Advertise with Us

Advertise with Us

DHall

DHall

Pages

November 5, 2013

Edward Lowassa ana nguvu ya hoja au nguvu ya pesa?!

Mbunge wa jimbo la Monduli Mhe. Edward Lowassa.

Kwa wale ambao ni wafuatiliaji wazuri wa mambo ya Kisiasa hususani ya nchini Tanzania mtakubaliana na mimi kwamba licha ya changamoto kadhaa alizozipitia katika miaka michache iliyopita akiwa kama Waziri Mkuu wa Tanzania aliyelazimika kujiuzulu kutokana na kashfa ya ufisadi ni wazi kwamba Lowassa bado ana Nguvu sana, Dakika5 tu alizoongea Bungeni jana zilitosha kubadili uelekeo wa vyombo vya habari nchini... habari ya Division Five ikawekwa pembeni, shinikizo la Spika kujiuzulu ikatupwa kule, Zitto vs Lema ikawekwa kando na vyombo vyote vya habari vikawa vikimzungumzia yeye.

Media karibu zote haswahaswa magazeti yalikabadili upepo wa habari na kuzungumzia kile Lowassa alichokizungumza jana Bungeni kwa muda mfupi tu ambao unakadiriwa kuwa si zaidi ya dakika5, sasa sijui kama Lowassa angeongea kwa masaa mawili ingekuaje! 


Swali ninalotaka kuliuliza ni hili: Edward Lowassa ana nguvu ya hoja au nguvu ya pesa??

Tukiachilia mbali Vituo vya Redio na Television haya ni baadhi tu ya Magazeti ambayo yaliripoti habari katika ukurasa wake wa mbele kuhusiana na Mhe. Edward Lowassa.

Edward Lowassa anatajwa kuwa mmoja ya watu wenye nguvu kubwa sana ya kiushawishi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye kwa harakati na mitazamo yake kuna kila hali kwamba yeye ni moja ya watu kadhaa wanaotajwa kuwa katika nafasi za mbele kabisa za kuwania urais kupitia Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi mkuu wa octoba mwaka 2015.

• NIPASHE: EDWARD LOWASSA : VIJANA WATATUNG'OA MADARAKANI.

• MWANANCHI: LOWASSA AKOSOA MPANGO WA MATOKEO MAKUBWA SASA.

• TANZANIA DAIMA: LOWASSA AMVAA KIKWETE.

• JAMBO LEO: LOWASSA AMFYATUA KAGAME.

• RAI: LOWASSA AIPA DARASA SERIKALI.

• MAJIRA: LOWASSA ALIPUKA, AWAVAA VIONGOZI.

• HABARILEO: LOWASSA AITAKA SERIKALI KUAINISHA VIPAUMBELE VICHACHE.

• FAHAMU: LOWASSA vs SUMAYE, MEMBE vs SITTA.

• JAMHURI: KINACHONIFANYA NIMPENDE LOWASSA NI HIKI.


Habari Na: Malisa Godlisten

1 comment:

  1. Anonymous6:18 PM

    Anatumia tu nguvu ya pesa kuhonga media hana jipya.

    ReplyDelete