Advertise with Us

Advertise with Us

DHall

DHall

Pages

November 5, 2013

Zitto Kabwe anaudanganya Umma?! Angalia Risiti hii ya Posho!!


Chini ni maneno ya Zitto kabwe kama alivyopost kwenye ukurasa wake wa Facebook mnamo tarehe 2 November 2013!

"Kuchukua au kutochukua posho za vikao kama mbunge ni suala la misingi (principles) na sio suala la uwezo kifedha. Kuna wabunge matajiri sana lakini wakachukua posho na wengine wa kawaida kabisa hatuchukui posho. Sio posho tu, hata msamaha wa kodi wa kuingia magari nimeukataa sababu ya misingi tu, kwamba siwezi kuwa Waziri kivuli ninayepinga misamaha ya kodi wakati huo huo nikachukua misamaha ya kodi. Ninaamini katika siasa za kutenda ninachosema. Mjadala wa posho kwangu mimi nimeufunga toka Juni 8, 2011 nilipoacha kupokea posho za vikao. Mwaka huo pia nilikataa msamaha wa kodi ya kuingia gari. Ni msimamo tu, hapa mtu hupendi msimamo wangu isiwe uadui, wewe endelea kuchukua posho, omba ziwe nyingi zaidi na wala sitatia neno kwenye msimamo huo japo nitaudharau maana posho za vikao ni kuwaibia wananchi ambao hawana maji safi na salama, watoto wao hawana walimu sababu Serikali haiwalipi walimu vizuri, kina mama waja wazito wanakufa kutokana na huduma mbovu za afya huko vijijini nk. Haya ndio masuala ya wananchi wetu na sio kudai kuongezewa posho.
Zitto Kabwe

Haya ni maneno ya Zitto Kabwe.. Nanukuu tena "Mjadala wa posho kwangu mimi nimeufunga toka Juni 8, 2011 nilipoacha kupokea posho za vikao". Mwisho wa kunukuu.

Kama umesoma kwa makini kile alichokiandika Zitto Kabwe (Kwenye ukurasa wake wa facebook) basi linganisha maelezo yake sambamba na tarehe inayoonekana katika Risiti ya malipo hapo juu

Picha Na: Chanzo chetu

Kupata habari zaidi kuhusiana na harakati za Zitto Kabwe katika kupinga posho Bofya hapa....http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/548888-ushahidi-wa-nyaraka-zinazomuhusu-zitto-zuber-kabwe.html

4 comments:

  1. Anonymous5:54 PM

    huyu zzk anatafuta umaarufu hana kitu

    ReplyDelete
  2. Anonymous5:54 PM

    sema anatumika sio hana kitu

    ReplyDelete
  3. Anonymous6:02 PM

    A Liar.

    ReplyDelete
  4. Anonymous3:50 AM

    He is looking for the cheap popularity

    ReplyDelete