili ya kugharamia shughuli fulani
hazitoshi;
(b) imekuwa lazima kulipa gharama za shughuli ambayo
haikupangiwa fedha za matumizi kwa mujibu wa Sheria;
(c) kuna fedha ambazo zimetumiwa kwa ajili ya shughuli fulani
kwa kiasi kinachozidi kiwango cha matumizi yaliyoidhinishwa
na Sheria ya Matumizi ya Fedha za Serikali kuhusu shughuli
hiyo;
(d) fedha zimetumiwa kulipia gharama za shughuli ambayo
haikupangiwa fedha za matumizi kwa mujibu wa Sheria,
kutawasilishwa kwenye Bunge makadirio ya matumizi ya nyongeza au,
kadri itakavyokuwa, maelezo ya matumizi ya ziada, na baada ya Bunge
kuyakubali hayo makadirio ya matumizi ya nyongeza au maelezo ya
matumizi ya ziada, kutawasilishwa kwenye Bunge Muswada wa Sheria ya
Matumizi ya Fedha za Serikali kwa ajili ya kuidhinisha matumizi ya fedha
kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali, na fedha hizo zitagharamia
shughuli zinazohusika na hayo makadirio au maelezo.
Utaratibu wa
kuidhinisha
matumizi ya
fedha kabla
209.-(1) Iwapo mwaka wa fedha wa Serikali umeanza na Sheria ya
Matumizi ya Fedha za Serikali inayohusika na mwaka huo haijaanza
kutumika, Rais anaweza kuidhinisha fedha itolewe kutoka Mfuko Mkuu
‐ 85 ‐
ya Sheria ya
Matumizi ya
Fedha za
Serikali
kuanza
kutumika
wa Hazina ya Serikali kwa ajili ya kugharamia shughuli za lazima za
Serikali, na fedha hizo zitatumiwa mpaka ipite miezi minne tangu mwanzo
wa mwaka wa fedha mpaka Sheria ya Matumizi ya Fedha za
Serikaliitakapoanza kutumika, kutegemea na lipi kati ya mambo hayo
litatokea mapema zaidi.
(2) Bunge linaweza kutunga sheria kwa ajili ya kuweka masharti ya
kuidhinisha matumizi ya fedha kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali
kwa kufuata utaratibu ulioelezwa katika Ibara ndogo ya (1).
Mfuko wa
Matumizi ya
Dharura.
210.-(1) Kutakuwa na Mfuko wa Matumizi ya Dharura ambao
matumizi yake yatawekewa masharti na Sheria itakayotungwa na Bunge.
(2) Sheria iliyotajwa katika Ibara ndogo ya (1) itaruhusu Rais au
Waziri mwenye dhamana ya masuala ya fedha, pale anaporidhika kuwa
kuna:
(a) jambo la haraka na la dharura na ambalo halikutazamiwa
kutokea na ambalo halikupangiwa fedha, kuazima fedha
kutoka Mfuko wa Matumizi ya Dharura kwa ajili ya
kugharamia jambo hilo; au
(b) jambo la haraka na la dharura kama ilivyoelezwa katika aya
ya (a) ya Ibara ndogo ya (2), kutumia fedha zilizotengwa
mahsusi kwa ajili ya kugharamia shughuli fulani kulipia
gharama za jambo hilo.
(3) Iwapo fedha zimeazimwa kutoka Mfuko wa Matumizi ya
Dharura au fedha zilizotengwa mahsusi kwa ajili ya shughuli fulani
zimetumiwa kugharamia jambo la haraka na la dharura, basi
kutawasilishwa kwenye Bunge makadirio ya matumizi ya nyongeza, na
baada ya Bunge kuyakubali makadirio hayo Muswada wa Sheria ya
Matumizi ya Fedha za Serikali utakaowasilishwa kwenye Bunge kwa ajili
ya kuidhinisha matumizi hayo utahakikisha kwamba fedha zozote
zilizoazimwa kwenye Mfuko wa Matumizi ya Dharura zitarudishwa
kwenye Mfuko huo kutoka katika fedha za matumizi yatakayoidhinishwa
na Muswada huo.
Mishahara ya
baadhi ya
watumishi
kudhaminiwa
na Mfuko
Mkuu
211.-(1) Watumishi wa Serikali wanaohusika na masharti ya Ibara
hii watalipwa mishahara na posho kama itakavyoelezwa na sheria
itakayotungwa na Bunge.
(2) Fedha za malipo ya mishahara na posho za watumishi wa
Serikali wanaohusika na masharti ya Ibara hii pamoja na fedha za malipo
ya uzeeni na kiinua mgongo kwa wale wanaostahili malipo hayo miongoni
mwa watumishi hao zitatolewa kutoka Mfuko Mkuu wa Hazina ya
Serikali.
(3) Mshahara anaolipwa mtumishi wa Serikali anayehusika na
masharti ya Ibara hii pamoja na masharti yake ya kazi havitabadilishwa,
baada ya mtumishi huyo kuteuliwa, kwa jinsi ambayo itapunguza maslahi
ya mtumishi huyo, lakini maelezo haya hayahusiki na posho anayolipwa
mtumishi huyo.
(4) Iwapo mtumishi wa Serikali anayehusika na masharti ya Ibara
hii ana hiari ya kuchagua kima cha mshahara au aina ya masharti ya kazi,
‐ 86 ‐
basi kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya Ibara ndogo ya (3),
mshahara wa kima hicho atakaochagua na aina hiyo ya masharti ya kazi
atakayochagua vitahesabiwa kuwa vina maslahi zaidi kwake kuliko kima
cha mshahara kingine chochote ambacho anaweza kuchagua au aina ya
masharti ya kazi nyingine yoyote ambayo angeweza kuchagua.
(5) Masharti ya Ibara hii yatatumika kwa Jaji Mkuu, Naibu Jaji
Mkuu, Jaji wa Mahakama ya Juu, Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani,
Naibu Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani, Jaji wa Mahakama ya
Rufani, Mwenyekiti na Mjumbe wa Tume ya Haki za Binadamu na
watumishi wengine watakaotajwa na sheria itakayotungwa na Bunge.
(b) Deni la Taifa na Mikopo ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano
Deni la Taifa
212.-(1) Deni la Taifa litadhaminiwa na Mfuko Mkuu wa Hazina
ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
(2) Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa Ibara hii, deni la Taifa maana
yake ni deni lenyewe na pia riba inayolipwa juu ya deni hilo, fedha
zinazowekwa akiba kwa ajili ya kulipa deni kwa awamu na gharama zote
zinazoambatana na usimamizi wa deni hilo.
Mamlaka ya
kukopa ya
Serikali ya
Jamhuri ya
Muungano.
213.-(1) Serikali ya Jamhuri ya Muungano itakuwa na mamlaka ya
kukopa fedha ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano kwa ajili ya
kugharamia shughuli zilizo chini ya mamlaka yake.
(2) Bunge linaweza kutunga sheria ambayo:
(a) itaweka masharti ya kuzingatiwa na Serikali wakati wa kukopa;
na
(b) itaweka utaratibu wa Serikali kutoa taarifa Bungeni kuhusu
mikopo.
(3) Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ndogo ya (2)(b), taarifa
itakayowasilishwa Bungeni pamoja na mambo mengine itaeleza:
(a) kiasi cha deni lililopo na riba yake;
(b) matumizi yaliyofanywa au yatakayofanywa kutokana na fedha
za mkopo husika;
(c) utaratibu uliowekwa wa kulipa deni husika; na
(d) hatua iliyofikiwa katika kulipa deni husika.
Mamlaka ya
kukopa
fedha ya
Serikali za
Washirika
wa
Muungano.
214.-(1) Serikali ya Mshirika wa Muungano itakuwa na mamlaka
ya kukopa fedha ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano kwa ajili ya
kugharamia shughuli zilizo chini ya mamlaka yake.
(2) Endapo mkopo utahitaji dhamana, Serikali ya Jamhuri ya
Muungano, baada ya kushauriana na kukubaliana na Serikali ya Mshirika,
inaweza kutoa dhamana kwa mkopo unaoombwa.
(3) Bunge litatunga sheria itakayoweka utaratibu wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano kudhamini mikopo ya Serikali za Washirika wa
Muungano.
(4) Katika kipindi cha miezi mitatu tangu kumalizika kwa mwaka
wa fedha, Serikali itachapisha ripoti katika Gazeti la Serikali itakayoelezea
mikopo iliyodhaminiwa na Serikali katika mwaka wa fedha uliopita.
‐ 87 ‐
(c) Vyanzo vya Mapato ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano na
Manunuzi ya Umma
Vyanzo vya
mapato vya
Serikali ya
Jamhuri ya
Muungano
215. Vyanzo vya mapato ya Serikali ya Jamhuri ya
Muunganovitakuwa:
(a) ushuru wa bidhaa;
(b) maduhuli yatokanayo na taasisi za Muungano;
(c) mchango kutoka kwa Washirika wa Muungano; na
(d) mikopo kutoka ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano.
Manunuzi
ya Umma
216.-(1) Katika kufanya manunuzi ya umma, Serikali na taasisi
zote za umma zitatakiwa kutumia au kuweka mfumo utakaozingatiahaki,
uwazi, maslahi ya umma, uwajibikaji, ushindani na unaozingatia thamani
halisi ya fedha.
(2) Katika kufanya manunuzi ya umma, Serikali na taasisi zake
zitatakiwa kutumia au kuweka mfumo ambao utazingatia kununua bidhaa
zinazozalishwa au huduma zinazotolewa nchini kwa kuzingatia masharti
yaliyoainishwa katika Ibara hii na sheria itakayotungwa na Bunge.
(3) Bunge litatunga sheria itakayoweka masharti ya usimamizi na
udhibiti wa manunuzi ya umma.
(d)Benki Kuu
Benki Kuu
ya Jamhuri
ya
Muungano.
217.-(1) Kutakuwa na Benki Kuu ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania itakayojulikana kuwa “Benki Kuu” ambayo itakuwa na
majukumu yafuatayo:
(a) kutoa sarafu, kudhibiti na kusimamia mzunguko wa sarafu;
(b) kuandaa na kusimamia Sera na Mipango inayohusiana na
sarafu;
(c) kudhibiti na kusimamia masuala ya fedha za kigeni; na
(d) kusimamia Benki za Washirika wa Muungano.
(2) Katika utekelezaji wa majukumu yake, Benki Kuu itakuwa huru
na haitaingiliwa ama kwa kupewa maelekezo au kudhibitiwa na mtu au
mamlaka yoyote.
(3) Bunge litatunga sheria itakayoweka masharti kuhusu muundo wa
Benki Kuu itakayozingatia uwakilishi wa pande zote mbili za Muungano,
mamlaka, shughuli na utendaji wa Benki Kuu.
Benki za
Serikali za
Washirika
218. Serikali za Washirika zitakuwa na Benki zitakazokuwa
najukumu la kutunza akaunti ya fedha za Serikali husika, kusimamia Sera
za Kifedha na benki za biashara katika mamlaka zao.
SURA YA KUMI NA TANO
ULINZI NA USALAMA KATIKA JAMHURI YA MUUNGANO
(a) Ulinzi na Usalama wa Taifa
Usalama
wa Taifa
219.-(1) Jukumu la ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano ni
la kila raia.
‐ 88 ‐
(2) Usalama wa Jamhuri ya Muungano unahusu ulinzi wa mipaka
yote ya eneo la Jamhuri ya Muungano ikiwa ni pamoja na anga na bahari
kuu, watu wake, mali zao,haki, uhuru na maslahi mengine ya kitaifa dhidi
ya vitisho vya ndani na nje.
(3) Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano utaimarishwa na
kuhakikishwa kulingana na kanuni zifuatazo-
(a) usalama wa taifa unaongozwa na mamlaka ya Katiba hii na
Bunge;
(b) usalama wa taifa utatekelezwa kwa kuzingatia sheria, ikiwemo
sheria za kimataifa, na kwa kuheshimu kikamilifu utawala wa
kisheria na haki za binadamu; na
(c) taasisi za usalama wa Taifa zitaheshimu utamaduni wa aina
mbalimbali wa jamii katika kutekeleza majukumu yake.
Taasisi za
Ulinzi na
Usalama
wa Taifa.
220.-(1) Taasisi za ulinzi na usalama wa Taifa ni-
(a) Jeshi la Wananchi wa Tanzania;
(b) Jeshi la Polisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; na
(c) Idara ya Usalama wa Taifa.
(2) Lengo la kimsingi la taasisi za ulinzi na usalama wa Taifa na
mfumo wa usalama ni kulinda maslahi ya raia na watu wengine na mali zao
na haki na uhuru, na mamlaka, amani, umoja wa kitaifa na mipaka ya
Jamhuri ya Muungano.
(3) Katika utekelezaji wa majukumu yao, taasisi za ulinzi na
usalama wa taifa na kila mtumishi wa taasisi hizo hataruhusiwa-
(a) kuwa na upendeleo kwa njia yoyote;
(b) kuendeleza maslahi ya chama chochote cha kisiasa au sera zake;
(c) kuhujumu maslahi ya kisiasa au mpango wa kisiasa ambao ni
halali chini ya Katiba hii;
(d) kutishia, kudhulumu au kuwatendea raia ukatili; na
(e) kutii amri yoyote isiyokuwa halali.
(4) Mtu hataruhusiwa kuanzisha taasisi, kampuni, jumuiya au
shirika linalohusiana na ulinzi na usalama wa taifa au ushirika wa kijeshi,
isipokuwa kama inavyoruhusiwa na Katiba hii au sheria ya Bunge.
(5) Taasisi za ulinzi na usalama wa Taifa zitakuwa chini ya
mamlaka yaRais.
(6) Rais anaweza kuunda chombo cha ulinzi na usalama kwa
kushauriana na Baraza la Ulinzi na Usalama la Taifa.
(7) Bunge litatunga sheria kuweka masharti kuhusu utekelezaji wa
majukumu, utaratibu na usimamizi wa taasisi za ulinzi na usalama wa Taifa.
Kuanzishwa
kwa Baraza
la Ulinzi na
Usalama
wa Taifa.
221.-(1) Kutakuwa na Baraza la Ulinzi na Usalama wa Taifa
litakalokuwa na wajumbe wafuatao-
(a) Rais wa Jamhuri ya Muungano;
(b) Makamu wa Rais;
(c) Rais wa Tanzania Bara;
(d) Rais wa Zanzibar;
(e) Waziri mwenye dhamana na ulinzi;
‐ 89 ‐
(f) Waziri mwenye dhamana ya mambo ya ndani ya nchi;
(g) Waziri mwenye dhamana na mambo ya nje;
(h) Waziri mwenye dhamana na usalama wa taifa;
(i) Waziri mwenye dhamana ya fedha;
(j) Mwanasheria Mkuu wa Serikali;
(k) Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania;
(l) Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa; na
(m) Mkuu wa Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
(2) Mwenyekiti anaweza kumwalika mtu yeyote anayeshika nafasi
ya madaraka katika taasisi za Serikali, Bunge au Mahakama kushiriki katika
kikao cha Baraza la Usalama wa Taifa.
(3) Kutakuwa na Sekretarieti ya Baraza la Ulinzi na Usalama la
Taifa itakayoongozwa na Katibu Mkuu Kiogozi.
(4) Vikao vya Baraza la Ulinzi na Usalama la Taifa vitaongozwa na
Rais, endapo kama Rais hayupo vitaongozwa na Makamu wa Rais.
(5) Baraza la Ulinzi na Usalama la Taifa litaweka utaratibu wa
mwenendo wa vikao vyake.
(6) Bunge litatunga sheria itakayoweka masharti kuhusu utekelezaji
wa majukumu ya Baraza la Ulinzi na Usalama la Taifa.
Majukumu
ya Baraza
la Ulinzi na
Usalama
la Taifa.
222.-(1) Baraza la Ulinzi na Usalama wa Taifa litakuwa na jukumu
la-
(a) kuunganisha sera za ndani, sera za kigeni na za kijeshi
kuhusiana na usalama wa Taifa ili kuwezesha taasisi za ulinzi
na usalama wa Taifa kushirikiana kikamilifu;
(b) kutathmini na kuchunguza malengo, kujitoleana hatari kwa
Taifa kuhusiana na usalama wa nchi; na
(c) kuanzisha sera kuhusu masuala ya maslahi ya pamoja ya
kiusalama ya taasisi za kiusalama na kudhibiti taasisi hizo.
(2) Rais atatoa taarifa kwa Bunge kila mwaka kuhusiana na hali ya
usalama katika Jamhuri ya Muungano.
(b)Jeshi la Wananchi wa Tanzania
Kuanzishwa
kwa Jeshi
la
Wananchi
wa
Tanzania.
223.-(1) Kutakuwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania litakalokuwa
na mamlaka ya kusimamia ulinzi na usalama wa wananchi na mipaka ya
Jamhuri ya Muungano.
(2) Rais anaweza kuanzisha vikosi vingine vya Jeshi la Wananchi
wa Tanzania kama atakavyoona inafaa.
Uteuzi wa
Mkuu wa
Majeshi
224. Kutakuwa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ambaye atateuliwa
na Rais baada ya kushauriana na Baraza la Ulinzi na Usalama la Taifa.
Madaraka
ya Amiri
Jeshi Mkuu
225.-(1) Bila ya kuathiri masharti yatakayowekwa na sheria yoyote
iliyotungwa na Bunge, miongoni mwa madaraka ya Rais akiwa Amiri Jeshi
Mkuu ni kuyaamuru majeshi ya nchi yatende mambo yanayohusika na vita
vya ulinzi wa Jamhuri ya Muungano, mambo ya kuokoa maisha na mali ya
‐ 90 ‐
watu katika hali ya hatari na mambo mengineyo ambayo Amiri Jeshi Mkuu
ataona inahitajika, na kwa ajili hiyo Amiri Jeshi Mkuu anaweza kuyaamuru
majeshi hayo yatekeleze mambo hayo ama ndani au nje ya Tanzania.
(2) Bila ya kuathiri masharti yatakayowekwa na sheria iliyotungwa
na Bunge, madaraka juu ya mambo yafuatayo yatakuwa mikononi mwa
Amiri Jeshi Mkuu-
(a) madaraka ya kuwateua viongozi katika majeshi ya ulinzi ya
Jamhuri ya Muungano;
(b) madaraka ya kuwateua wanajeshi watakaoongoza vikosi mbali
mbali vya majeshi ya ulinzi; na
(c) madaraka ya kumwamuru mwanajeshi yeyote asitumie
madaraka yoyote aliyokabidhiwa na ambayo yanaambatana na
kuwa kwake mwanajeshi.
(3) Jambo lolote atakalotenda mwanajeshi yoyote kinyume cha amri
iliyotolewa na Amiri Jeshi Mkuu kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo
ya (1) na (2) ya ibara hii litakuwa batili.
Tume ya
utumishi ya
Jeshi la
Wananchi
wa
Tanzania
226.-(1) Kutakuwa na Tume ya Utumishi ya Jeshi la Wananchi wa
Tanzania itakayokuwa na jukumu la kusimamia masuala yote ya utumishi
wa wanajeshi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania na vikosi vyake.
(2) Bunge litatunga sheria itakayoweka masharti kuhusu muundo,
majukumu na mambo mengine yanayohusu Tume ya Utumishi ya Jeshi la
Wananchi wa Tanzania.
(c) Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano
Jeshi la
Polisi la
Tanzania
227.-(1) Kutakuwa na Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano
litakalokuwa na jukumu la ulinzi wa watu na mali zao chini ya masharti ya
Katiba hii.
(2) Bunge litatunga sheria kuweka masharti ya utekelezaji wa kazi
na majukumu ya Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano kwa kuzingatia
haki za raia na sheria za kimataifa.
Misingi ya
utendaji wa
Jeshi la
Polisi
228. Katika utekelezaji wa majukumu yake, Jeshi la Polisi la
Jamhuri ya Muungano litazingatia-
(a) viwango vya juu vya kitaaluma na nidhamu miongoni mwa
wafanyakazi wake;
(b) ulinzi na ukuzaji wa haki za binadamu;
(c) kanuni za uwazi na uwajibikaji;
(d) kuzuia rushwa na ufisadi; na
(e) kukuza mahusiano na jamii.
Uteuzi wa
Mkuu wa
Jeshi la
Polisi
229. Kutakuwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano
ambaye atateuliwa na Rais baada ya kushauriana na Baraza la Ulinzi na
Usalama wa Taifa.
Tume ya
Utumishi
ya Jeshi la
Polisi
231.-(1) Kutakuwa na Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi
itakayokuwa na jukumu la kusimamia masuala yote ya utumishi wa Jeshi la
Polisi na idara zake.
(2) Katika suala la uajiri wa maofisa na watumishi wengine wa Jeshi
‐ 91 ‐
la Polisi, Tume ya Utumishi waJeshi la Polisi itazingatia Kanuni na Misingi
ya Utumishi iliyoainishwa katika Katiba hii.
(3) Bunge litatunga sheria kuweka masharti ya muundo na
utekelezaji wa kazi na majukumu ya Tume ya Utumishi waJeshi la Polisi.
Polisi wa
Washirika
wa
Muungano.
232.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, nchi washirika wa
Muungano wanaweza kuanzisha vikosi vya ulinzi vitakavyosimamia
masuala ya usalama wa watu na mali katika maeneo yao.
(2) Vikosi vya ulinzi vya Washirika wa Muungano, vitatekeleza
majukumu yao kwa ushirikiano na Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano
ili kuepusha mgongano wa mamlaka katika utekelezaji wa majukumu
katika maeneo hayo.
(d) Idara ya Usalama wa Taifa ya Jamhuri ya Muungano
Kuanzishwa
kwa Idara ya
Usalama ya
Taifa.
233.-(1) Kutakuwa na Idara ya Usalama wa Taifa ya Jamhuri ya
Muungano.
(2) Idara ya Usalama ya Jamhuri ya Muungano itahusika na
shughuli za kuimarisha usalama wa Jamhuri ya Muungano na kulinda
Katiba hii, maslahi ya Taifa na ya watu na itatekeleza majukumu mengine
kama yatakavyoainishwa na Sheria itakayotungwa na Bunge.
Uteuzi wa
Mkurugenzi
wa Idara ya
Usalama wa
Taifa.
234.- Rais, baada ya kushauriana na Baraza la Ulinzi na Usalama la
Taifa, atamteua Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa.
Usalama
wa
Washirika
wa
Muungano
235. Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, Washirika wa
Muungano wanaweza kuanzisha Idara au Taasisi zitakazoshughulika na
mambo ya kiusalama katika mamlaka zao ambazo zitafanya na kutekeleza
majukumu yao kwa kushirikiana na Idara ya Usalama ya Jamhuri ya
Muungano.
SURA YA KUMI NA SITA
MENGINEYO
Masharti
kuhusu
utaratibu
wa
kukabidhi
madaraka
236.-(1) Mtu yeyote mwenye dhamana ya kazi yoyote iliyoanzishwa
na Katiba hii pamoja na kazi ya Waziri, Naibu Waziri au Mbungeanaweza
kujiuzulu kwa kutoa taarifa iliyoandikwa na kutiwa saini kwa mkono wake,
kwa kufuata masharti yafuatayo:
(a) iwapo mtu huyo aliteuliwa au kuchaguliwa na mtu mmoja,
basi taarifa hiyo ya kujiuzulu atawasilisha kwa mtu huyo
aliyemteua au aliyemchagua, au iwapo aliteuliwa au
kuchaguliwa na kikao cha watu, basi taarifa hiyo ya kujiuzulu
ataiwasilisha kwenye kikao hicho;
(b) iwapo mtu huyo ni Rais, basi taarifa hiyo ya kujiuzulu
ataiwasilisha kwa Spika;
(c) iwapo mtu huyo ni Spika au Naibu Spika wa Bunge, basi
‐ 92 ‐
taarifa hiyo ya kujiuzulu ataiwasilisha kwenye Bunge; na
(d) iwapo mtu huyo ni Mbunge, basi taarifa hiyo ya kujiuzulu
ataiwasilisha kwa Spika.
(2) Mtu aliyetoa taarifa ya kujiuzulu kwa mujibu wa masharti ya
Ibara ndogo ya (1), atahesabiwa kuwa amejiuzulu tangu siku ile ambayo
taarifa yake ya kujiuzulu itakapopokelewa na mtu anayehusika au kikao
kinachohusika na itakapopokelewa na mtu yeyote aliyeruhusiwa kuipokea
taarifa hiyo na mtu anayehusika au kikao kinachohusika, lakini kama taarifa
hiyo ya kujiuzulu imeeleza kwamba mtu huyo atajiuzulu tangu siku
nyingine baada ya taarifa hiyo kupokelewa na mtu anayehusika au kikao
kinachohusika, basi mtu huyo atahesabiwa kuwa amejiuzulu tangu siku
hiyo nyingine ya baadaye.
(3) Endapo mtu yeyote mwenye dhamana ya kazi yoyote
iliyoanzishwa na Katiba hii, pamoja na kazi ya Waziri, Naibu Waziri au
Mbunge, amejiuzulu, basi ikiwa anazo sifa zote zinazohitajika na kwa kila
hali anastahili, anaweza kuteuliwa au kuchaguliwa tena kushika madaraka
ya kazi hiyo kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.
(4) Masharti yaliyomo katika Ibara ndogo ya (3) hayatamzuia mtu
ambaye ni Rais kuchaguliwa tena kuwa Rais wakati bado ameshika
madaraka ya kazi ya Rais.
Masharti
kuhusu
madaraka
ya kazi
237.-(1) Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya Katiba hii
kuhusu utaratibu wa kukabidhi madaraka ya kazi katika utumishi wa
Serikali ya Jamhuri ya Muungano, ifahamike kuwa mtu yeyote mwenye
mamlaka, kwa mujibu wa Katiba hii, ya kumteua mtu mwingine kushika
madaraka ya kazi pia atakuwa na uwezo wa kumteua kaimu au mtu ambaye
atashika kwa muda na kutekeleza madaraka ya kazi hiyo:
Isipokuwa kwamba maelezo hayo hayatatumika kwa madaraka ya
kazi ya Waziri, Naibu Waziri, Jaji wa Mahakama ya Juu, Jaji wa
Mahakama ya Rufani, Mjumbe wa Tume yaMaadili ya Uongozi na
Uwajibikaji au Mjumbe wa Tume Huru ya Uchaguzi.
(2) Kanuni zifuatazo zitatumika pia kwa madhumuni ya ufafanuzi
wa masharti ya Katiba hii kuhusu utaratibu wa kukabidhiana madaraka ya
kazi katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano, yaani:
(a) iwapo kuna mtu mwenye madaraka ya kazi aliyokabidhiwa kwa
mujibu wa masharti ya Katiba hii na mtu huyo yupo likizo na
wakati huo huo anangojea kuacha kazi hiyo, basi anaweza
kuteuliwa mtu mwingine na kukabidhiwa madaraka ya kazi
hiyo, bila ya kujali kuwapo kwa yule mtu anayengojea kuacha
kazi hiyo;
(b) iwapo kuna watu wawili au zaidi ambao kwa wakati mmoja
wote wanashika madaraka ya kazi fulani kutokana na uteuzi
wao uliofanywa kwa mujibu wa Kanuni iliyoelezwa katika aya
ya (a) ya Ibara hii ndogo, basi katika hali hiyo kukitokea haja ya
kutekeleza shughuli yoyote inayohusika na madaraka ya kazi
hiyo yule mtu wa mwisho kuteuliwa ndiye atakayehesabiwa
kuwa mtu pekee mwenye dhamana ya kazi hiyo; na
(c) iwapo mtu ameteuliwa, kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii,
kuwa kaimu au kushikilia madaraka ya kazi fulani wakati mtu
‐ 93 ‐
maalum aliyeteuliwa kushika madaraka ya kazi hiyo
anashindwa kutekeleza shughuli zinazohusika na kazi hiyo, basi
haitaruhusiwa kufanya uchunguzi wowote au kutoa hoja yoyote
juu ya uteuzi wa huyo kaimu kwa sababu mtu huyo maalum
aliyeteuliwa kushika madaraka ya kazi hiyo ameshindwa
kutelekeza shughuli zinazohusika na kazi hiyo.
Ufafanuzi 238.-(1) Katika Katiba hii, isipokuwa kama itaelezwa vinginevyo:
“amri ya Jeshi” maana yake ni sheria au amri iliyotolewa kwa mujibu wa
sheria, ya kusimamia nidhamu katika jeshi;
“askari” likitumika kuhusiana na jeshi lolote, maana yake ni pamoja na
askari yeyote ambaye kwa mujibu wa amri ya jeshi hilo ni mtu
anayewajibika kinidhamu;
“Bunge” maana yake ni Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
lililoanzishwa katika Ibara ya 105;
“Chama cha Siasa” maana yake ni chama cha Siasa kilichoandikishwa kwa
mujibu wa sheria za nchi;
“Jamhuri ya Muungano” maana yake ni Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania;
“Jaji Mkuu” maana yake ni Jaji Mkuu wa Mahakama ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania aliyeteuliwa katika Ibara ndogo ya 151
ambaye inajumuisha Kaimu Jaji Mkuu;
“Jeshi” maana yake ni lolote kati ya majeshi ya ulinzi na ni pamoja na jeshi
lolote jingine lililoundwa na Katiba hii au kwa mujibu wa sheria na
linalotawaliwa kwa amri ya jeshi;
“Jumuiya ya Madola”maana yake ni jumuiya ambayo wanachama wake ni
Jamhuri ya Muungano na kila nchi ambayo inahusika na masharti ya
Sheria ya Uraia;
“madaraka ya kazi katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano"
maana yake itabidi ifahamike kwa mujibu wa maana ya kawaida ya
maneno hayo na ni pamoja na utumishi katika Majeshi ya Ulinzi ya
Jamhuri ya Muungano na katika Jeshi la Polisi au jeshi linginelo
lililoundwa kwa mujibu wa Sheria;
“mahakama” maana yake ni mahakama yoyote yenye mamlaka katika
Jamhuri ya Muungano isipokuwa mahakama iliyoundwa kwa amri ya
jeshi;
“Mwanasheria Mkuu” maaana yake ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya
Jamhuri ya Muungano aliyeteuliwa chini ya masharti ya Ibara ya 97;
“Raia” maana yake Raia wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa masharti
ya Katiba hii na sheria za nchi;
“Serikali” maana yake ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano na mtu yeyote
anayetekeleza madaraka au mamlaka yoyote kwa niaba ya Serikali;
“Tanzania Bara” maana yake ni eneo lote la Jamhuri ya Muungano ambalo
zamani lilikuwa eneo la Jamhuri ya Tanganyika;
“Zanzibar” maana yake ni eneo lote la Jamhuri ya Muungano ambalo zamani
lilikuwa eneo la Jamhuri ya Watu wa Zanzibar;
“Uchaguzi Mkuu” maana yake ni uchaguzi wa Rais na uchaguzi wa
Wabunge wanaowakilisha majimbo ya uchaguzi unaofanywa baada
ya Bunge kumaliza muda wake;
‐ 94 ‐
“Waziri” maana yake ni mtu aliyekabidhiwa madaraka ya kazi ya Waziri,
isipokuwa Naibu Waziri;
(2) Kanuni zifuatazo zitatumika kwa madhumuni ya ufafanuzi wa
masharti ya Katiba, yaani -
(a) kila yanapotajwa madaraka ya Rais, ifahamike kuwa madaraka
yanayohusika ni pamoja na mamlaka ya kutekeleza shughuli za kazi
mbalimbali na vile vile wajibu wa kutekeleza shughuli na kazi mbali
mbali kama Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano, na pia
mamlaka mengine kama hayo au wajibu mwingine kama huo ikiwa
imeelezwa katika Katiba hii au katika sheria nyingine yoyote
kwamba mamlaka hayo mengine ni ya Rais au kwamba wajibu huo
mwingine ni wa Rais;
(b) kila yanapotajwa madaraka ya kazi katika utumishi wa Serikali,
ifahamike kuwa kazi inayohusika ni kazi katika Utumishi wa
Serikali ya Jamhuri ya Mungano isipokuwa kama imeelezwa
vingine, na kila inapotajwa Idara ya Serikali ifahamike kuwa idara
inayohusika ni idara ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano,
isipokuwa kama imeelezwa vingine;
(c) iwapo kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii kuna jambo lolote
linalotakiwa litekelezwe au lishughulikiwe na chama chochote cha
siasa, basi, jambo hilo litatekelezwa au litashughulikiwa na chama
hicho kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na chama hicho kwa ajili
hiyo, na pia kwa kuzingatia masharti ya Katiba hii au Sheria yoyote
iliyotungwa na Bunge kwa ajili hiyo;
(d) kwa madhumuni ya Katiba hii, mtu hatahesabiwa kuwa ana
madaraka ya kazi katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya
Muungano kwa sababu tu kwamba anapokea malipo ya uzeeni au
malipo mengine ya aina hiyo kwa ajili ya utumishi wake wa zamani
katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano au katika Jeshi la Ulinzi au
la Polisi la Serikali ya Jamhuri ya Muungano au Serikali ya zamani
ya Zanzibar;
(e) katika Katiba hii, isipokuwa kama maelezo yahitaji vingine, kila
anapotajwa mtu mwenye dhamana ya kazi kwa kutaja madaraka ya
kazi yake, ifahamike kuwa mtu anayehusika ni pamoja na mtu
yeyote ambaye ni Kaimu au aliyeteuliwa kihalali kushikilia
dhamana ya kazi hiyo;
(f) katika Katiba hii, kila yalipotajwa mamlaka ya kumwondoa mtu
katika madaraka ya kazi katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya
Muungano, ifahamike kuwa mamlaka yanayohusika ni pamoja na
mamlaka yaliyotolewa kwa mujibu wa masharti ya Sheria yoyote
yanayomtaka mtu huyo au yanayomruhusu mtu huyo kustaafu:
Isipokuwa kwamba maelezo ya Kanuni hii yasifahamike kuwa
yanampa mtu yeyote mamlaka ya kumtaka Jaji wa Mahakama au
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu astaafu; na
(g) katika Katiba hii, kila ilipotajwa sheria ambayo inabadilisha au
kufuta sheria nyingine, ifahamike kuwa sheria inayohusika ni
pamoja na sheria ambayo inarekebisha sheria hiyo nyingine au
ambayo inaendeleza kutumika kwa hiyo sheria nyingine, ama bila
mabadiliko au baada ya kubadilishwa au kurekebishwa; au sheria
‐ 95 ‐
________________
NYONGEZA
[Imetajwa katika Ibara ya 60]
Mambo ya Muungano
________________
1. Katiba na mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
2. Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
3. Uraia na Uhamiaji;
4. Sarafu na Benki Kuu;
5. Mambo ya Nje;
6. Usajili wa Vyama vya Siasa; na
7. Ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na
mambo ya Muungano.
ambayo inaweka masharti mapya katika sheria nyingine.
Jina la
Katiba na
kuanza
kutumika.
239.-(1) Jina kamili la Katiba hii ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania ya mwaka 2013.
(2) Katiba hii itaanza kutumika mara baada ya kuzinduliwa Rasmi
na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kufutwa
kwa Katiba
ya Jamhuri
ya
Muungano
ya mwaka
1977.
240. Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 inafutwa na
itaacha kutumika mara baada ya kuanza kutumika kwa Katiba hii.

No comments:

Post a Comment