Advertise with Us

Advertise with Us

DHall

DHall

Pages

March 11, 2013

ALIYEKUWA AKITAPELI WATU MTANDAONI KWA JINA LA RAFIKIELIMU AJULIKANA!

Hashim  Mkane,  mwenye  namba 0765283703  tapeli  wa  mtandaoni, aliyewatapeli  makumi  ya  wananchi  kwa  jina  la  RafikiElimu  akiwahadaa  kuwapatia  kazi  katika  taasisi  mbalimbali.

 

Habari kwa hisani ya http://rafikielimu.blogspot.com/

Hatimaye  yule  tapeli  sugu  wa  mtandaoni  aliyekuwa  akiwatapeli  wananchi  mbalimbali  kwa  jina  la  RafikiElimu  akiwahadaa  kuwapatia  ajira  ajulikana . 

INAPOTOKA :   Mnamo  siku  ya  tarehe  11  Machi  2013, tuliripoti  kupitia  blogu  yetu  na  katika  blogu  mbalimbali  nchini  kuhusu  kuwepo  kwa  mtu  anaye  watapeli  wananchi  fedha  kwa  kutumia  jina  la  taasisi  yetu.  Tapeli  huyu  asiye  na  hata  chembe  ya  huruma  kwa  masikini  wenzake, aliweka  tangazo  katika  mtandao  wa  Zoom  Tanzania, mnamo  mwanzoni  mwa  mwezi  February  2013  akitangaza  nafasi  za  kazi z a  kuvolunteer  katika  mikoa  mbali mbali  ya  Tanzania  bara.  Baada  ya  watu  kutuma  maombi  yao, tapeli  huyo  aliyekuwa  akijitambulisha  kwa  jina  bandia  la  EMMANUEL  ALBERT  na  kwamba  yeye  ni  HR  wa  RafikiElimu,  aliwaambia  kuwa  wamepata  nafasi, na  kuwatumia   fomu  za  kujaza  kisha kuwataka  wamtumie  shilingi  elfu Tano ( Tshs. 5,000/=)  za  kitanzania  kwa  mpesa  kwenda  namba   0763906931  ( AMBAYO  MBAYA  ZAIDI  AMEISAJILI  KWA  JINA  LA  RAFIKIELIMU) Baada  ya  kumtumia  pesa , tapeli  huyo  aliwatumia  barua  na  kuwaagiza  kuripoti  kazini  katika  taasisi  mbalimbali, huku  mmoja  kati  yao  akimuagiza  aje  kuripoti  katika  ofisi  zetu.

Tulibaini  juu  ya  uwepo  wa  utapeli  huu  mara  baada  ya  kutembelewa  na  mmoja  kati  ya  wahanga  wa  utapeli  huo.   Dada  huyo  aliye jitambulisha  kwa  jina  la   HAWA  MUSSA  ambaye  ni  Muhitimu  wa  Chuo  Kikuu  Cha  Dodoma  ( 2012 )  aliripoti  katika  ofisi  zetu  siku  ya  tarehe  11  Machi  2013  saa  nne  kamili  asubuhi  na  kuomba  kumuona  HR . Baada  ya  kufanya  naye  mazungumzo  ndipo  tulipo  baini  kuwepo  kwa  utapeli  unao  fanyika  kwa  jina  la  taasisi  yetu. Haraka  haraka  tukaenda  kuripoti  uhalifu  huu  kwenye  kituo  kidogo  cha  polisi  cha  Chuo  Kikuu  Cha  Dar  Es salaam, na  kukabidhiwa  RB namba   UD/RB/849/2013  WIZI  KWA  NJIA  YA  MTANDAO.

Mara  baada  ya  kupata  RB  moja  kwa  moja  tulipost    taarifa   ya  kuwatahadharisha  wananchi  juu  ya  uwepo  wa  mtu  anaye  tapeli  watu  kwa  kutumia  jina  la  taasisi  yetu,  huku  tukiwaachia  polisi  na  kazi  ya  uchunguzi  wa  tukio  hili  la  uhalifu.  Wakati  polisi  wakiwa  bado  wanaendelea  na  uchunguzi, siku  ya  Jumatatu  ya  jana,  tarehe  11  Machi  2013  saa  sita  kamili  asubuhi, tulipokea  simu  kutoka  kwa  mwakilishi  wetu  wa  Mwanza, Dada  HADIJA  SEJA  akiomba  tumpe  namba  za  " MR. EMMANUEL  ALBERT "  (  HR  wa  RafikiElimu   Foundation  ).. Kwa  kuwa  tayari  tulikuwa  na  taarifa  za  jina  hilo, tulimuomba  dada   Hadija  Seja  atutaarifu  kitu  gani  kimetokea. Dada  Hadija  alitupa  taarifa  ya  kusikitisha  sana, kwamba  kuna  mtu  mmoja  aliyemtaja  kwa  jina  moja tu  la  Gerlad  kutoka  Arusha, amewasili  jijini  Mwanza  kuripoti  katika  ofisi  za  taasisi  ya  RESTLESS  DEVELOPMENT  kwa  ajili  ya  kuanza  kazi. Mtu  huyo  naye  ni  muhanga  wa  tapeli  huyu, na  baada  ya  kumtumia  tapeli  huyo  sh. elfu  tano, tapeli  alimuagiza  aende  kuripoti  jijini   Mwanza  katika  ofisi  za  RESTLESS  DEVELOPMENT (mabazo  kimsingi  hazipo  Mwanza)  Can  You  imagine, huu  ni  unyama  wa  kiwango  gani, kumfanyia  masikini  mwenzako  ushenzi  kama  huo?

 Baada  ya  kupata  taarifa  hii, moja  kwa  moja  tukaamua  sisi  wenyewe  kama  taasisi  kwenda  katika  ofisi  za  VODACOM  makao  makuu  zilizopo  Mlimani  City  ili  kuweza  kumbaini  mtu  anaye  fanya  unyama  huu
Tunashukuru  sana  Mungu, Vodacom  walitupa  ushirikiano  wa  kutosha..  Kutoka   kwenye  database  za  Vodacom, tuligundua  kwamba, mtumiaji  wa    0763906931  anaishi  Njombe.  Namba  hii  imesajiliwa  MPESA  tarehe  02  February  2013, hakusajili  kwa  kitambulisho  chake  halisi, bali  kwa  barua  kutoka  kwa   Mwenyekiti  wa  Serikali  za  Mitaa.  Alisajili  akiwa  NJOMBE  na  alipokea  simu  nyingi  sana.  Zaidi  ya  watu  kumi  waliingia  katika  mkenge  wake  na  kumtumia  hizo  shilingi  Elfu  Tano.

Mwanzoni  alikuwa  ana toa  hela  zake  kwa  wakala  ambaye  alisajilia  namba  hii, lakini  baadaye  alisafiri  na  kwenda    tarafa  nyingine  hivyo  basi  kushindwa  kutoa  hela  kwa  sababu   namba  ameisajili  kwa  jina  ambalo  sio  lake. Hivyo  basi  ili  kuweza  kutoa  pesa  ilimbidi, ajihamishie  salio  kutoka  katika  namba  076390631  kwenda  kwenye  namba  yake  halisi  ambayo  ni  0765283703. Hapo  ndipo  tulipo  weza  kumbaini  tapeli  huyu.

Jina  la  huyu  mtu  anaitwa  HASHIM  MKANE  na  namba  yake  halisi  ni  0765283703.  Ni  mkaazi  wa  Njombe  na  amehitimu  Chuo  Kikuu  Cha  Sokoine  (SUA) .   Aliwahi  kuomba  nafasi  ya  uwakala  wa  RafikiElimu  katika  wilaya  ya Njombe,  mwezi  Agosti  2012.

Baada  ya  kupata  taarifa  hizi  tuliamua  kutafuta  mbinu  za  kumkamata  kirahisi,ambapo  tulimtumia  barua  pepe, jana  jioni  kisha  ujumbe  mfupi  wa  maneno  (SMS)  tukimwambia  aje  Dar  Es  salaam  kuhudhuria  semina  ya  siku  tano  ya  mawakala  wa  RafikiElimu (Tukamtajia  na  malipo) Nadhani  alistukia  kwamba  huenda  ameshajulikana, akatuma  ujumbe  mfupi  wa  maneno  uliosomeka :

 "   Nashukuru  kwa  taarifa  hii  ingawa  nitashindwa    kuhudhuria  kwa  kuwa  taarifa   imechelewa    kufika na  ukichukulia  mimi  ni  mwajiliwa  wa  taasisi  binafsi  hivyo  kuweza  kupata  ruhusa  kwa   siku  moja    au  mbili  ilihali  tunafanya  evaluation  ya  mradi  ni  ngumu. natumai  kuhudhuria  semina  nyingine  kama  mtaiandaa  " 

Hapa  tukajua  jamaa  ameshastukia  mchezo  na  uwezekano  wa  kumkamata  kwa  njia  hiyo  usingekuwa  rahisi. Hivyo  basi  tumeamua  kuweka    taarifa  hii  mtandaoni  pamoja  na  picha  za  mtuhumiwa  huyu, ili  kwa  yoyote  yule  atakaye  fanikisha  kukamatwa  kwa  mtuhumiwa  huyu  aweze  kupewa   zawadi  nono  ya  shilingi  Laki  Tano  za  kitanzania .  Taarifa  nyingine  zitatumwa  kwenye  magazeti  na  televisheni  ili  iwe  rahisi  kusambaza  ujumbe  kwa  watanzania  wengi  na  hivyo  kurahisisha  kutiwa  hatiani  kwa  dhalimu  huyu . Tafadhali  upatapo  ujumbe  huu, wafahamishe  na  ndugu  jamaa  na  marafiki  zako  woote...

UKIMUONA  MTU  HUYU, TOA  TAARIFA  KATIKA  KITUO  CHOCHOTE  CHA  POLISI  KILICHO  KARIBU  NAWE , KISHA  WASILIANA  NASI  KWA SIMU  0782405936. NA  ENDAPO  TAARIFA  YAKO  ITASAIDIA  KUKAMATWA  KWA   TAPELI HUYU, TUTAKUPATIA   ZAWADI  YA  FEDHA  TASLIMU  ZA  KITANZANIA  SHILINGI  LAKI  TANO ( Tsh. 500,000/ =)..

 

1 comment:

  1. Anonymous6:19 PM

    Huyu jamaa ni mpumbavu...njaa na ujinga wake eti anatapeli buku tano 5 sass zitampeleka wapi??hata mimi niliapply hiyo post kumbe nimeapply ya mpuuzi niliyegraduate nae....mwaka mmoja......mxxxxuuuuu!!

    ReplyDelete