Advertise with Us

Advertise with Us

DHall

DHall

Pages

January 11, 2014

Waziri mkuu wa zamani wa Israel Ariel Sharon afariki dunia!

Ariel Sharon enzi za Uhai wake

Ariel Sharon ambaye amekuwa kwenye umahututi kwa miaka nane.
Hali yake ilizidi kuzorota katika siku za karibuni na kufanya baadhi ya viungo vyake kushindwa kufanya kazi ikiwemo figo zake. Amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 85 baada ya kuugua ugonjwa wa kupooza toka mwaka 2006 wakati akiwa kwenye zama za juu za maisha yake ya kisiasa.
Ariel Sharon ni mtu muhimu kwenye historia ya taifa la Israel tangu akiwa jenerali wa jeshi na baadaye mwanasiasa.
Lakini atasalia kiongozi aliyekuwa na utatanishi mkubwa.

No comments:

Post a Comment